Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 137

Mamia Wanamuona Mbele ya Pentekoste

Mamia Wanamuona Mbele ya Pentekoste

MATAYO 28:16-20 LUKA 24:50-52 MATENDO 1:1-12; 2:1-4

  • YESU ANATOKEA WATU WENGI

  • ANAPANDA MBINGUNI

  • YESU ANAMWANGA ROHO TAKATIFU JUU YA WANAFUNZI 120

Kisha Yesu kufufuliwa, anafanya mipango ili mitume wake 11 wakutane naye kwenye mulima fulani katika Galilaya. Wanafunzi wengine pia wako hapo, watu 500 hivi, wamoja kati yao walikuwa na mashaka mwanzoni. (Matayo 28:17; 1 Wakorinto 15:6) Lakini mambo yenye Yesu anasema sasa yanasaidia kila mumoja wao akuwe hakika kuwa yeye ni mwenye kuishi.

Yesu anaeleza kuwa Mungu amemupatia mamlaka yote mbinguni na duniani. Yesu anawaambia hivi “Kwa hiyo, muende, na mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na muwabatize katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na muwafundishe kushika mambo yote yenye nimewaamuru ninyi.” (Matayo 28:18-20) Ndiyo, Yesu ni mwenye kuishi lakini anapenda pia kuona kazi ya kuhubiri habari njema inafanywa.

Wanafunzi wote wa Yesu, ni kusema wanaume, wanamuke, na watoto wanapewa kazi hiyo ya kufanya wanafunzi. Wapinzani wanaweza kujaribu kuzuia kazi yao ya kuhubiri na kufundisha, lakini Yesu anawahakikishia hivi: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.” Hilo linamaanisha nini kwa wanafunzi wake? Anawaambia hivi: “Muangalie! Niko pamoja nanyi sikuzote mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” Yesu haseme kuwa wote wenye wanafanya kazi ya kuhubiri habari njema watakuwa na uwezo wa kufanya miujiza. Lakini, watapata musaada wa roho takatifu.

Kwa ujumla, Yesu anatokea wanafunzi wake kwa “siku makumi ine (40)” kisha kufufuliwa kwake. Anavaa miili mbalimbali ya kibinadamu na anajionyesha “mwenyewe kwao akiwa muzima kupitia uhakikisho mwingi wenye kusadikisha,” na kuwafundisha “juu ya Ufalme wa Mungu.”—Matendo 1:3; 1 Wakorinto 15:7.

Inaonekana mitume wangali Galilaya, wakati Yesu anawaambia warudie Yerusalemu. Wakati anakutana nao katika muji, anasema hivi: “Musitoke Yerusalemu, lakini muendelee kungojea kile Baba aliahidi, kile mulisikia ninazungumuzia; kwa maana Yohana, kwa kweli, alibatiza kwa maji, lakini ninyi mutabatizwa kwa roho takatifu kisha siku kidogo.”—Matendo 1:4, 5.

Kisha Yesu anakutana tena na mitume wake. Anawaongoza “mupaka Betania,” yenye kuwa upande wa mashariki mwa Mulima wa Mizeituni. (Luka 24:50) Hata kama Yesu alikuwa amewaambia mambo yote juu ya kuenda kwake, wangali wanaamini kuwa kwa njia fulani Ufalme wake utakuwa hapa duniani.—Luka 22:16, 18, 30; Yohana 14:2, 3.

Mitume wanauliza Yesu hivi: “Bwana, je, unarudishia Israeli ufalme wakati huu?” Anajibu tu hivi: “Haiko kazi yenu kujua nyakati ao vipindi vyenye Baba ameweka katika mamlaka yake mwenyewe.” Kisha, anakazia tena kazi yenye wanapaswa kufanya, kwa kusema hivi: “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”—Matendo 1:6-8.

Wanafunzi wako kwenye Mulima wa Mizeituni pamoja na Yesu mwenye amefufuliwa wakati anaanza kupanda kuenda mbinguni. Kisha muda mufupi wingu linawazuia kumuona. Kisha kufufuliwa kwake, Yesu alivaa miili mbalimbali ya kibinadamu. Lakini sasa Yesu anatosha mwili wenye alikuwa nao wakati huu, anapanda mbinguni na mwili wa roho. (1 Wakorinto 15:44, 50; 1 Petro 3:18) Wakati mitume waaminifu wanaendelea kumuangalia, “mara moja wanaume wawili wenye kuvaa nguo nyeupe” wanatokea pembeni yao. Wanaume hao wawili ni malaika wenye kuvaa miili ya kibinadamu, wanauliza hivi: “Wanaume wa Galilaya, sababu gani munasimama na kuangalia katika anga? Huyu Yesu mwenye alichukuliwa kutoka kwenu kuenda katika anga, atakuja kwa namna ileile mumemuona akienda katika anga.”—Matendo 1:10, 11.

Yesu anatoka duniani bila kujionyesha kwa watu wengi, ni wanafunzi wake waaminifu tu ndio wanaona. Atarudia “kwa namna ileile,” bila kujionyesha kwa watu wengi, ni wanafunzi wake waaminifu tu ndio wanatambua kuwapo kwake katika mamlaka ya Kifalme.

Mitume wanarudia Yerusalemu. Katika siku zenye kufuata, wanakusanyika pamoja na wanafunzi wengine, na pia “Maria mama ya Yesu . . . na ndugu za Yesu.” (Matendo 1:14) Kikundi hicho kinaendelea kusali sana. Kati ya mambo yenye wanazungumuzia katika sala yao ni kuchagua mwanafunzi mwenye atakamata nafasi ya Yuda Iskariote na kufanya hesabu ya mitume ikuwe 12. (Matayo 19:28) Wanapenda kupata mwanafunzi mwenye aliona namna Yesu anafanya kazi zake na kufufuliwa. Hii ndiyo mara ya mwisho Biblia inazungumuzia tendo la kupiga kura ili kujua mapenzi ya Mungu. (Zaburi 109:8; Methali 16:33) Matia, mwenye pengine alikuwa kati ya wanafunzi 70 wenye Yesu alituma, anachaguliwa na ‘kuhesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja (11).’—Matendo 1:26.

Siku kumi kisha Yesu kuenda mbinguni, Sikukuu ya Wayahudi ya Pentekoste ya mwaka 33 wakati wetu inafanywa. Wanafunzi 120 hivi wanakusanyika katika chumba cha juu katika Yerusalemu. Mara moja, makelele kama ya upepo wenye nguvu wenye kuvuma yanajaa katika nyumba yote. Ndimi kama za moto zinaonekana juu ya kila mutu mwenye iko hapo. Wanafunzi wote wanaanza kuzungumuza katika luga mbalimbali. Roho takatifu yenye Yesu alikuwa ameahidi inamwangwa juu yao!—Yohana 14:26.