Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 4:1-43

  • Wazao wengine wa Yuda (1-23)

    • Yabesi na sala yake (9, 10)

  • Wazao wa Simeoni (24-43)

4  Wana wa Yuda walikuwa Perezi,+ Hezroni,+ Karmi, Huru,+ na Shobali.+  Reaya mwana wa Shobali alimzaa Yahathi; Yahathi akamzaa Ahumai na Lahadi. Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wasorathi.+  Hawa ndio waliokuwa wana wa baba ya Etamu:+ Yezreeli, Ishma, na Idbashi (na dada yao aliitwa Haselelponi),  Penueli alimzaa Gedori, na Ezeri akamzaa Husha. Hao ndio waliokuwa wana wa Huru,+ mzaliwa wa kwanza wa Efratha na baba ya Bethlehemu.+  Ashuri+ baba ya Tekoa+ alikuwa na wake wawili, Hela na Naara.  Naara akamzalia Ashuri wana hawa: Ahuzamu, Heferi, Temeni, na Haahashtari. Hao ndio waliokuwa wana wa Naara.  Na wana wa Hela walikuwa Serethi, Ishari, na Ethnani.  Kosi alimzaa Anubu, Zobeba, na familia za Aharheli mwana wa Harumi.  Yabesi aliheshimiwa sana kuliko ndugu zake; na mama yake alimwita jina Yabesi, akisema: “Nilimzaa kwa uchungu.”* 10  Yabesi akamlilia Mungu wa Israeli, akisema: “Laiti ungenibariki na kupanua eneo langu na kuuruhusu mkono wako uwe pamoja nami na kuniokoa kutoka katika msiba, ili msiba huo usinidhuru!” Basi Mungu akatimiza ombi lake. 11  Kelubu ndugu ya Shuha akamzaa Mehiri, aliyekuwa baba ya Eshtoni. 12  Eshtoni akamzaa Beth-rafa, Pasea, na Tehina, baba ya Ir-nahashi. Hao ndio waliokuwa wanaume wa Reka. 13  Na wana wa Kenasi walikuwa Othnieli+ na Seraya, na mwana* wa Othnieli alikuwa Hathathi. 14  Meonothai akamzaa Ofra. Seraya akamzaa Yoabu baba ya Ge-harashimu,* walipewa jina hilo kwa sababu walikuwa mafundi. 15  Wana wa Kalebu+ mwana wa Yefune walikuwa Iru, Ela, na Naamu; na mwana* wa Ela alikuwa Kenasi. 16  Wana wa Yehaleleli walikuwa Zifu, Zifa, Tiria, na Asareli. 17  Wana wa Ezra walikuwa Yetheri, Meredi, Eferi, na Yaloni; alishika* mimba na kumzaa Miriamu, Shamai, na Ishba baba ya Eshtemoa. 18  (Na mke wake Myahudi alimzaa Yeredi baba ya Gedori, Heberi baba ya Soko, na Yekuthieli baba ya Zanoa.) Hao ndio waliokuwa wana wa Bithia, binti ya Farao, aliyeolewa na Meredi. 19  Wana wa mke wa Hodia, dada ya Nahamu, walikuwa baba za Keila Mgarmi na Eshtemoa Mmaakathi. 20  Na wana wa Shimoni walikuwa Amnoni, Rina, Ben-hanani, na Tiloni. Na wana wa Ishi walikuwa Zohethi na Ben-zohethi. 21  Wana wa Shela+ mwana wa Yuda walikuwa Eri baba ya Leka, Laada baba ya Maresha, na familia za wafumaji wa vitambaa bora wa nyumba ya Ashbea, 22  na Yokimu, wanaume wa Kozeba, Yoashi, na Sarafi, waliowaoa wanawake Wamoabu, na Yashubi-lehemu. Habari hizi ni za zamani za kale.* 23  Hao ndio wafinyanzi walioishi Netaimu na Gedera. Waliishi huko na kumtumikia mfalme. 24  Wana wa Simeoni+ walikuwa Nemueli, Yamini, Yaribu, Zera, na Shauli.+ 25  Mwana wa Shauli alikuwa Shalumu, mwana wa Shalumu alikuwa Mibsamu, na mwana wa Mibsamu alikuwa Mishma. 26  Na wana wa Mishma walikuwa Hamueli, Zakuri mwana wa Hamueli, na Shimei mwana wa Zakuri. 27  Na Shimei alikuwa na wana 16 na mabinti 6; lakini ndugu zake hawakuwa na wana wengi, na hakuna familia yao yoyote iliyokuwa na wana wengi kama wanaume wa Yuda.+ 28  Waliishi Beer-sheba,+ Molada,+ Hasar-shuali,+ 29  Bilha, Esemu,+ Toladi, 30  Bethueli,+ Horma,+ Siklagi,+ 31  Beth-markabothi, Hasar-susimu,+ Beth-biri, na Shaaraimu. Hayo yalikuwa majiji yao mpaka wakati wa utawala wa Daudi. 32  Waliishi Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni, na Ashani,+ majiji matano, 33  pamoja na vijiji vyao vilivyozunguka majiji hayo mpaka Baali. Hizo ndizo orodha za koo zao zilizoandikishwa na mahali walipoishi. 34  Na Meshobabu, Yamleki, Yosha mwana wa Amazia, 35  Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia mwana wa Seraya mwana wa Asieli, 36  na Elioenai, Yaakoba, Yeshohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya, 37  na Ziza mwana wa Shifi mwana wa Aloni mwana wa Yedaya mwana wa Shimri mwana wa Shemaya; 38  watu hao waliotajwa kwa majina walikuwa wakuu katika koo zao, na idadi ya watu katika nyumba ya mababu zao iliongezeka. 39  Nao walienda kwenye njia ya kuingia Gedori, upande wa mashariki wa bonde, ili kutafuta malisho ya wanyama wao. 40  Hatimaye walipata malisho mazuri yenye majani mengi, na nchi ilikuwa kubwa, yenye utulivu, na amani. Wahamu ndio walioishi katika nchi hiyo awali.+ 41  Watu hao ambao majina yao yameorodheshwa walikuja katika siku za utawala wa Mfalme Hezekia+ wa Yuda, wakayabomoa mahema ya Wahamu na Wameunimu waliokuwa huko. Waliwaangamiza tangu siku hiyo; wakachukua eneo lao kwa sababu lilikuwa na malisho kwa ajili ya wanyama wao. 42  Baadhi ya watu wa kabila la Simeoni, wanaume 500, walienda kwenye Mlima Seiri+ wakiwa na Pelatia, Nearia, Refaya, na Uzieli, wana wa Ishi ambao waliwaongoza. 43  Kisha wakawaangamiza Waamaleki+ waliobaki ambao walikuwa wametoroka, nao wamekuwa wakiishi huko mpaka leo.

Maelezo ya Chini

Huenda jina Yabesi linahusiana na neno la Kiebrania linalomaanisha “uchungu.”
Tnn., “wana.”
Maana yake “Bonde la Mafundi.”
Tnn., “wana.”
Inawezekana ni Bithia anayetajwa katika mstari wa 18.
Au “Maneno haya ni ya utamaduni wa kale.”