Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 122

Sala ya Mwisho ya Yesu Katika Chumba cha Juu

Sala ya Mwisho ya Yesu Katika Chumba cha Juu

YOHANA 17:1-26

  • MATOKEO YA KUJUA MUNGU NA MWANA WAKE

  • UMOJA KATI YA YEHOVA, YESU, NA WANAFUNZI

Kwa sababu anasukumwa na upendo mwingi juu ya mitume wake, Yesu amewatayarisha juu ya kuondoka kwake kwenye kunakaribia sana. Sasa anainua macho yake kuelekea mbinguni na anasali kwa Baba yake hivi: “Tukuza mwana wako ili mwana wako akutukuze, kwa kuwa ulimupatia mamlaka juu ya kila mwili, ili apatie uzima wa milele wale wote wenye umemupatia.”—Yohana 17:1, 2.

Ni wazi kwamba Yesu anaelewa kuwa kumupatia Baba yake utukufu ndilo jambo la maana zaidi. Lakini tumaini lenye Yesu anazungumuzia ni lenye kutia moyo sana, ni kusema, uzima wa milele! Kwa sababu amepewa “mamlaka juu ya kila mwili,” Yesu anaweza kutoa faida ya zabihu yake ya ukombozi kwa wanadamu wote. Lakini, ni hesabu fulani tu ndio watabarikiwa. Sababu gani ni watu fulani tu? Kwa sababu Yesu atatolea faida za zabihu yake ya ukombozi wale tu wenye kutenda kulingana na jambo lenye anazungumuzia sasa. Anasema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wajifunze ili wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3.

Mutu anapaswa kujua muzuri kabisa Baba na Mwana, ni kusema, kuwa na urafiki wa sana pamoja nao. Anapaswa kuona mambo namna wanayaona. Zaidi ya hilo, anapaswa kujikaza kuiga sifa zao za muzuri katika namna yake ya kuwatendea wengine. Na anapaswa kuelewa kuwa, kati ya kumutukuza Mungu na wanadamu kupata uzima wa milele, kumutukuza Mungu ndilo jambo la maana zaidi. Sasa Yesu anarudilia habari hii kubwa:

“Nimekutukuza katika dunia, kwa kuwa nimemaliza kazi yenye ulinipatia nifanye. Basi sasa, Baba, unitukuze pembeni yako kwa utukufu wenye nilikuwa nao pembeni yako mbele ya ulimwengu kuwa.” (Yohana 17:4, 5) Ndiyo, Yesu anaomba arudishwe katika utukufu wa mbinguni kupitia ufufuo.

Hata hivyo, Yesu hasahau mambo yenye ametimiza katika kazi yake ya kuhubiri. Anasali hivi: “Nimejulisha jina lako kwa watu wenye ulinipatia kutoka katika ulimwengu. Walikuwa wako, na ukanipatia, na wameshika neno lako.” (Yohana 17:6) Katika kazi yake ya kuhubiri, Yesu hakutaja tu jina la Mungu, Yehova. Alisaidia mitume wake wajue jina hilo linawakilisha nini, ni kusema, sifa za Mungu na namna yake ya kutendea wanadamu.

Mitume wamefikia kumujua Yehova, daraka la Mwana wake, na mambo yenye Yesu amefundisha. Kwa unyenyekevu, Yesu anasema hivi: “Nimewapatia maneno yenye ulinipatia, na wameyakubali na wamejua kabisa kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wako, na wameamini kwamba ulinituma.”—Yohana 17:8.

Kisha Yesu anazungumuzia waziwazi tofauti kati ya wanafunzi wake na ulimwengu wa wanadamu wote kwa ujumla. Anasema hivi: “Ninaomba kwa ajili yao; siombe kwa ajili ya ulimwengu, lakini ninaomba kwa ajili ya wale wenye wewe ulinipatia, kwa sababu ni wako. . . . Baba Mutakatifu, uwalinde kwa sababu ya jina lako lenye umenipatia, ili wakuwe kitu kimoja kama vile sisi tuko kitu kimoja. . . . Nimewalinda, na hakuna hata mumoja wao mwenye aliharibiwa isipokuwa ule mwana wa uharibifu,” ni kusema, Yuda Iskariote, mwenye alikuwa anatafuta namna ya kumusaliti Yesu.—Yohana 17:9-12.

Yesu anaendelea kusali hivi: “Ulimwengu umewachukia. . . . Siombe kwamba uwatoshe katika ulimwengu, lakini ninaomba kwamba uwalinde kwa sababu ya ule muovu. Wao hawako sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:14-16) Mitume na wanafunzi wengine wako katika ulimwengu, ni kusema, ulimwengu wa wanadamu wenye kuongozwa na Shetani, lakini wanapaswa kuendelea kujitenga na ulimwengu huo na ubaya wake. Namna gani?

Wanapaswa kuendelea kuwa watakatifu, ni kusema, wenye kuwekwa pembeni ili wamutumikie Mungu, kwa kutumikisha katika maisha yao kweli yenye kupatikana katika Maandiko ya Kiebrania na kweli zenye Yesu alikuwa amefundisha. Yesu anasali hivi: “Uwatakase kwa njia ya ile kweli; neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Kisha wakati fulani, mitume fulani wataandika vitabu vyenye kuongozwa na roho ya Mungu vyenye vitakuwa sehemu ya “ile kweli” yenye inaweza kumutakasa mutu.

Lakini kisha wakati fulani, kutakuwa wengine pia wenye watakubali “ile kweli.” Kwa hiyo, Yesu anasali haiko ‘kwa ajili ya hawa tu [wale wenye kuwa hapo], lakini anaomba pia kwa ajili ya wale wenye wanamuamini kupitia neno lao.’ Yesu anaomba nini kwa ajili yao wote? Anasema hivi: “Ili wote wakuwe kitu kimoja, kama vile wewe, Baba, uko katika umoja na mimi na mimi niko katika umoja na wewe, wao pia wakuwe katika umoja na sisi.” (Yohana 17:20, 21) Hilo halimaanishe kuwa Yesu na Baba yake wako mutu mumoja kwa njia ya moja kwa moja. Wako mumoja katika maana ya kwamba wanapatana katika mambo yote. Yesu anasali kuwa wanafunzi wake pia wakuwe na umoja kama huo.

Muda mufupi mbele ya hapo, Yesu alikuwa amemuambia Petro na wengine kuwa alikuwa anaenda kuwatayarishia nafasi, ni kusema, nafasi huko mbinguni. (Yohana 14:2, 3) Yesu anarudilia wazo hilo katika sala. Anasema hivi: “Baba, ninataka wale wenye umenipatia wakuwe pamoja na mimi kwenye niko, ili waone utukufu wangu wenye umenipatia, kwa sababu ulinipenda mbele ya kuwekwa kwa musingi wa ulimwengu.” (Yohana 17:24) Anahakikisha kuwa zamani sana, mbele Adamu na Eva wazae watoto, Mungu alimupenda Mwana wake muzaliwa wa kwanza, mwenye alifikia kuwa Yesu Kristo.

Ili kumalizia sala yake, Yesu anakazia jina la Mungu na upendo wake kwa mitume na wengine wenye watakubali “ile kweli.” Anasema hivi: “Nimewajulisha jina lako na nitalijulisha, ili upendo wenye ulinipenda ukuwe ndani yao na mimi nikuwe katika umoja nao.”—Yohana 17:26.