Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SWALI LA 1

Mungu Ni Nani?

“Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Zaburi 83:⁠18

“Jueni kwamba Yehova ni Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, na sisi ni mali yake.”

Zaburi 100:3

“Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu; simpi yeyote utukufu wangu, wala kuzipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.”

Isaya 42:8

“Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”

Waroma 10:⁠13

“Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.”

Waebrania 3:4

“Inueni macho yenu mbinguni mwone. Ni nani aliyeviumba vitu hivi? Ni Yule anayelileta nje jeshi lao kwa hesabu; huziita zote kwa majina. Kwa sababu ya nguvu zake nyingi zenye msukumo na nguvu zake zenye kuogopesha, hakuna hata moja inayokosekana.”

Isaya 40:⁠26