Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 16:1-43

  • Sanduku la agano lawekwa hemani (1-6)

  • Wimbo wa shukrani wa Daudi (7-36)

    • “Yehova amekuwa Mfalme!” (31)

  • Utumishi mbele ya sanduku la agano (37-43)

16  Basi wakaliingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amepiga ili aliweke humo;+ nao wakatoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika mbele za Mungu wa kweli.+  Daudi alipomaliza kutoa dhabihu za kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika,+ akawabariki watu katika jina la Yehova.  Isitoshe, aliwagawia Waisraeli wote, kila mwanamume na mwanamke, mkate mmoja wa mviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu kavu.  Kisha akawaweka baadhi ya Walawi wahudumu mbele ya Sanduku la Yehova,+ wamheshimu,* wamshukuru, na kumsifu Yehova Mungu wa Israeli.  Asafu+ alikuwa kiongozi, na wa pili Zekaria; naye Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu, na Yeieli+ walipiga vinanda na vinubi;+ na Asafu alipiga matoazi,+  na makuhani Benaya na Yahazieli walipiga tarumbeta daima mbele ya sanduku la agano la Mungu wa kweli.  Hiyo ndiyo siku ambayo Daudi kwa mara ya kwanza alitunga* wimbo huu wa kumshukuru Yehova na kumwagiza Asafu+ na ndugu zake wauimbe:  “Mshukuruni Yehova,+ liitieni jina lake,Yajulisheni mataifa matendo yake!+  Mwimbieni, mwimbieni sifa,*+Tafakarini* kazi zake zote zinazostaajabisha.+ 10  Jivunieni jina lake takatifu.+ Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+ 11  Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake,Utafuteni uso* wake daima.+ 12  Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,+Miujiza yake na hukumu alizotangaza, 13  Enyi uzao wa* Israeli mtumishi wake,+Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+ 14  Yeye ni Yehova Mungu wetu.+ Hukumu zake ziko duniani kote.+ 15  Kumbukeni agano lake milele,Ahadi aliyotoa,* hata kufikia vizazi elfu,+ 16  Agano alilofanya na Abrahamu,+Na kiapo alichomwapia Isaka,+ 17  Alichotoa kama amri kwa Yakobo+Na kama agano la kudumu kwa Israeli, 18  Akisema, ‘Nitakupa nchi ya Kanaani+Kuwa urithi wako uliogawiwa.’+ 19  Mlipokuwa wachache,Naam, wachache sana, nanyi mlikuwa wageni nchini.+ 20  Walitembeatembea kutoka taifa moja hadi taifa lingine,Kutoka ufalme mmoja hadi ufalme mwingine.+ 21  Hakumruhusu mtu yeyote awakandamize,+Lakini kwa sababu yao aliwakaripia wafalme,+ 22  Akisema, ‘Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,Wala msiwatendee manabii wangu jambo lolote baya.’+ 23  Mwimbieni Yehova, dunia yote! Tangazeni wokovu wake siku baada ya siku!+ 24  Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote. 25  Kwa maana Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote. Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.+ 26  Miungu yote ya mataifa ni miungu ya ubatili,+Lakini Yehova ndiye aliyeziumba mbingu.+ 27  Mbele zake kuna utukufu* na fahari;+Katika makao yake kuna nguvu na shangwe.+ 28  Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+ 29  Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+Leteni zawadi na mje mbele zake.+ Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu.*+ 30  Tetemekeni mbele zake, dunia yote! Dunia imeimarishwa kabisa; haiwezi kusogezwa.*+ 31  Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;+Tangazeni miongoni mwa mataifa: ‘Yehova amekuwa Mfalme!’+ 32  Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie. 33  Wakati uleule miti ya msituni na ishangilie kwa sauti mbele za Yehova,Kwa maana anakuja* kuihukumu dunia. 34  Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+ 35  Nanyi semeni, ‘Tuokoe, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Tukusanye na kutuokoa kutoka katika mataifa,Ili tulishukuru jina lako takatifu+Na tushangilie kukusifu wewe.+ 36  Yehova, Mungu wa Israeli, na asifiweKwa umilele wote.’”* Na watu wote wakasema, “Amina!”* nao wakamsifu Yehova. 37  Kisha Daudi akamwacha Asafu+ na ndugu zake hapo mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wahudumu daima mbele ya Sanduku+ hilo, kulingana na utaratibu wa kila siku.+ 38  Obed-edomu na ndugu zake, watu 68, na Obed-edomu mwana wa Yeduthuni, na Hosa walikuwa walinzi wa malango; 39  na kuhani Sadoki+ na makuhani wenzake walikuwa mbele ya hema la ibada la Yehova mahali pa juu kule Gibeoni+ 40  ili wamtolee Yehova kwa ukawaida dhabihu za kuteketezwa kwenye madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa, asubuhi na jioni, na kufanya mambo yote yaliyoandikwa katika Sheria ya Yehova aliyowaamuru Waisraeli wafuate.+ 41  Walikuwa pamoja na Hemani na Yeduthuni+ na wanaume wengine waliochaguliwa na kutajwa majina ili wamshukuru Yehova,+ kwa sababu “upendo wake mshikamanifu unadumu milele”;+ 42  nao walikuwa pamoja na Hemani+ na Yeduthuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na ala zilizotumiwa kumsifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yeduthuni+ walikuwa langoni. 43  Kisha watu wote wakaenda nyumbani kwao, na Daudi akaenda kuwabariki watu wa nyumba yake mwenyewe.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wamkumbuke.”
Au “alichangia.”
Au “mpigieni muziki.”
Au labda, “Zungumzeni kuhusu.”
Au “uwepo.”
Au “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Neno aliloamuru.”
Au “adhama.”
Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”
Au “Mwabuduni.”
Au “kutikiswa; kufanywa ipepesuke.”
Au “amekuja.”
Au “milele na milele.”
Au “Na iwe hivyo!”
Au “na ala za wimbo wa.”