Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 17:1-27

  • Daudi hatajenga hekalu (1-6)

  • Agano pamoja na Daudi kwa ajili ya ufalme (7-15)

  • Sala ya Daudi ya shukrani (16-27)

17  Mara tu Daudi alipoanza kuishi katika nyumba yake mwenyewe,* alimwambia hivi nabii Nathani:+ “Mimi hapa ninaishi katika nyumba ya mierezi+ huku sanduku la agano la Yehova likiwa ndani ya vitambaa vya mahema.”+  Nathani akamwambia Daudi: “Fanya jambo lolote lililo moyoni mwako, kwa sababu Mungu wa kweli yuko pamoja nawe.”  Usiku huohuo, neno hili la Mungu likamjia Nathani:  “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Si wewe utakayenijengea nyumba nitakayokaa ndani yake.+  Kwa maana sijakaa ndani ya nyumba tangu siku nilipowatoa nje Waisraeli mpaka leo, bali nimekuwa nikihama hema moja hadi hema lingine na kutoka hema moja la ibada hadi hema lingine la ibada.*+  Wakati wote nilipotembea na Waisraeli wote, je, niliwahi wakati wowote kumuuliza mwamuzi yeyote wa Israeli niliyemweka awachunge watu wangu, ‘Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?’”’  “Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo, uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+  Nami nitakuwa pamoja nawe popote utakapoenda,+ nami nitawaangamiza maadui wako wote kutoka mbele yako;+ nami nitakujengea jina kama jina la watu maarufu duniani.+  Nitachagua mahali kwa ajili ya watu wangu Waisraeli na kuwaweka humo, nao wataishi humo na hawatasumbuliwa tena; na watu waovu hawatawakandamiza* tena kama walivyofanya zamani,+ 10  tangu siku nilipowaweka waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli.+ Nami nitawashinda maadui wako wote.+ Pia, ninakuambia, ‘Yehova atakujengea nyumba.’* 11  “‘“Siku zako zitakapokwisha nawe uzikwe pamoja na mababu zako, nitamwinua mzao wako* baada yako, mmoja wa wana wako,+ nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 12  Yeye ndiye atakayenijengea nyumba,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme milele.+ 13  Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Sitauondoa upendo wangu mshikamanifu kutoka kwake+ kama nilivyouondoa kutoka kwa yule aliyekutangulia.+ 14  Nitamfanya asimame katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele,+ na kiti chake cha ufalme kitadumu milele.”’”+ 15  Nathani alimwambia Daudi maneno hayo yote na maono hayo yote. 16  Ndipo Mfalme Daudi akaingia na kuketi mbele za Yehova na kusema: “Mimi ni nani, Ee Yehova Mungu? Na nyumba yangu ni nini hivi kwamba umenileta mpaka hapa nilipofika?+ 17  Na kana kwamba hilo halitoshi, Ee Mungu, unasema pia kwamba nyumba yangu mimi mtumishi wako itadumu kwa muda mrefu,+ nawe umeniona kuwa mtu anayepaswa kukwezwa zaidi,* Ee Yehova Mungu. 18  Mimi mtumishi wako Daudi nitakwambia nini zaidi kuhusu heshima uliyonipa na wewe unanijua vizuri sana mimi mtumishi wako?+ 19  Ee Yehova, kwa ajili yangu mimi mtumishi wako na kupatana na moyo wako* umetenda mambo haya yote makuu kwa kufunua ukuu wako.+ 20  Ee Yehova, hakuna aliye kama wewe,+ na hakuna Mungu ila wewe;+ mambo yote tuliyosikia kwa masikio yetu yanathibitisha jambo hilo. 21  Na kuna taifa gani lingine duniani lililo kama watu wako Waisraeli?+ Wewe Mungu wa kweli ulienda na kuwakomboa wakiwa watu wako.+ Ulijijengea jina kwa matendo yako makuu na yenye kuogopesha,+ ukayafukuza mataifa kutoka mbele ya watu wako+ uliowakomboa kutoka Misri. 22  Uliwafanya watu wako Waisraeli wawe watu wako milele;+ na wewe, Ee Yehova, ukawa Mungu wao.+ 23  Sasa, Ee Yehova, ahadi uliyotoa kunihusu mimi mtumishi wako na nyumba yangu na ithibitike kuwa ya uaminifu milele, na ufanye kama ulivyoahidi.+ 24  Jina lako na lidumu na kukwezwa+ milele, ili watu waseme, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, ni Mungu kwa Israeli,’ na nyumba yangu mimi mtumishi wako Daudi na iimarishwe kabisa mbele zako.+ 25  Kwa maana wewe, Mungu wangu, umenifunulia mimi mtumishi wako kusudi lako la kunijengea nyumba.* Ndiyo sababu mimi mtumishi wako nina ujasiri wa kutoa sala hii kwako. 26  Na sasa, Ee Yehova, wewe ndiye Mungu wa kweli, nawe umeahidi mambo hayo mema kunihusu mimi mtumishi wako. 27  Basi na ufurahie kuibariki nyumba yangu mimi mtumishi wako, na idumu milele mbele zako, kwa sababu wewe, Ee Yehova, umeibariki, nayo imebarikiwa milele.”

Maelezo ya Chini

Au “jumba lake mwenyewe la mfalme.”
Labda inamaanisha “kutoka kambi moja ya mahema hadi nyingine na kutoka eneo moja la kuishi hadi lingine.”
Tnn., “hawatawachosha.”
Au “ukoo wa kifalme.”
Tnn., “nitainua mbegu yako.”
Au “mtu mwenye cheo kikubwa.”
Au “kulingana na mapenzi yako.”
Au “ukoo wa kifalme.”