Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 6:1-81

  • Wazao wa Lawi (1-30)

  • Waimbaji wa hekaluni (31-47)

  • Wazao wa Haruni (48-53)

  • Makao ya Walawi (54-81)

6  Wana wa Lawi+ walikuwa Gershoni, Kohathi,+ na Merari.+  Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari,+ Hebroni, na Uzieli.+  Watoto* wa Amramu+ walikuwa Haruni,+ Musa,+ na pia Miriamu.+ Na wana wa Haruni walikuwa Nadabu, Abihu,+ Eleazari,+ na Ithamari.+  Eleazari alimzaa Finehasi;+ Finehasi akamzaa Abishua.  Abishua akamzaa Buki; Buki akamzaa Uzi.  Uzi akamzaa Zeraya; Zeraya akamzaa Merayothi.  Merayothi akamzaa Amaria; Amaria akamzaa Ahitubu.+  Ahitubu akamzaa Sadoki;+ Sadoki akamzaa Ahimaazi.+  Ahimaazi akamzaa Azaria; Azaria akamzaa Yohanani. 10  Yohanani akamzaa Azaria. Alitumikia akiwa kuhani katika nyumba ambayo Sulemani alijenga Yerusalemu. 11  Azaria akamzaa Amaria; Amaria akamzaa Ahitubu. 12  Ahitubu akamzaa Sadoki;+ Sadoki akamzaa Shalumu. 13  Shalumu akamzaa Hilkia;+ Hilkia akamzaa Azaria. 14  Azaria akamzaa Seraya;+ Seraya akamzaa Yehosadaki.+ 15  Na Yehosadaki alipelekwa uhamishoni wakati Yehova alipowapeleka watu wa Yuda na Yerusalemu uhamishoni kwa mkono wa Nebukadneza. 16  Wana wa Lawi walikuwa Gershomu,* Kohathi, na Merari. 17  Haya ndiyo majina ya wana wa Gershomu: Libni na Shimei.+ 18  Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+ 19  Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi kulingana na mababu zao:+ 20  kutoka katika ukoo wa Gershomu,+ Libni mwana wa Gershomu, Yahathi mwana wa Libni, Zima mwana wa Yahathi, 21  Yoa mwana wa Zima, Ido mwana wa Yoa, Zera mwana wa Ido, Yeatherai mwana wa Zera. 22  Wana* wa Kohathi walikuwa Aminadabu mwanawe, Kora+ mwana wa Aminadabu, Asiri mwana wa Kora, 23  Elkana mwana wa Asiri, Ebiasafu+ mwana wa Elkana, Asiri mwana wa Ebiasafu, 24  Tahathi mwana wa Asiri, Urieli mwana wa Tahathi, Uzia mwana wa Urieli, na Shauli mwana wa Uzia. 25  Wana wa Elkana walikuwa Amasai na Ahimothi. 26  Kwa habari ya Elkana, wana wa Elkana walikuwa Zofai mwanawe, Nahathi mwana wa Zofai, 27  Eliabu mwana wa Nahathi, Yerohamu mwana wa Eliabu, Elkana+ mwana wa Yerohamu. 28  Wana wa Samweli+ walikuwa Yoeli mzaliwa wa kwanza na wa pili Abiya.+ 29  Wana* wa Merari walikuwa Mali,+ Libni mwana wa Mali, Shimei mwana wa Libni, Uza mwana wa Shimei, 30  Shimei mwana wa Uza, Hagia mwana wa Shimei, na Asaya mwana wa Hagia. 31  Hao ndio watu ambao Daudi aliwaweka ili waongoze uimbaji katika nyumba ya Yehova baada ya Sanduku kuletwa likae* humo.+ 32  Ndio waliokuwa na jukumu la kusimamia uimbaji katika hema la ibada, yaani, hema la mkutano mpaka Sulemani alipoijenga nyumba ya Yehova huko Yerusalemu,+ nao walitekeleza utumishi wao kulingana na maagizo waliyopewa.+ 33  Hawa ndio wanaume waliotumikia pamoja na wana wao: kutoka katika ukoo wa Wakohathi, Hemani+ mwimbaji, mwana wa Yoeli+ mwana wa Samweli 34  mwana wa Elkana+ mwana wa Yerohamu mwana wa Elieli mwana wa Toa 35  mwana wa Sufu mwana wa Elkana mwana wa Mahathi mwana wa Amasai 36  mwana wa Elkana mwana wa Yoeli mwana wa Azaria mwana wa Sefania 37  mwana wa Tahathi mwana wa Asiri mwana wa Ebiasafu mwana wa Kora 38  mwana wa Ishari mwana wa Kohathi mwana wa Lawi mwana wa Israeli. 39  Asafu+ ndugu yake alisimama kwenye mkono wake wa kulia; Asafu alikuwa mwana wa Berekia mwana wa Shimea 40  mwana wa Mikaeli mwana wa Baaseya mwana wa Malkiya 41  mwana wa Ethni mwana wa Zera mwana wa Adaya 42  mwana wa Ethani mwana wa Zima mwana wa Shimei 43  mwana wa Yahathi mwana wa Gershomu mwana wa Lawi. 44  Wazao wa Merari+ ndugu zao walikuwa kwenye mkono wake wa kushoto; kulikuwa na Ethani+ mwana wa Kishi mwana wa Abdi mwana wa Maluku 45  mwana wa Hashabia mwana wa Amazia mwana wa Hilkia 46  mwana wa Amzi mwana wa Bani mwana wa Shemeri 47  mwana wa Mali mwana wa Mushi mwana wa Merari mwana wa Lawi. 48  Ndugu zao Walawi waliwekwa* ili watekeleze utumishi wote wa hema la ibada, nyumba ya Mungu wa kweli.