Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 131

Mufalme Mwenye Hana Kosa Anateseka Kwenye Muti

Mufalme Mwenye Hana Kosa Anateseka Kwenye Muti

MATAYO 27:33-44 MARKO 15:22-32 LUKA 23:32-43 YOHANA 19:17-24

  • YESU ANATUNDIKWA KWENYE MUTI WA MATESO

  • ALAMA YENYE KUWEKWA JUU YA KICHWA CHA YESU INAFANYA WATU WAMUCHEKE

  • YESU ANATOA TUMAINI LA UZIMA KATIKA PARADISO DUNIANI

Yesu anapelekwa nafasi moja yenye haiko mbali sana na muji, kwenye yeye na wezi wengine wawili wanapaswa kuuawa. Nafasi hiyo inaitwa Golgota, ao Mahali pa Fuvu la kichwa, na ni mahali penye watu wanaweza kuona “kwa mbali.”—Marko 15:40.

Wanaume hao watatu wenye kuhukumiwa wanatoshwa nguo zao. Kisha divai yenye kuwa na manemane na nyongo yenye kuwa chungu inaletwa. Inaonekana kuwa wanamuke wa Yerusalemu wametengeneza divai hiyo yenye kupunguza maumivu. Na Waroma hawakataze kuipatia wale wenye kutundikwa. Lakini, wakati tu Yesu anaionja, anakataa kabisa kuikunywa. Sababu gani? Anapenda kutumia akili yake yote wakati huu wa jaribu kubwa; anapenda kuwa na uwezo wa kufikiri na kuwa muaminifu mupaka kifo.

Yesu ananyoroshwa kwenye muti wa mateso. (Marko 15:25) Maaskari wanapigilia misumari katika mikono yake na miguu yake, wanatoboa minofu na misuli na hilo linaleta maumivu makali. Wakati muti unasimamishwa, maumivu yanakuwa makali hata zaidi wakati uzito wa mwili wa Yesu unapasua vidonda vyake. Lakini, Yesu hatukane maaskari hao. Anasali hivi: “Baba, wasamehe, kwa maana hawajue jambo lenye wanafanya.”—Luka 23:34.

Waroma wako na zoezi la kuweka alama yenye kuonyesha kosa lenye mutu mwenye kuhukumiwa alifanya. Wakati huu Pilato amewaka alama yenye kuwa na maneno haya: “Yesu Munazareti Mufalme wa Wayahudi.” Yameandikwa katika Kiebrania, Kilatini, na Kigiriki, kwa hiyo, karibu watu wote wanaweza kuisoma. Tendo hilo la Pilato linaonyesha kuwa anachukia Wayahudi wenye walikazia sana ili Yesu auawe. Wakubwa wa makuhani hawafurahie jambo hilo, kwa hiyo wanakataa kwa kusema hivi: “Usiandike, ‘Mufalme wa Wayahudi,’ lakini uandike kwamba alisema, ‘Mimi ni Mufalme wa Wayahudi.’” Lakini kwa sababu Pilato hapendi tena wamuchochee, anajibu hivi: “Maneno yenye nimeandika, nimeyaandika.”—Yohana 19:19-22.

Makuhani hao wenye kukasirika wanarudilia mashitaka ya uongo yenye yalikuwa yametolewa wakati Yesu alikuwa anasambishwa katika Sanhedrini. Haiko jambo la kushangaza kuwa watu wenye kupita katika njia wanatingiza vichwa vyao na kusema hivi kwa kumucheka na kwa zarau: “Aha! Wewe mwenye ulitaka kubomoa hekalu na kulijenga kwa siku tatu (3) jiokoe mwenyewe kwa kushuka kutoka kwenye muti wa mateso.” Vilevile wakubwa wa makuhani na waandishi wanaambiana hivi: “Sasa Kristo, Mufalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka kwenye muti wa mateso, ili tuone na kuamini.” (Marko 15:29-32) Hata wezi wenye walikuwa wametundikwa kwenye upande wa kuume na wa kushoto wa Yesu wanamusema pia, hata kama ni yeye tu ndiye mwenye hana kosa kabisa.

Maaskari ine Waroma wanamucheka pia Yesu. Pengine walikuwa wanakunywa divai yenye kuwa makali, sasa wanamucheka Yesu kwa kuweka divai hiyo mbele yake, lakini Yesu hawezi kuifikia na kunywa. Kwa zarau Waroma wanatumia maneno yenye kuwa juu ya kichwa cha Yesu na kusema hivi: “Kama wewe ndiye Mufalme wa Wayahudi, jiokoe wewe mwenyewe.” (Luka 23:36, 37) Fikiria jambo hili! Mwanaume mwenye ameonyesha wazi kuwa yeye ndiye njia, kweli, na uzima sasa anatendewa kwa zarau na kuchekelewa bila sababu. Lakini anavumilia mambo hayo yote bila kusema jambo lolote juu ya Wayahudi wenye kuangalia, maaskari Waroma wenye kumucheka, ao watenda zambi wawili wenye wametundikwa pembeni yake.

Maaskari hao ine wamekamata nguo za inje za Yesu na kuzigawanya katika vipande ine. Wanapiga kura ili kuona ni nani mwenye atachukua kila kipande. Lakini nguo ya Yesu ya ndani ni ya hali ya juu, “haikukuwa na mushono, ilikuwa imesukwa kuanzia juu mupaka chini.” Maaskari hao wanawaza hivi: “Tusiipasue, lakini tuipigie kura ili kuamua itakuwa ya nani.” Kwa hiyo, wanatimiza andiko lenye kusema hivi: “Waligawana nguo zangu kati yao wenyewe, na wakapigia nguo yangu kura.”—Yohana 19:23, 24; Zaburi 22:18.

Kisha wakati fulani, mwizi mumoja mwenye kutundikwa karibu na Yesu anatambua kuwa Yesu anapaswa kuwa Mufalme kabisa. Anakaripia ule mwingine kwa kumuambia maneno haya: “Je, wewe haumuogope Mungu hata kidogo, kwa kuwa sasa umepata hukumu ileile? Sisi tunastahili kutendewa hivi, kwa maana tunapewa azabu kupatana na makosa yenye tulifanya; lakini mutu huyu hakufanya jambo lolote la mubaya.” Kisha anamuomba Yesu hivi: “Unikumbuke wakati utaingia katika Ufalme wako.”—Luka 23:40-42.

Yesu anajibu hivi: “Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso,” hapana katika Ufalme lakini “katika Paradiso.” (Luka 23:43) Ahadi hiyo iko tofauti na ahadi yenye Yesu ameambia mitume wake, ni kusema, watakaa kwenye viti vya ufalme katika Ufalme wake. (Matayo 19:28; Luka 22:29, 30) Lakini, pengine mutenda zambi huyo Muyahudi alikuwa amekwisha kusikia juu ya Paradiso yenye Yehova alikuwa ametolea Adamu, Eva na wazao wao. Sasa mwizi huyo anaweza kufa na tumaini hilo.