Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 105

Anatumia Muti wa Tini ili Kufundisha Somo Fulani Kuhusu Imani

Anatumia Muti wa Tini ili Kufundisha Somo Fulani Kuhusu Imani

MATAYO 21:19-27 MARKO 11:19-33 LUKA 20:1-8

  • MUTI WA TINI WENYE ULIKAUKA—SOMO KUHUSU IMANI

  • MAMLAKA YA YESU YANAPINGWA

Siku ya Kwanza kisha midi, Yesu anatoka Yerusalemu na anarudia Betania, upande wa mashariki wa Mulima wa Mizeituni. Bila shaka analala kwa rafiki zake Lazaro, Maria, na Marta.

Sasa ni asubui ya tarehe 11 Mwezi wa Nisani. Yesu na wanafunzi wake wako njiani tena, wakirudi Yerusalemu. Huko atakuwa kwenye hekalu mara ya mwisho. Na ni siku ya mwisho ya utumishi wake mbele ya watu wengi mbele asherehekee Pasaka, aanzishe Ukumbusho wa kifo chake, na kisha apatwe na majaribu na kifo.

Wakati walikuwa wanatoka Betania upande wa Mulima wa Mizeituni kuelekea Yerusalemu, Petro anaona ule muti wenye Yesu alilaani asubui yenye ilipita. Anashangaa na kusema hivi: “Rabi, ona! ule muti wa tini wenye ulilaani umekauka.”—Marko 11:21.

Lakini, sababu gani Yesu alifanya ule muti ukauke? Anafunua sababu katika jibu lake: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, kama muko na imani na hamuna mashaka, hamutafanya tu jambo lenye nilifanyia muti wa tini, lakini hata mukiambia mulima huu, ‘Ondoka na utupwe katika bahari,’ jambo hilo litatendeka. Na mambo yote yenye munaomba katika sala, kama muko na imani, mutayapokea.” (Matayo 21:21, 22) Kwa hiyo anarudilia jambo lenye alikuwa amesema kuhusu uwezo wa imani wa kuhamisha mulima.—Matayo 17:20.

Kwa hiyo kwa kufanya muti ukauke, Yesu anaonyesha kuwa ni jambo la maana kumuamini Mungu. Anasema hivi: “Mambo yote yenye munaomba katika sala, mukuwe na imani kwamba mumekwisha kuyapokea, na mutayapata.” (Marko 11:24) Ni somo la maana kabisa kwa wanafunzi wote wa Yesu! Jambo hilo linafaa kabisa kwa mitume kwa sababu ya majaribu makali yenye watapata hivi karibuni. Kuko uhusiano mwengine kati ya muti wa tini kukauka na sifa ya imani.

Kama muti huo wa tini, taifa la Israeli liko na sura yenye kudanganya. Watu wa taifa hili wako katika agano pamoja na Mungu, na kwa inje wanaonekana kuwa wenye kushika Sheria yake. Lakini, wanashindwa kuzaa matunda mazuri na wanamukataa hata Mwana wa Mungu! Kwa hiyo, kwa kufanya muti wa tini ukauke, Yesu anaonyesha namna mwisho utakuwa kwa taifa hilo lenye kushindwa kuzaa matunda na lenye kukosa imani.

Kisha wakati kidogo, Yesu na wanafunzi wake wanaingia katika Yerusalemu. Na kulingana na desturi yake, Yesu anaenda kwenye hekalu na anaanza kufundisha. Bila shaka wakubwa wa makuhani na wazee wa watu wangali wanakumbuka mambo yenye Yesu alifanyia wabadilisha-feza siku yenye ilipita. Wanamuuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ao ni nani alikupatia mamlaka hii ya kufanya mambo haya?”—Marko 11:28.

Yesu anawajibu: “Nitawauliza ulizo moja. Munijibu, na mimi nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani. Ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni ao kwa wanadamu? Munijibu.” Sasa wale wenye kumupinga ndio wanajikuta mbele ya tatizo. Makuhani na wazee wanaanza kuambiana: “Kama tunasema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atasema, ‘Basi, sababu gani hamukumuamini?’ Lakini je, tupime kusema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’?” Walifikiri kwa njia hiyo kwa sababu waliogopa watu, “kwa maana wote waliona kwamba kwa kweli Yohana alikuwa nabii.”—Marko 11:29-32.

Wale wenye wanamupinga Yesu wanashindwa kupata jibu la muzuri. Basi wanajibu: “Hatujue.” Yesu anawaambia: “Na mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”—Marko 11:33.