Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SWALI LA 15

Unawezaje Kuwa na Furaha?

“Ni afadhali kula mboga za majani mahali penye upendo kuliko kula ng’ombe dume aliyenoneshwa mahali penye chuki.”

Methali 15:⁠17

“Mimi, Yehova, ni Mungu wako, ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, ninayekuongoza katika njia unayopaswa kutembea.”

Isaya 48:⁠17

“Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao.”

Mathayo 5:3

“Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”

Mathayo 22:⁠39

“Kama vile mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo.”

Luka 6:​31

“Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”

Luka 11:⁠28

“Mtu anapokuwa na vitu vingi, uhai wake hautokani na vitu alivyo navyo.”

Luka 12:⁠15

“Basi, tukiwa na chakula na mavazi, tutaridhika na vitu hivyo.”

1 Timotheo 6:8

“Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”

Matendo 20:⁠35