+ 49  Haruni na wanawe+ walifukiza moshi wa dhabihu kwenye madhabahu ya dhabihu ya kuteketezwa+ na kwenye madhabahu ya uvumba,+ wakitekeleza majukumu yaliyohusiana na vitu vitakatifu kabisa, ili kufunika dhambi za Waisraeli,+ kulingana na yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu wa kweli alikuwa ameamuru. 50  Hawa ndio waliokuwa wazao wa Haruni:+ Eleazari mwanawe, Finehasi mwana wa Eleazari,+ Abishua mwana wa Finehasi, 51  Buki mwana wa Abishua, Uzi mwana wa Buki, Zeraya mwana wa Uzi, 52  Merayothi mwana wa Zeraya, Amaria mwana wa Merayothi, Ahitubu+ mwana wa Amaria, 53  Sadoki+ mwana wa Ahitubu, na Ahimaazi mwana wa Sadoki. 54  Haya ndiyo yaliyokuwa makao yao kulingana na kambi zao* katika eneo lao: wazao wa Haruni waliokuwa wa ukoo wa Wakohathi, waliangukiwa na kura ya kwanza, 55  waliwapa Hebroni+ katika nchi ya Yuda, pamoja na malisho yake. 56  Lakini mashamba ya jiji na vijiji vyake walimpa Kalebu+ mwana wa Yefune. 57  Na wazao wa Haruni walipewa majiji haya ya* makimbilio:+ Hebroni,+ na pia Libna+ na malisho yake, Yatiri,+ Eshtemoa na malisho yake,+ 58  Hileni na malisho yake, Debiri+ na malisho yake, 59  Ashani+ na malisho yake, na Beth-shemeshi+ na malisho yake; 60  na kutoka katika kabila la Benjamini, Geba+ na malisho yake, Alemethi na malisho yake, na Anathothi+ na malisho yake. Majiji yao yote kwa ajili ya koo zao yalikuwa majiji 13.+ 61  Wakohathi waliobaki walipewa* majiji kumi, kutoka katika ukoo wa kabila, kutoka katika nusu ya kabila, nusu ya kabila la Manase.+ 62  Wagershomu kulingana na koo zao walipewa majiji 13 kutoka katika kabila la Isakari, kabila la Asheri, kabila la Naftali, na kabila la Manase kule Bashani.+ 63  Wamerari kulingana na koo zao walipewa majiji 12 kutoka katika kabila la Rubeni, kabila la Gadi, na kabila la Zabuloni.+ 64  Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi majiji hayo na malisho yake.+ 65  Isitoshe, waliwapa kwa kura majiji hayo kutoka katika kabila la Yuda, kabila la Simeoni, na kabila la Benjamini, ambayo yametajwa majina yao. 66  Baadhi ya koo za Wakohathi zilipewa majiji kutoka katika kabila la Efraimu, yakawa maeneo yao.+ 67  Waliwapa majiji ya* makimbilio, Shekemu+ na malisho yake katika eneo lenye milima la Efraimu, Gezeri+ na malisho yake, 68  Yokmeamu na malisho yake, Beth-horoni+ na malisho yake, 69  Aiyaloni+ na malisho yake, na Gath-rimoni+ na malisho yake; 70  na koo zilizobaki za Wakohathi zilipewa kutoka katika nusu ya kabila la Manase, Aneri na malisho yake na Bileamu na malisho yake. 71  Wagershomu walipewa kutoka katika ukoo wa nusu ya kabila la Manase, Golani+ kule Bashani na malisho yake na Ashtarothi na malisho yake;+ 72  na kutoka katika kabila la Isakari, Kedeshi na malisho yake, Daberathi+ na malisho yake,+ 73  Ramothi na malisho yake, na Anemu na malisho yake; 74  na kutoka katika kabila la Asheri, Mashali na malisho yake, Abdoni na malisho yake,+ 75  Hukoki na malisho yake, na Rehobu+ na malisho yake; 76  na kutoka katika kabila la Naftali, Kedeshi+ kule Galilaya+ na malisho yake, Hamoni na malisho yake, na Kiriathaimu na malisho yake. 77  Wamerari waliobaki walipewa kutoka katika kabila la Zabuloni,+ Rimono na malisho yake, Tabori na malisho yake; 78  na katika eneo la Yordani kule Yeriko, upande wa mashariki wa Yordani, kutoka katika kabila la Rubeni, walipewa Beseri kule nyikani na malisho yake, Yahazi+ na malisho yake, 79  Kedemothi+ na malisho yake, na Mefaathi na malisho yake; 80  na kutoka katika kabila la Gadi, Ramothi kule Gileadi na malisho yake, Mahanaimu+ na malisho yake, 81  Heshboni+ na malisho yake, na Yazeri+ na malisho yake.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Wana.”
Pia anaitwa Gershoni katika mstari wa 1.
Au “Wazao.”
Au “Wazao.”
Tnn., “lipumzike.”
Tnn., “walitolewa.”
Au “kambi zao zilizozingirwa na kuta.”
Au labda, “jiji hili la,” kulingana na Yos 21:13.
Au “walipewa kwa kura.”
Au labda, “jiji la,” kulingana na Yos 21:21.