Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 24:1-31

  • Daudi awapanga makuhani katika vikundi 24 (1-19)

  • Kazi nyingine za Walawi (20-31)

24  Basi hivi ndivyo vilivyokuwa vikundi vya wazao wa Haruni: Wana wa Haruni walikuwa Nadabu, Abihu,+ Eleazari, na Ithamari.+  Hata hivyo, Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao,+ nao hawakuwa na wana wowote; lakini Eleazari+ na Ithamari waliendelea kutumikia wakiwa makuhani.  Daudi, pamoja na Sadoki+ kutoka kwa wana wa Eleazari na Ahimeleki kutoka kwa wana wa Ithamari, waliwagawa katika vikundi kulingana na mpangilio wao wa utumishi.  Kwa kuwa wana wa Eleazari walikuwa na viongozi wengi kuliko wana wa Ithamari, waliwagawa ifaavyo: Wana wa Eleazari walikuwa na viongozi 16 wa koo zao,* na wana wa Ithamari walikuwa na viongozi 8 wa koo zao.*  Pia, waliwagawa kwa kura,+ kikundi kimoja pamoja na kingine, kwa maana kulikuwa na wakuu wa mahali patakatifu na wakuu wa Mungu wa kweli kutoka kwa wana wa Eleazari na pia wana wa Ithamari.  Kisha Shemaya mwana wa Nethaneli mwandishi wa Walawi akaandika majina yao mbele ya mfalme, wakuu, kuhani Sadoki,+ Ahimeleki+ mwana wa Abiathari,+ na viongozi wa koo* za makuhani na za Walawi, ukoo* mmoja ulichaguliwa kutoka kwa Eleazari na ukoo mmoja ulichaguliwa kutoka kwa Ithamari.  Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu; ya pili Yedaya,  ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,  ya tano Malkiya, ya sita Miyamini, 10  ya saba Hakozi, ya nane Abiya,+ 11  ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania, 12  ya 11 Eliashibu, ya 12 Yakimu, 13  ya 13 Hupa, ya 14 Yeshebeabu, 14  ya 15 Bilga, ya 16 Imeri, 15  ya 17 Heziri, ya 18 Hapisesi, 16  ya 19 Pethahia, ya 20 Yehezkeli, 17  ya 21 Yakini, ya 22 Gamuli, 18  ya 23 Delaya, ya 24 Maazia. 19  Huo ndio uliokuwa mpangilio wao wa utumishi+ walipokuwa wakiingia katika nyumba ya Yehova kulingana na utaratibu uliowekwa na Haruni babu yao, kama Yehova Mungu wa Israeli alivyokuwa amemwamuru. 20  Hawa ndio Walawi waliobaki: kutoka kwa wana wa Amramu+ kulikuwa na Shubaeli;+ kutoka kwa wana wa Shubaeli, Yehdeya; 21  wana wa Rehabia:+ kutoka kwa wana wa Rehabia, Ishia kiongozi wao; 22  kutoka kwa Waishari, Shelomothi;+ kutoka kwa wana wa Shelomothi, Yahathi; 23  na kutoka kwa wana wa Hebroni, Yeria+ kiongozi wao, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, wa nne Yekameamu; 24  kutoka kwa wana wa Uzieli, Mika; kutoka kwa wana wa Mika, Shamiri. 25  Ndugu ya Mika alikuwa Ishia; kutoka kwa wana wa Ishia, Zekaria. 26  Wana wa Merari+ walikuwa Mali na Mushi; kutoka kwa wana wa Yaazia, Beno. 27  Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibri; 28  kutoka kwa Mali, Eleazari, ambaye hakuwa na wana wowote;+ 29  Kishi: kutoka kwa wana wa Kishi, Yerahmeeli; 30  na wana wa Mushi walikuwa Mali, Ederi, na Yerimothi. Hao ndio waliokuwa wana wa Lawi kulingana na koo zao.* 31  Na pia walipiga kura+ kama walivyofanya ndugu zao wana wa Haruni mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki, na viongozi wa koo* za makuhani na za Walawi. Kuhusiana na koo,* kiongozi alikuwa sawa kabisa na ndugu yake mdogo.

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.