Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 120

Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Marafiki wa Yesu

Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Marafiki wa Yesu

YOHANA 15:1-27

  • MUZABIBU WA KWELI NA MATAWI

  • NAMNA YA KUBAKIA KATIKA UPENDO WA YESU

Yesu ametoka tu kutia wanafunzi wake moyo kwa kuzungumuza nao kwa moyo wote. Ni usiku sana, pengine katikati ya usiku imekwisha kupita. Sasa Yesu anatoa mufano wenye kuchochea:

Anaanza hivi: “Mimi ndiye muzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mulimaji.” (Yohana 15:1) Mufano wake unafanana na mambo yenye yalikuwa yamesemwa mamia ya miaka mbele ya hapo juu ya taifa la Israeli, taifa lenye liliitwa muzabibu wa Yehova. (Yeremia 2:21; Hosea 10:1, 2) Lakini, Yehova anakaribia kukataa taifa hilo. (Matayo 23:37, 38) Kwa hiyo, Yesu anazungumuzia wazo la mupya. Yeye ndiye muzabibu wenye Baba yake amepanda tangu atiwe mafuta kwa roho takatifu katika mwaka wa 29 wakati wetu. Lakini, Yesu anaonyesha kuwa muzabibu unafananisha mambo mengi zaidi, anasema hivi:

“[Baba yangu] anatosha ndani yangu kila tawi lenye halizae matunda, na anasafisha kila tawi lenye linazaa matunda, ili lizae matunda zaidi. . . . Kama vile tawi likiwa peke yake haliwezi kuzaa matunda ikiwa halikae kwenye muzabibu, vilevile ninyi hamuwezi kuzaa matunda ikiwa hamukae katika umoja na mimi. Mimi ndiye muzabibu; na ninyi ndio matawi.”—Yohana 15:2-5.

Yesu ameahidi wanafunzi wake waaminifu kuwa kisha yeye kuenda, atatuma musaidizi, roho takatifu. Kisha siku makumi tano na moja, mitume na watu wengine walipata roho takatifu, na wakakuwa matawi ya muzabibu huo. Na “matawi” yote yalipaswa kubakia katika muungano na Yesu. Ili kutimiza kazi gani?

Anaeleza hivi: “Kila mutu mwenye anakaa katika umoja na mimi, na mimi katika umoja naye, huyo anazaa matunda mengi; kwa maana bila mimi hamuwezi kufanya jambo lolote hata kidogo.” “Matawi” hayo, ni kusema, wanafunzi wake waaminifu wangezaa matunda mengi, kwa kuiga sifa za Yesu, kwa kuhubiria wengine kwa bidii juu ya Ufalme wa Mungu, na kufanya wanafunzi wengi zaidi. Mambo yatakuwa namna gani ikiwa mutu anakosa kubakia katika muungano pamoja na Yesu na kushindwa kuzaa matunda? Yesu anasema hivi: “Kama mutu yeyote hakae katika umoja na mimi, anatupwa inje.” Kwa upande mwengine, Yesu anasema hivi: “Kama munakaa katika umoja na mimi, na maneno yangu yanakaa ndani yenu, muombe kila kitu chenye munataka na kitatendeka kwenu.”—Yohana 15:5-7.

Sasa Yesu anarudilia jambo lenye alikuwa amezungumuzia mara mbili, ni kusema, kushika amri zake. (Yohana 14:15, 21) Anaeleza ni katika njia gani ya maana wanafunzi wake wanaweza kuonyesha kuwa wanafanya hivyo, anasema hivi: “Kama munashika amri zangu, mutabakia katika upendo wangu, kama vile mimi nilishika amri za Baba na ninabakia katika upendo wake.” Lakini, zaidi ya kumupenda Mungu na Mwana wake, wanapaswa kufanya mambo mengine. Yesu anasema hivi: “Hii ndiyo amri yangu, kwamba mupendane kama vile niliwapenda ninyi. Hakuna mwenye iko na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu atoe uzima wake kwa ajili ya marafiki wake. Ninyi ni marafiki wangu kama munafanya mambo yenye ninawaamuru.”—Yohana 15:10-14.

Katika saa kidogo, Yesu ataonyesha upendo wake kwa kutoa uzima wake kwa wale wote wenye kuonyesha imani katika yeye. Mufano wake unapaswa kuchochea wanafunzi wake wakuwe na upendo kama huo wa kujitoa kwa ajili ya mutu na mwenzake. Upendo huo utawatambulisha kama vile Yesu alikuwa amesema: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu—kama muko na upendo kati yenu.”—Yohana 13:35.

Kwa kweli, mitume wanasikia namna Yesu anawaita “marafiki.” Anaeleza sababu gani anawaita hivyo, anasema hivi: “Lakini nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote yenye nilisikia kutoka kwa Baba yangu.” Ni pendeleo kubwa sana kuwa marafiki wa sana wa Yesu na kujua mambo yenye Baba alimuambia! Lakini ili kufurahia urafiki huo, wanapaswa ‘kuendelea kuzaa matunda.’ Ikiwa wanafanya hivyo, Yesu anasema hivi: ‘Jambo lolote lenye munaomba Baba katika jina langu, atawapatia ninyi jambo hilo.’—Yohana 15:15, 16.

Upendo kati ya “matawi” hayo, ni kusema, wanafunzi wake, utawasaidia kuvumilia mambo yenye kuwa mbele. Aliwaonya kuwa ulimwengu utawachukia, lakini aliwatia moyo hivi: “Kama ulimwengu unawachukia ninyi, munajua kwamba umenichukia mimi mbele ya kuwachukia ninyi. Kama mungekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kitu chake. Sasa kwa sababu ninyi hamuko sehemu ya ulimwengu, . . . kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.”—Yohana 15:18, 19.

Yesu anaendelea kueleza sababu gani ulimwengu utawachukia, anasema hivi: “Watawatendea ninyi mambo yote haya kwa sababu ya jina langu, kwa kuwa hawajue Ule mwenye alinituma.” Yesu anasema kuwa kazi zake za miujiza zinahukumu wale wenye kumuchukia. Anasema hivi: “Kama singefanya kati yao kazi zenye hakuna mutu mwingine mwenye alizifanya, hawangekuwa na zambi; lakini sasa wameniona mimi na wamenichukia na wamemutendea Baba yangu vilevile.” Kwa kweli, chuki yao inatimiza unabii.—Yohana 15:21, 24, 25; Zaburi 35:19; 69:4.

Yesu anatoa tena ahadi ya kutuma musaidizi, roho takatifu. Wanafunzi wake wote watapokea roho hiyo yenye kuwa na nguvu na itawasaidia kuzaa matunda, ni kusema, ‘kutoa ushahidi.’—Yohana 15:27.