Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 15:1-29

  • Walawi wabeba sanduku la agano na kulipeleka Yerusalemu (1-29)

    • Mikali amdharau Daudi (29)

15  Naye akaendelea kujijengea nyumba katika Jiji la Daudi, akatayarisha mahali kwa ajili ya Sanduku la Mungu wa kweli na kupiga hema kwa ajili yake.+  Huo ndio wakati ambao Daudi alisema: “Hakuna mtu yeyote anayepaswa kubeba Sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua ili walibebe Sanduku la Yehova na kumhudumia sikuzote.”+  Kisha Daudi akawakusanya Waisraeli wote Yerusalemu ili kulipandisha Sanduku la Yehova na kulileta mahali alipotayarisha kwa ajili yake.+  Daudi akawakusanya wazao wa Haruni+ na Walawi:+  kutoka kwa Wakohathi, mkuu Urieli na ndugu zake 120;  kutoka kwa Wamerari, mkuu Asaya+ na ndugu zake 220;  kutoka kwa Wagershomu, mkuu Yoeli+ na ndugu zake 130;  kutoka kwa wazao wa Elisafani,+ mkuu Shemaya na ndugu zake 200;  kutoka kwa wazao wa Hebroni, mkuu Elieli na ndugu zake 80; 10  kutoka kwa wazao wa Uzieli,+ mkuu Aminadabu na ndugu zake 112. 11  Tena, Daudi akawaita makuhani Sadoki+ na Abiathari+ na Walawi Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli, na Aminadabu, 12  akawaambia: “Ninyi ndio viongozi wa koo* za Walawi. Jitakaseni, ninyi na ndugu zenu, nanyi mlipandishe Sanduku la Yehova, Mungu wa Israeli mpaka mahali ambapo nimetayarisha kwa ajili yake. 13  Kwa kuwa mara ya kwanza hamkulibeba,+ hasira ya Yehova Mungu wetu iliwaka dhidi yetu,+ kwa sababu hatukutafuta utaratibu unaofaa.”+ 14  Basi makuhani na Walawi wakajitakasa ili walipandishe Sanduku la Yehova Mungu wa Israeli. 15  Kisha Walawi wakalibeba Sanduku la Mungu wa kweli mabegani mwao kwa kutumia fito zake,+ kama Musa alivyoamuru kwa neno la Yehova. 16  Ndipo Daudi akawaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji ili waimbe kwa shangwe na sauti kubwa, kwa ala za muziki: vinanda, vinubi,+ na matoazi.+ 17  Basi Walawi wakamweka Hemani+ mwana wa Yoeli na, kutoka kati ya ndugu zake, Asafu+ mwana wa Berekia na, kutoka kati ya ndugu zao Wamerari, Ethani+ mwana wa Kushaya. 18  Walikuwa pamoja na ndugu zao wa kikundi cha pili,+ Zekaria, Beni, Yaazieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Benaya, Maaseya, Matithia, Elifelehu, na Mikneya na Obed-edomu na Yeieli walinzi wa malango. 19  Waimbaji Hemani,+ Asafu,+ na Ethani waliwekwa kupiga matoazi ya shaba;+ 20  na Zekaria, Azieli, Shemiramothi, Yehieli, Uni, Eliabu, Maaseya, na Benaya walipiga vinanda vilivyopatanishwa na sauti ya Alamothi;*+ 21  na Matithia,+ Elifelehu, Mikneya, Obed-edomu, Yeieli, na Azazia walipiga vinubi vilivyopatanishwa na sauti ya Sheminithi,*+ ili waongoze uimbaji. 22  Kenania+ mkuu wa Walawi alisimamia usafirishaji, kwa maana alikuwa stadi, 23  na Berekia na Elkana walikuwa walinzi wa malango kwa ajili ya Sanduku. 24  Makuhani Shebania, Yoshafati, Nethaneli, Amasai, Zekaria, Benaya, na Eliezeri walipiga tarumbeta kwa sauti kubwa mbele ya Sanduku la Mungu wa kweli,+ na Obed-edomu na Yehia walitumikia pia wakiwa walinzi wa malango kwa ajili ya Sanduku. 25  Kisha Daudi na wazee wa Israeli na wakuu wa maelfu walikuwa wakitembea kandokando ili kulipandisha sanduku la agano la Yehova kutoka katika nyumba ya Obed-edomu+ wakishangilia.+ 26  Mungu wa kweli alipowasaidia Walawi waliokuwa wakilibeba sanduku la agano la Yehova, waliwatoa dhabihu ng’ombe dume saba wachanga na kondoo dume saba.+ 27  Daudi alikuwa amevaa joho lisilo na mikono la kitambaa bora, kama walivyovaa Walawi wote waliobeba Sanduku hilo, waimbaji, na Kenania mkuu wa usafirishaji na wa waimbaji; Daudi pia alikuwa amevaa efodi ya kitani.+ 28  Waisraeli wote walikuwa wakilipandisha sanduku la agano la Yehova kwa kelele za shangwe,+ wakipiga pembe, tarumbeta,+ matoazi, na kupiga kwa sauti kubwa vinanda na vinubi.+ 29  Lakini sanduku la agano la Yehova lilipofika kwenye Jiji la Daudi,+ Mikali, binti ya Sauli,+ akaangalia chini kupitia dirishani, akamwona Mfalme Daudi akirukaruka na kusherehekea; akaanza kumdharau moyoni mwake.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.