Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 126

Petro Anamukana Yesu Kwenye Nyumba ya Kayafa

Petro Anamukana Yesu Kwenye Nyumba ya Kayafa

Kisha Yesu kukamatwa katika bustani ya Getsemane, mitume wanamuacha, wanakimbia kwa sababu wanaogopa. Hata hivyo, wawili kati yao wanaacha kukimbia. Ni Petro “na vilevile mwanafunzi mwingine,” pengine mutume Yohana. (Yohana 18:15; 19:35; 21:24) Pengine wanamukaribia Yesu wakati anapelekwa katika nyumba ya Anasi. Wakati Anasi anamutuma Yesu kwa Kuhani Mukubwa Kayafa, Petro na Yohana wanamufuata kwa mbali. Inawezekana kuwa wanaogopea maisha yao wenyewe na wanahangaika kwa sababu ya mambo yenye yatamupata Bwana wao.

Yohana anajulikana kwa kuhani mukubwa na kwa hiyo, anaruhusiwa kuingia katika uwanja wa nyumba ya Kayafa. Petro anabakia inje mupaka wakati Yohana anarudia na kuzungumuza na mutumishi mwanamuke mwenye kuchunga mulango. Kisha Petro anaruhusiwa kuingia

Ni usiku wenye baridi, kwa hiyo, watu wenye kuwa katika uwanja wanawasha moto wa makaa. Petro anakaa pamoja nao ili kuota moto wakati iko anangojea “ili aone mambo yatakuwa namna gani” wakati Yesu iko anasambishwa. (Matayo 26:58) Sasa, kupitia mwangaza wa moto, mwanamuke mwenye alikuwa anachunga mulango mwenye aliingiza Petro anamuangalia muzuri. Anamuuliza hivi: “Wewe pia ni mumoja wa wanafunzi wa mutu huyu, haiko vile?” (Yohana 18:17) Na wengine pia wanamutambua Petro na kusema kuwa alikuwa pamoja na Yesu.—Matayo 26:69, 71-73; Marko 14:70.

Petro anaogopa sana kwa sababu ya jambo hilo. Hapendi watu wamutambue, anajaribu hata kuondoka na kuenda kwenye mulango. Kwa hiyo, Petro anakataa kuwa hakukuwa pamoja na Yesu, kwa kusema hivi: “Simujue na sielewe unataka kusema nini.” (Marko 14:67, 68) Pia anaanza “kulaani na kuapa,” maana yake, iko tayari kufanya kiapo ili kuonyesha kuwa maneno yake ni kweli na kuwa anakubali kupatwa na matokeo ya mubaya ikiwa anasema uongo.—Matayo 26:74.

Wakati huohuo, Yesu anaendelea kusamba, pengine katika sehemu fulani ya nyumba ya Kayafa yenye kuwa juu ya uwanja. Petro na wengine wenye wanangojea chini, pengine wanaona namna mashahidi mbalimbali wako wanaingia ndani na kutoka ili kutoa ushuhuda.

Kwa sababu namna ya kusema ya Petro ni ya Wagalilaya, hilo linaonyesha kuwa anasema uongo kwa kusema kama hamujue Yesu. Zaidi ya hilo, mutu mumoja katika kikundi hicho ni mutu wa familia ya Malko, mwenye Petro alikata sikio. Kwa hiyo, anamuambia Petro hivi: “Mimi nilikuona katika bustani pamoja naye, haiko vile?” Wakati Petro anamukana Yesu kwa mara ya tatu, jogoo anawika kama vile Yesu alikuwa ametabiri.—Yohana 13:38; 18:26, 27.

Wakati huo, inawezekana kuwa Yesu iko kwenye baraza na iko anaangalia kwenye uwanja. Bwana anageuka na kumuangalia Petro mara moja, hilo lilipaswa kumuumiza sana Petro. Anakumbuka mambo yenye Yesu alikuwa amesema saa fulani mbele ya hapo katika chumba cha juu. Wazia namna Petro anajisikia wakati anatambua jambo lenye amefanya! Petro anaenda inje na analia kwa uchungu.—Luka 22:61, 62.

Jambo hilo liliwezekana namna gani? Namna gani Petro mwenye alikuwa hakika kuwa iko nguvu kiroho na mushikamanifu, anakana Bwana wake? Watu hawaseme kweli juu ya Yesu, na wanamushitaki kuwa mutu mwenye alifanya makosa makubwa. Petro alipaswa kumutetea mutu huyo mwenye hana kosa, lakini alimukana mutu huyo mwenye kuwa “na maneno ya uzima wa milele.”—Yohana 6:68.

Mambo ya mubaya yenye yalimupata Petro yanaonyesha kuwa hata mutu mwenye kuwa na imani yenye nguvu na mushikamanifu anaweza kuanguka ikiwa hajitayarishe muzuri juu ya majaribu yenye yanaweza kutokea. Watumishi wote wa Mungu wanapaswa kujifunza somo fulani juu ya mambo yenye yalimupata Petro!