Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 9:1-44

  • Koo zilizoandikishwa baada ya kurudi kutoka uhamishoni (1-34)

  • Orodha ya wazao wa Sauli yarudiwa (35-44)

9  Waisraeli wote waliandikishwa kulingana na ukoo wao, na koo hizo zimeandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Na watu wa Yuda walipelekwa uhamishoni kule Babiloni kwa sababu hawakuwa waaminifu.+  Baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, na watumishi wa hekaluni*+ walikuwa wakaaji wa kwanza kurudi katika miliki yao kwenye majiji yao.  Na baadhi ya wazao wa Yuda,+ wa Benjamini,+ wa Efraimu, na wa Manase walioishi Yerusalemu walikuwa:  Uthai mwana wa Amihudi mwana wa Omri mwana wa Imri mwana wa Bani, kutoka kwa wazao wa Perezi+ mwana wa Yuda.  Na kutoka kwa wazao wa Washilo, Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.  Na wana wa Zera,+ Yeueli na ndugu zao 690.  Na kutoka kwa wazao wa Benjamini, Salu mwana wa Meshulamu mwana wa Hodavia mwana wa Hasenua,  Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi mwana wa Mikri, na Meshulamu mwana wa Shefatia mwana wa Reueli mwana wa Ibniya.  Na ndugu zao kulingana na ukoo wao walikuwa 956. Wanaume hao wote walikuwa viongozi wa koo zao.* 10  Na kutoka kwa makuhani, kulikuwa na Yedaya, Yehoyaribu, Yakini,+ 11  Azaria mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayothi mwana wa Ahitubu, kiongozi wa nyumba ya* Mungu wa kweli, 12  Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pashuri mwana wa Malkiya, Maasai mwana wa Adieli mwana wa Yahzera mwana wa Meshulamu mwana wa Meshilemithi mwana wa Imeri, 13  na ndugu zao, viongozi wa koo* zao, mashujaa 1,760, wanaume wenye uwezo waliokuwa tayari kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli. 14  Na kutoka kwa Walawi, kulikuwa na Shemaya+ mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia kutoka kwa wazao wa Merari; 15  na Bakbakari, Hereshi, Galali, Matania mwana wa Mika mwana wa Zikri mwana wa Asafu, 16  Obadia mwana wa Shemaya mwana wa Galali mwana wa Yeduthuni, na Berekia mwana wa Asa mwana wa Elkana, aliyekuwa akiishi katika vijiji vya Wanetofa.+ 17  Walinzi wa malango+ walikuwa Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani, na ndugu yao Shalumu alikuwa kiongozi, 18  na kufikia wakati huo alikuwa katika lango la mfalme upande wa mashariki.+ Hao walikuwa walinzi wa malango wa kambi za Walawi. 19  Na Shalumu mwana wa Kore mwana wa Ebiasafu mwana wa Kora, na ndugu zake wa ukoo wake,* Wakora, walisimamia majukumu ya utumishi wa walinzi wa milango ya hema, na baba zao walikuwa wakisimamia kambi ya Yehova wakiwa walinzi wa njia ya kuingilia. 20  Finehasi+ mwana wa Eleazari+ ndiye aliyekuwa kiongozi wao zamani; Yehova alikuwa pamoja naye. 21  Zekaria+ mwana wa Meshelemia alikuwa mlinzi wa lango la kuingia katika hema la mkutano. 22  Wote waliochaguliwa kuwa walinzi kwenye vizingiti walikuwa 212. Waliishi katika vijiji vyao kulingana na orodha ya ukoo wao.+ Daudi na Samweli yule mwonaji+ waliwaweka katika wadhifa wa kuaminiwa. 23  Watu hao pamoja na wana wao walisimamia utumishi wa ulinzi wa malango ya nyumba ya Yehova,+ nyumba ya hema. 24  Walinzi wa malango walikuwa pande zote nne—mashariki, magharibi, kaskazini, na kusini.+ 25  Mara kwa mara, ndugu zao walipaswa kuja kwa siku saba kutoka katika vijiji vyao ili kutumikia pamoja nao. 26  Kulikuwa na walinzi wakuu* wanne waliowekwa katika wadhifa huo wa kuaminiwa. Walikuwa Walawi, nao walisimamia vyumba* na hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+ 27  Walikuwa wakikesha usiku kucha katika vituo vyao kuzunguka nyumba yote ya Mungu wa kweli, kwa maana walishughulikia utumishi wa ulinzi na kutunza ufunguo, nao walikuwa wakifungua nyumba hiyo asubuhi baada ya asubuhi. 28  Baadhi yao walisimamia vyombo+ vya utumishi; walikuwa wakivihesabu vilipokuwa vikiingizwa ndani na kuvihesabu vilipotolewa nje. 29  Baadhi yao waliwekwa kusimamia vyombo, kusimamia vyombo vyote vitakatifu,+ na kusimamia unga laini,+ divai,+ mafuta,+ ubani,+ na mafuta ya zeri.+ 30  Baadhi ya wana wa makuhani walichanganya manukato ya mafuta ya zeri. 31  Na Matithia mmoja wa Walawi, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, Mkora, alipewa wadhifa wa kuaminiwa wa kusimamia vitu vilivyookwa kwenye vikaangio.+ 32  Baadhi ya ndugu zao Wakohathi walisimamia mikate ya tabaka,*+ waliitayarisha kila sabato.+ 33  Hao walikuwa waimbaji, viongozi wa koo* za Walawi katika vyumba* vya nyumba hiyo, wale ambao hawakupewa kazi nyingine; kwa maana usiku na mchana walikuwa na wajibu wa kushika zamu zao. 34  Hao walikuwa viongozi wa koo* za Walawi kulingana na ukoo wao, viongozi. Waliishi Yerusalemu. 35  Yeieli, baba ya Gibeoni, aliishi Gibeoni.+ Mke wake aliitwa Maaka. 36  Na mwana wake mzaliwa wa kwanza aliitwa Abdoni, kisha Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu, 37  Gedori, Ahio, Zekaria, na Miklothi. 38  Miklothi alimzaa Shimeamu. Na wote waliishi karibu na ndugu zao kule Yerusalemu, pamoja na ndugu zao wengine. 39  Neri+ akamzaa Kishi; Kishi akamzaa Sauli;+ Sauli akamzaa Yonathani,+ Malki-shua,+ Abinadabu,+ na Eshbaali. 40  Na mwana wa Yonathani aliitwa Merib-baali.+ Merib-baali akamzaa Mika.+ 41  Na wana wa Mika walikuwa Pithoni, Meleki, Tahrea, na Ahazi. 42  Ahazi akamzaa Yara; Yara akamzaa Alemethi, Azmavethi, na Zimri. Zimri akamzaa Mosa. 43  Mosa akamzaa Binea na Refaya mwanawe, Refaya akamzaa Eleasa, Eleasa akamzaa Aseli. 44  Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia, na Hanani. Hao ndio waliokuwa wana wa Aseli.

Maelezo ya Chini

Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Tnn., “vichwa vya akina baba kwa ajili ya nyumba za baba zao.”
Au “hekalu la.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “vyumba vya kulia chakula.”
Tnn., “wenye uwezo.”
Yaani, mikate ya wonyesho.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “vyumba vya kulia chakula.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.