Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 23:1-32

  • Daudi awapanga Walawi (1-32)

    • Haruni na wanawe watengwa kando (13)

23  Daudi alipokuwa amezeeka na kukaribia mwisho wa maisha yake,* alimweka Sulemani mwanawe kuwa mfalme wa Israeli.+  Akawakusanya wakuu wote wa Israeli, makuhani,+ na Walawi.+  Walawi waliokuwa na umri wa miaka 30 na zaidi walihesabiwa;+ idadi yao, mwanamume kwa mwanamume,* ilikuwa 38,000.  Walawi 24,000 kati yao walikuwa wasimamizi wa kazi ya nyumba ya Yehova, na kulikuwa na maofisa na waamuzi 6,000,+  na walinzi 4,000 wa malango,+ na watu 4,000 walimsifu+ Yehova kwa ala ambazo Daudi alisema hivi kuzihusu: “Nilizitengeneza ili zitumiwe kumsifu Mungu.”  Kisha Daudi akawapanga* katika vikundi+ kulingana na wana hawa wa Lawi: Gershoni, Kohathi, na Merari.+  Kutoka kwa Wagershoni: Ladani na Shimei.  Wana wa Ladani walikuwa Yehieli kiongozi wao, Zethamu, na Yoeli,+ wana watatu.  Wana wa Shimei walikuwa Shelomothi, Hazieli, na Harani, wana watatu. Hao walikuwa viongozi wa koo* za Ladani. 10  Na wana wa Shimei walikuwa Yahathi, Zina, Yeushi, na Beria. Hao wanne walikuwa wana wa Shimei. 11  Yahathi alikuwa kiongozi na wa pili alikuwa Ziza. Lakini kwa kuwa Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi, walihesabiwa kama ukoo* mmoja nao walipewa majukumu yaleyale. 12  Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari,+ Hebroni, na Uzieli,+ wana wanne. 13  Wana wa Amramu walikuwa Haruni+ na Musa.+ Lakini Haruni alitengwa kando daima+ ili atakase Patakatifu Zaidi, yeye na wanawe, ili watoe dhabihu mbele za Yehova, wamhudumie, na kutangaza baraka katika jina lake sikuzote.+ 14  Majina ya wana wa Musa, mtu wa Mungu wa kweli, yaliorodheshwa miongoni mwa kabila la Walawi. 15  Wana wa Musa walikuwa Gershomu+ na Eliezeri.+ 16  Shebueli+ alikuwa kiongozi wa wana wa Gershomu. 17  Rehabia+ alikuwa kiongozi wa wazao* wa Eliezeri; Eliezeri hakuwa na wana wengine, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana. 18  Shelomithi+ alikuwa kiongozi wa wana wa Ishari.+ 19  Wana wa Hebroni walikuwa Yeria kiongozi wao, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.+ 20  Wana wa Uzieli+ walikuwa Mika kiongozi wao na wa pili Ishia. 21  Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.+ Wana wa Mali walikuwa Eleazari na Kishi. 22  Eleazari alikufa, lakini hakuwa na wana ila mabinti tu. Basi wana wa Kishi, watu wao wa ukoo,* waliwaoa. 23  Wana wa Mushi walikuwa Mali, Ederi, na Yeremothi, wana watatu. 24  Hao ndio waliokuwa wana wa Lawi kulingana na koo zao,* viongozi wa koo zao,* wale walioandikishwa na kuhesabiwa na kuorodheshwa kulingana na majina yao na ambao walitekeleza kazi ya utumishi wa nyumba ya Yehova, kuanzia umri wa miaka 20 na zaidi. 25  Kwa maana Daudi alikuwa amesema hivi: “Yehova Mungu wa Israeli amewapumzisha watu wake,+ naye atakaa Yerusalemu milele.+ 26  Pia Walawi hawatalazimika kubeba hema la ibada wala chombo chake chochote kinachotumiwa katika utumishi wa hema hilo.”+ 27  Kwa maana kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi wenye umri wa miaka 20 na zaidi walihesabiwa. 28  Jukumu lao lilikuwa kuwasaidia wana wa Haruni+ katika utumishi wa nyumba ya Yehova, kusimamia nyua,+ vyumba vya kulia chakula, kukitakasa kila kitu kitakatifu, na kazi yoyote iliyohitaji kufanywa katika utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 29  Waliwasaidia katika kazi ya mikate ya tabaka,*+ unga laini wa toleo la nafaka, mikate myembamba isiyo na chachu,+ keki zilizookwa, unga wa kukandwa uliochanganywa,+ na vipimo vyote vya wingi na ukubwa. 30  Walipaswa kusimama asubuhi baada ya asubuhi+ ili kumshukuru na kumsifu Yehova, na walipaswa kufanya hivyo jioni pia.+ 31  Walisaidia wakati wowote ambapo dhabihu za kuteketezwa zilitolewa kwa Yehova nyakati za Sabato,+ miezi mipya,+ na wakati wa sherehe za majira,+ kulingana na idadi iliyoamriwa katika sheria kuzihusu, nao walifanya hivyo kwa ukawaida mbele za Yehova. 32  Walitimiza pia majukumu yao kuhusiana na hema la mkutano, mahali patakatifu, na kuhusiana na ndugu zao wana wa Haruni katika utumishi wa nyumba ya Yehova.

Maelezo ya Chini

Tnn., “akiwa amezeeka na akiwa amejaa siku.”
Tnn., “kichwa kwa kichwa.”
Au “akawagawa.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “wana.”
Tnn., “ndugu zao.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, mikate ya wonyesho.