Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 110

Siku ya Mwisho ya Yesu Kwenye Hekalu

Siku ya Mwisho ya Yesu Kwenye Hekalu

MATAYO 23:25–24:2 MARKO 12:41–13:2 LUKA 21:1-6

  • YESU ANAENDELEA KUHUKUMU VIONGOZI WA DINI

  • HEKALU LITAHARIBIWA

  • MUJANE MASKINI ANATOA MUCHANGO WA FEZA MBILI ZA VICHELE ZENYE SAMANI KIDOGO SANA

Wakati wa mwisho wa Yesu kuonekana kwenye hekalu, anaendelea kufunua unafiki wa waandishi na Wafarisayo, kwa kuwaita waziwazi wanafiki. Anatumia maneno ya mufano, kwa kusema: “Munasafisha upande wa inje wa kikombe na wa sahani, lakini ndani vimejaa pupa na kukosa kujizuia. Mufarisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe na sahani, ili upande wake wa inje ukuwe safi pia.” (Matayo 23:25, 26) Hata kama Wafarisayo wanatilia sana mukazo mambo yenye kuhusu usafi wakati wa karamu na usafi wa mwili, wanapuuza hali ya kiroho na wanashindwa kusafisha moyo wao wa mufano.

Unafiki wao unaonekana pia katika utayari wao wa kujenga na kupamba makaburi kwa ajili ya manabii. Lakini Yesu anaonyesha kama wao ni “wana wa wale wenye waliua manabii.” (Matayo 23:31) Maneno hayo ni ya kweli kwa sababu wanafanya nguvu yao yote ili wamuue Yesu.—Yohana 5:18; 7:1, 25.

Yesu anaonyesha jambo lenye linangojea viongozi hawa wa dini kama hawatubu: “Ninyi nyoka, uzao wa nyoka-vipiri, mutakimbia namna gani hukumu ya Gehena?” (Matayo 23:33) Gehena, ni kusema, Bonde la Hinomu, lenye kuwa karibu linatumiwa ili kuchoma uchafu ao takataka, na ni mahali pa mufano penye kufananisha uharibifu wa milele wenye kuwangojea waandishi na Wafarisayo waovu.

Wanafunzi wa Yesu watamuwakilisha wakiwa “manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.” Watawatendea namna gani? Yesu anaambia viongozi hao wa dini hivi: “Wamoja kati yao [wanafunzi wangu] mutawaua na kuwapigilia misumari kwenye miti, na wamoja kati yao mutawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwatesa katika muji baada ya muji, ili damu yote yenye haina kosa yenye ilimwangwa katika dunia ikuje juu yenu, kuanzia damu ya Abeli mwenye alikuwa bila kosa mupaka damu ya Zekaria . . . mwenye muliua.” Anawaambia hivi: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, mambo yote haya yatafikia kizazi hiki.” (Matayo 23:34-36) Maneno hayo yanatimia katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wakati majeshi ya Waroma yanaharibu Yerusalemu na kuua maelfu ya Wayahudi.

Yesu anahuzunika wakati anakumbuka hali hii yenye kuogopesha. Anasema hivi kwa huzuni: “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na mwenye kupiga majiwe wale wenye walitumwa kwake—ni mara ngapi nilitaka kukusanya watoto wako, kama vile kuku anakusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake! Lakini hamukutaka. Angalia! Mungu ameacha nyumba yenu.” (Matayo 23:37, 38) Wale wenye wanasikia maneno haya wanapaswa kujiuliza ni “nyumba” gani anazungumuzia. Je, alikuwa anazungumuzia hekalu hilo lenye utukufu la Yerusalemu, lenye linaonekana kuwa ni lenye kulindwa na Mungu?

Kisha Yesu anaongeza hivi: “Ninawaambia ninyi, tangu sasa hamutaniona tena mupaka wakati mutasema, ‘Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!’” (Matayo 23:39) Anataja maneno ya unabii yenye kuwa katika Zaburi 118:26: “Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova; tunakubariki tukiwa katika nyumba ya Yehova.” Ni wazi kwamba, hakuna mutu mwenye angesema maneno hayo katika hekalu kwa sababu lingeharibiwa.

Yesu anaenda sasa sehemu ya hekalu kwenye kunapatikana visanduku vya hazina. Watu wanaweza kutia michango yao katika tundu ndogo kwenye sehemu ya juu ya kisanduku. Yesu anaona Wayahudi wengi wakifanya hivyo; matajiri “walikuwa wanatumbukiza ndani feza nyingi za vichele” kama zawadi. Kisha Yesu anamuangalia mujane maskini mwenye anatumbukiza ndani “feza mbili za vichele zenye samani kidogo sana.” (Marko 12:41, 42) Bila shaka, Yesu anajua kwamba Mungu anapendezwa sana na zawadi yake.

Anaita wanafunzi wake na kusema: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, mujane huyu maskini ametoa zaidi ya wote wenye walitia feza ndani ya masanduku ya hazina.” Namna gani? Anaeleza: “Wote walitoa kutokana na wingi wa feza zao, lakini yeye, hata kama ni maskini, alitoa kila kitu chenye alikuwa nacho, kila kitu chenye alikuwa nacho lazima ili kuishi.” (Marko 12:43, 44) Mujane huyo iko tofauti kabisa na viongozi wa dini!

Nisani 11 inaendelea, Yesu anaondoka kwenye hekalu, na hii ndio mara yake ya mwisho. Mumoja kati ya wanafunzi wake anashangaa: “Mwalimu, ona namna majiwe na majengo haya ni ya ajabu!” (Marko 13:1) Kwa kweli, majiwe fulani ya ukuta wa hekalu ni makubwa sana, na yanafanya hekalu likuwe nguvu sana. Kwa hiyo maneno ya Yesu yanaonekana kuwa yenye kushitusha wakati anasema: “Unaona majengo haya makubwa? Hakuna jiwe lenye litaachwa hapa juu ya jiwe bila kuangushwa chini.”—Marko 13:2.

Kisha kusema maneno hayo, Yesu pamoja na wanafunzi wake wanatambuka Bonde la Kidroni na wanapanda kwenye Mulima wa Mizeituni. Wakati huu iko pamoja na wanafunzi wake ine: Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana. Wakati wako huko, wanaweza kuona vizuri hekalu lenye kupendeza.