Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 7:1-40

  • Wazao wa Isakari (1-5), wa Benjamini (6-12), wa Naftali (13), wa Manase (14-19), wa Efraimu (20-29), na wa Asheri (30-40)

7  Sasa wana wa Isakari walikuwa Tola, Pua, Yashubu, na Shimroni+—wana wanne.  Na wana wa Tola walikuwa Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu, na Shemueli, viongozi wa koo* zao. Wazao wa Tola walikuwa mashujaa hodari, na idadi yao katika siku za Daudi ilikuwa 22,600.  Na wazao* wa Uzi walikuwa Izrahia na wana wa Izrahia: Mikaeli, Obadia, Yoeli, na Ishia—wote watano walikuwa wakuu.*  Na pamoja nao, kulingana na wazao wao, kulingana na koo* zao, kulikuwa na wanajeshi 36,000 katika jeshi lao waliokuwa tayari kwa ajili ya vita, kwa maana walikuwa na wake wengi na wana wengi.  Na ndugu zao wa koo zote za Isakari walikuwa mashujaa hodari 87,000 walioandikishwa katika orodha ya koo.+  Wana wa Benjamini+ walikuwa Bela,+ Bekeri,+ na Yediaeli+—wana watatu.  Na wana wa Bela walikuwa Esboni, Uzi, Uzieli, Yerimothi, na Iri—wana watano—viongozi wa koo zao, mashujaa hodari, na 22,034 walikuwa wameandikishwa katika orodha ya ukoo* wao.+  Na wana wa Bekeri walikuwa Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi, Alemethi—hao wote walikuwa wana wa Bekeri.  Na wale walioandikishwa katika orodha ya ukoo wao kulingana na wazao wao kuhusiana na viongozi wa koo* zao walikuwa mashujaa hodari 20,200. 10  Na wana wa Yediaeli+ walikuwa Bilhani na wana wa Bilhani walikuwa Yeushi, Benjamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi, na Ahishahari. 11  Hao wote walikuwa wana wa Yediaeli, kulingana na viongozi wa koo za mababu zao, mashujaa hodari 17,200 waliokuwa tayari kujiunga na jeshi kwa ajili ya vita. 12  Washupimu na Wahupimu walikuwa wana wa Ire;+ Wahushimu walikuwa wana wa Aheri. 13  Wana wa Naftali+ walikuwa Yahzieli, Guni, Yezeri, na Shalumu—wazao* wa Bilha.+ 14  Wana wa Manase:+ Asrieli, aliyezaliwa na suria wake Msiria. (Suria huyo alimzaa Makiri+ baba ya Gileadi. 15  Makiri alimtafutia mke Hupimu na Shupimu, na dada yake aliitwa Maaka.) Mwana wa pili aliitwa Selofehadi, lakini Selofehadi+ alizaa mabinti.+ 16  Maaka, mke wa Makiri, alizaa mwana na kumwita jina Pereshi; na ndugu yake aliitwa Shereshi; na wanawe walikuwa Ulamu na Rekemu. 17  Na mwana* wa Ulamu alikuwa Bedani. Hao ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase. 18  Na dada yake alikuwa Hamolekethi. Alimzaa Ishodi, Abiezeri, na Mala. 19  Na wana wa Shemida walikuwa Ahiani, Shekemu, Likhi, na Aniamu. 20  Wana wa Efraimu+ walikuwa Shuthela,+ Beredi mwana wa Shuthela, Tahathi mwana wa Beredi, Eleada mwana wa Tahathi, na Tahathi mwana wa Eleada, 21  Zabadi mwana wa Eleada, Shuthela mwana wa Zabadi, Ezeri, na Eleadi. Wanaume wa Gathi+ waliozaliwa nchini waliwaua kwa sababu waliteremka huko kuchukua mifugo yao. 22  Efraimu baba yao aliendelea kuomboleza kwa siku nyingi, na ndugu zake walikuwa wakija kumfariji. 23  Baadaye akalala na mke wake, naye akapata mimba na kuzaa mwana. Lakini akamwita mwana huyo Beria* kwa sababu mama yake alikuwa katika nyumba ya Efraimu wakati wa msiba. 24  Na binti yake alikuwa Sheera, aliyejenga Beth-horoni ya Chini+ na ya Juu+ na Uzen-sheera. 25  Na kulikuwa na Refa mwanawe, Reshefu, Tela mwana wa Reshefu, Tahani mwana wa Tela, 26  Ladani mwana wa Tahani, Amihudi mwana wa Ladani, Elishama mwana wa Amihudi, 27  Nuni mwana wa Elishama, na Yoshua*+ mwana wa Nuni. 28  Walimiliki na kuishi Betheli+ na katika miji yake, na upande wa mashariki, Naarani, na upande wa magharibi, Gezeri na miji yake, na Shekemu* na miji yake, mpaka Aya na miji yake; 29  na kando ya wazao wa Manase, walimiliki Beth-sheani+ na miji yake, Taanaki+ na miji yake, Megido+ na miji yake, na Dori+ na miji yake. Wazao wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi humo. 30  Wana wa Asheri walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, na Beria,+ na dada yao aliitwa Sera.+ 31  Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba ya Birzaithi. 32  Heberi akamzaa Yafleti, Shomeri, na Hothamu, na Shua dada yao. 33  Wana wa Yafleti walikuwa Pasaki, Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio waliokuwa wana wa Yafleti. 34  Wana wa Shemeri* walikuwa Ahi, Roga, Yehuba, na Aramu. 35  Wana wa Helemu* ndugu yake walikuwa Sofa, Imna, Sheleshi, na Amali. 36  Wana wa Sofa walikuwa Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra, 37  Beseri, Hodi, Shama, Shilsha, Ithrani, na Beera. 38  Wana wa Yetheri walikuwa Yefune, Pispa, na Ara. 39  Wana wa Ula walikuwa Ara, Hanieli, na Risia. 40  Hao wote walikuwa wana wa Asheri, viongozi wa koo* zao, watu wa pekee, mashujaa hodari, viongozi wa wakuu; na wanaume wao walioandikishwa jeshini kwa ajili ya vita katika orodha ya koo+ walikuwa 26,000.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “wana.”
Tnn., “viongozi.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “wana.”
Tnn., “wana.”
Maana yake “Wakati wa Msiba.”
Au “Yehoshua,” linalomaanisha “Yehova Ni Wokovu.”
Au labda, “Gaza,” ingawa si jiji la Gaza kule Ufilisti.
Pia anaitwa Shomeri katika mstari wa 32.
Inaelekea ni sawa na “Hothamu” katika mstari wa 32.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.