Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 133

Mwili wa Yesu Unatayarishwa na Kuzikwa

Mwili wa Yesu Unatayarishwa na Kuzikwa

MATAYO 27:57–28:2 MARKO 15:42–16:4 LUKA 23:50–24:3 YOHANA 19:31–20:1

  • MWILI WA YESU UNAONDOLEWA KWENYE MUTI

  • MWILI UNATAYARISHWA KWA AJILI YA MAZIKO

  • WANAMUKE WANAKUTA KABURI LIKO WAZI

Sasa ni mangaribi ya Siku ya Tano tarehe 14 mwezi wa Nisani. Wakati jua litashuka, Sabato ya tarehe 15 ya mwezi wa Nisani itaanza. Yesu amekwisha kufa, lakini wezi wawili wenye kuwa pembeni hawajakufa. Sheria ilisema kuwa miili yenye kufa “isibakie kwenye muti usiku wote” lakini, inapaswa kuzikwa “siku hiyo.”—Kumbukumbu la Torati 21:22, 23.

Zaidi ya hilo, kipindi cha kisha muchana cha Siku ya Tano kinaitwa Matayarisho kwa sababu watu wanatayarisha chakula na kumalizia kazi zenye zinapaswa kufanywa mbele ya Sabato kuanza. Wakati jua litashuka, Sabato “kubwa,” itaanza. (Yohana 19:31) Inaitwa hivyo kwa sababu tarehe 15 ya mwezi wa Nisani itakuwa siku ya kwanza ya siku saba za Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu, kwa kawaida siku ya kwanza inakuwa Sabato. (Mambo ya Walawi 23:5, 6) Wakati huu siku ya kwanza inakuwa siku ileile ya Sabato ya kila juma, ni kusema, siku ya saba.

Kwa hiyo, Wayahudi wanaomba Pilato afanye jambo fulani ili Yesu na wezi wenye walikuwa wanatundikwa pembeni yake wakufe haraka. Namna gani? Kwa kuwavunja miguu. Hilo litafanya washindwe kutumia miguu yao ili kuinua mwili wao ili waweze kupumua. Maaskari wanakuja na kuvunja miguu ya wezi hao wawili. Lakini, inaonekana kuwa Yesu amekufa, na kwa hiyo, hawavunje miguu yake. Hilo linatimiza andiko la Zaburi 34:20 lenye kusema hivi: “Analinda mifupa yake yote; hakuna mumoja kati ya mifupa yake wenye umevunjwa.”

Ili wakuwe hakika kuwa Yesu amekufa kabisa, askari mumoja anaingiza mukuki katika mbavu zake, sehemu kwenye moyo wake unapatikana. ‘Mara moja damu na maji vinatoka.’ (Yohana 19:34) Hilo linatimiza andiko lingine lenye kusema hivi: “Wataangalia ule mwenye walitoboa.”— Zekaria 12:10.

Yosefu “mutu mumoja tajiri” kutoka katika muji wa Arimatea, na ambaye ni mutu mwenye kuheshimiwa sana wa Sanhedrini, iko pia nafasi kwenye Yesu anatundikwa. (Matayo 27:57) Biblia inamuita kuwa “mutu mwema na mwenye kufanya mambo yenye kuwa sawa,” mwenye “anangojea Ufalme wa Mungu.” Kwa kweli, kwa sababu yeye ni “mwenye alikuwa mwanafunzi wa Yesu lakini kwa uficho,” hakuunga muko tribinali wakati ilimuhukumu Yesu. (Luka 23:50; Marko 15:43; Yohana 19:38) Yosefu anatenda bila kuogopa na anamuomba Pilato mwili wa Yesu. Pilato anamuita mukubwa wa jeshi mwenye alikuwa anasimamia kuuawa kwa Yesu, na mukubwa huyo anahakikisha kuwa Yesu amekufa. Mara moja, Pilato anakubali ombi la Yosefu.

Yosefu anauza nguo ya kitani safi na kizuri na kushusha mwili wa Yesu kwenye muti. Anafunga mwili huo katika nguo hiyo na kuutayarisha kwa ajili ya maziko. Nikodemo, “mwenye alikuwa amekuja kwake [Yesu] usiku mara ya kwanza,” anasaidia kufanya matayarisho. (Yohana 19:39) Analeta kilo 33 ya muchanganyiko wa bei sana wa manemane na udi. Mwili wa Yesu unafungwa katika vitambaa vyenye kuwa na vikolezo hivyo, kulingana na desturi ya Wayahudi ya maziko.

Yosefu iko na kaburi lenye halijatumiwa lenye kuchimbuliwa katika mwamba wenye kuwa karibu na mahali hapo, na mwili wa Yesu unawekwa katika kaburi hilo. Kisha jiwe kubwa linawekwa kwenye muingilio wa kaburi. Wanafanya hivyo haraka sana, mbele Sabato ianze. Inawezekana kuwa Maria Magdalene na Maria mama ya Yakobo Mudogo walikuwa wanasaidia kutayarisha mwili wa Yesu. Sasa wanaenda haraka nyumbani “kutayarisha manukato na mafuta yenye marashi” yenye watapakaa mwili wa Yesu kisha Sabato.—Luka 23:56.

Siku yenye ilifuata, ni kusema, siku ya Sabato, wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wanaenda kwa Pilato na kumuambia hivi: “Tumekumbuka mambo yenye ule mujanja alisema wakati alikuwa angali muzima, ‘Nitafufuliwa kisha siku tatu (3).’ Kwa hiyo, amuru kaburi lilindwe mupaka siku ya tatu (3), ili wanafunzi wake wasikuje na kumuiba na kuambia watu, ‘Amefufuliwa kutoka kwa wafu!’ Halafu uongo huu wa mwisho utakuwa mubaya kuliko ule wa kwanza.” Pilato akawaambia: “Ninyi muko na walinzi. Muende mulilinde vile munajua.”—Matayo 27:63-65.

Siku ya Yenga asubui sana, Maria Magdalene, Maria mama ya Yakobo, na wanamuke wengine wanaleta vikolezo kwenye kaburi ili kupakaa mwili wa Yesu. Wanaambiana hivi: “Ni nani atatuviringishia jiwe kutoka kwenye muingilio wa kaburi?” (Marko 16:3) Lakini tetemeko la inchi limetokea. Zaidi ya hilo, malaika wa Mungu ametosha jiwe hilo, walinzi hawako tena, na kaburi liko wazi!