Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 18:1-17

  • Ushindi mbalimbali wa Daudi (1-13)

  • Wasimamizi wa Daudi (14-17)

18  Wakati fulani baadaye, Daudi aliwashinda Wafilisti na kuwatiisha, akachukua jiji la Gathi+ na miji yake kutoka mikononi mwa Wafilisti.+  Kisha akawashinda Wamoabu,+ na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na kumletea ushuru.+  Daudi alimshinda Mfalme Hadadezeri+ wa Soba+ karibu na Hamathi+ alipokuwa akienda kuimarisha mamlaka yake katika eneo la Mto Efrati.+  Daudi akateka magari 1,000 ya vita, wapanda farasi 7,000, na wanajeshi 20,000 wanaotembea kwa miguu.+ Kisha Daudi akawakata farasi wote mishipa ya miguu isipokuwa farasi 100 waliokokota magari.+  Wasiria wa Damasko walipokuja kumsaidia Mfalme Hadadezeri wa Soba, Daudi aliwaua Wasiria 22,000.+  Halafu Daudi akaweka kambi za kijeshi kule Siria ya Damasko, na Wasiria wakawa watumishi wa Daudi na kumletea ushuru. Yehova alimpa Daudi ushindi* popote alipoenda.+  Isitoshe, Daudi alichukua ngao za mviringo za dhahabu kutoka kwa watumishi wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.  Daudi alichukua shaba nyingi sana kutoka Tibhathi na Kuni, majiji ya Hadadezeri. Sulemani aliitumia kutengenezea Bahari ya Shaba,+ nguzo, na vyombo vya shaba.+  Mfalme Tou wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi alikuwa amelishinda jeshi lote la Mfalme Hadadezeri+ wa Soba,+ 10  mara moja alimtuma Hadoramu mwana wake kwa Mfalme Daudi ili amjulie hali na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda (kwa maana mara nyingi Hadadezeri alimshambulia Tou), na Hadoramu alimletea Daudi kila aina ya vitu vya dhahabu, fedha, na shaba. 11  Mfalme Daudi akavitakasa vitu hivyo ili viwe vya Yehova,+ pamoja na fedha na dhahabu aliyokuwa amechukua kutoka kwa mataifa yote: kutoka kwa Waedomu na Wamoabu, kutoka kwa Waamoni,+ Wafilisti,+ na Waamaleki.+ 12  Abishai+ mwana wa Seruya+ aliwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.+ 13  Aliweka kambi za kijeshi huko Edomu, na Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi.+ Yehova alimpa Daudi ushindi* popote alipoenda.+ 14  Daudi akaendelea kutawala Israeli yote,+ naye aliwatawala watu wake wote kwa haki na uadilifu.+ 15  Yoabu mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi,+ Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alifanya kazi ya kuweka kumbukumbu, 16  Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavsha alikuwa mwandishi. 17  Benaya mwana wa Yehoyada aliwasimamia Wakerethi+ na Wapelethi.+ Na wana wa Daudi walikuwa na cheo cha kwanza baada ya mfalme.

Maelezo ya Chini

Au “wokovu.”
Au “wokovu.”