Utangulizi wa Vitabu vya Biblia
Video hizi fupi zinatupatia habari zenye thamani kuhusu maelezo ya msingi na mambo yaliyomo kwenye vitabu hivyo. Tumia masomo haya kuboresha funzo lako la kibinafsi na usomaji wako wa Biblia.
Utangulizi wa Yoshua
Ona jinsi Waisraeli wanavyoshinda na kugawanya nchi waliyopewa na Mungu.
Utangulizi wa Waamuzi
Kitabu hiki kilicho na masimulizi yenye kusisimua kinaitwa kwa jina la wanaume wenye ujasiri na wenye imani ambao Mungu aliwatumia kuwakomboa Waisraeli kutoka kwa mataifa yaliyowakandamiza.
Utangulizi wa Ruthu
Kitabu cha Ruthu kinasimulia kuhusu upendo wa kujidhabihu wa mjane mwenye umri mdogo kuelekea mama-mkwe wake na jinsi Yehova alivyowathawabisha wote wawili.
Utangulizi wa 1 Samweli
Ona jinsi historia ya Israeli inavyosonga kutoka kwenye kipindi cha Waamuzi hadi utawala wa wafalme.
Utangulizi wa 1 Wafalme
Ona historia ya Israeli kuanzia kipindi chenye utukufu na ufanisi chini ya utawala wa Mfalme Sulemani hadi kipindi chenye msukosuko cha mataifa mawili ya Israeli na Yuda.
Utangulizi wa 2 Wafalme
Ona jinsi uasi-imani unavyoathiri ufalme wa kaskazini wa Israeli, huku Yehova akiwabariki wachache wanaomtumikia kwa moyo kamili.
Utangulizi wa 1 Mambo ya Nyakati
Fuata nasaba na maisha yenye kusisimua ya Mfalme Daudi anayemwogopa Mungu tangu anapowekwa rasmi kuwa mfalme wa Israeli hadi kifo chake.
Utangulizi wa 2 Mambo ya Nyakati
Ona jinsi historia ya wafalme wa Yuda inakazia thamani ya ushikamanifu kwa Mungu.
Utangulizi wa Ezra
Yehova anatimiza ahadi yake ya kuwakomboa watu wake kutoka Babiloni na kurudisha ibada ya kweli Yerusalemu.
Utangulizi wa Nehemia
Kitabu cha Biblia cha Nehemia kina mambo muhimu ya kuwafundisha watumishi wote wa kweli leo.
Utangulizi wa Esta
Matukio yenye kusisimua ya siku za Esta yataimarisha imani yako katika uwezo wa Yehova Mungu wa kuwakomboa watu wake kutoka katika majaribu leo.
Utangulizi wa Ayubu
Wote wanaompenda Yehova watajaribiwa. Simulizi la Ayubu linatusaidia tuwe na uhakika kwamba tunaweza kudumisha utimilifu na kutetea enzi kuu ya Yehova.
Utangulizi wa Zaburi
Kitabu cha Zaburi kinategemeza enzi kuu ya Yehova, kinawasaidia na kuwafariji wale wanaompenda, na kuonyesha jinsi ulimwengu utakavyobadilika kupitia kwa Ufalme wake.