Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 22:1-19

  • Daudi afanya matayarisho ya kujenga hekalu (1-5)

  • Daudi ampa Sulemani maagizo (6-16)

  • Wakuu waamriwa wamsaidie Sulemani (17-19)

22  Ndipo Daudi akasema: “Hii ndiyo nyumba ya Yehova Mungu wa kweli, na hii ndiyo madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa kwa ajili ya Waisraeli.”+  Kisha Daudi akaagiza wakaaji wageni+ waliokuwa katika nchi ya Israeli wakusanywe, naye akawapa kazi ya kukata mawe na kuyachonga ili yatumiwe kujenga nyumba ya Mungu wa kweli.+  Daudi pia alitayarisha kiasi kikubwa sana cha chuma ili kitumiwe kutengenezea misumari ya milango ya malango na pia vibanio, na shaba nyingi sana hivi kwamba haingeweza kupimwa,+  na pia mbao za mierezi+ zisizohesabika, kwa maana Wasidoni+ na Watiro+ walimletea Daudi mbao nyingi sana za mierezi.  Daudi akasema: “Mwanangu Sulemani ni mchanga na hana uzoefu,*+ na nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Yehova itakuwa na utukufu usio na kifani,+ hivi kwamba umaarufu na umaridadi+ wake utajulikana katika nchi zote.+ Kwa hiyo, nitafanya matayarisho kwa ajili yake.” Basi Daudi akatayarisha vifaa vingi sana kabla ya kifo chake.  Isitoshe, alimwita Sulemani mwanawe na kumwagiza amjengee nyumba Yehova Mungu wa Israeli.  Daudi alimwambia hivi Sulemani mwanawe: “Moyo wangu ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu.+  Lakini neno la Yehova lilinijia likisema, ‘Umemwaga damu nyingi sana, nawe umepigana vita vikubwa. Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ kwa maana umemwaga damu nyingi sana duniani mbele zangu.  Tazama! Utazaa mwana+ atakayekuwa mtu wa amani,* nami nitampumzisha kutokana na maadui wake wote wanaomzunguka,+ kwa maana jina lake litakuwa Sulemani,*+ nami nitawapa Waisraeli amani na utulivu katika siku zake.+ 10  Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu.+ Atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake.+ Nitakiimarisha kabisa kiti cha ufalme wake juu ya Israeli milele.’+ 11  “Sasa, mwanangu, Yehova na awe pamoja nawe, nawe ufanikiwe na kujenga nyumba ya Yehova Mungu wako, kama alivyosema kukuhusu wewe.+ 12  Ila tu Yehova akupe busara na uelewaji+ atakapokupa mamlaka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Yehova Mungu wako.+ 13  Utafanikiwa ikiwa utashika kwa uangalifu masharti+ na sheria* ambazo Yehova alimwamuru Musa awape Waisraeli.+ Uwe jasiri na imara. Usiogope wala usihofu.+ 14  Tazama, nimejitahidi kabisa kufanya matayarisho kwa ajili ya nyumba ya Yehova, nimeweka talanta 100,000* za dhahabu na talanta 1,000,000 za fedha na shaba nyingi sana+ na chuma hivi kwamba haviwezi kupimwa, nami nimetayarisha mbao na mawe,+ lakini utaongeza vitu hivyo. 15  Una wafanyakazi wengi sana—wakataji wa mawe, waashi,+ maseremala, na wafanyakazi wenye ustadi wa kila aina.+ 16  Dhahabu, fedha, shaba, na chuma haviwezi kupimwa.+ Haya, anza kazi, Yehova na awe pamoja nawe.”+ 17  Kisha Daudi akawaagiza wakuu wote wa Israeli wamsaidie Sulemani mwanawe, akawaambia: 18  “Je, Yehova, Mungu wenu hayuko pamoja nanyi, na je, hajawapumzisha pande zote? Kwa maana aliwatia mikononi mwangu wakaaji wa nchi, na nchi imetiishwa mbele za Yehova na mbele ya watu wake. 19  Basi azimieni kwa moyo wenu wote na nafsi* yenu yote kumtafuta Yehova Mungu wenu,+ anzeni kujenga mahali patakatifu pa Yehova Mungu wa kweli,+ ili mlilete sanduku la agano la Yehova na vyombo vitakatifu vya Mungu wa kweli+ katika nyumba iliyojengwa kwa ajili ya jina la Yehova.”+

Maelezo ya Chini

Au “hana uwezo.”
Tnn., “mtulivu.”
Linatokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Amani.”
Tnn., “hukumu.”
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Angalia Kamusi.