Barua ya Kwanza ya Petro 1:1-25

  • Salamu (1, 2)

  • Kuzaliwa upya kwenye tumaini lililo hai (3-12)

  • Iweni watakatifu kama watoto watiifu (13-25)

1  Petro, mtume+ wa Yesu Kristo, kwa wakaaji wa muda waliotawanyika katika Ponto, Galatia, Kapadokia,+ Asia, na Bithinia, kwa wale waliochaguliwa  kulingana na ujuzi wa awali wa Mungu aliye Baba,+ kwa kutakaswa kwa roho,+ kusudi wawe watiifu na kunyunyiziwa damu ya Yesu Kristo:+ Na mwongezewe fadhili zisizostahiliwa na amani.  Asifiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwa maana kulingana na rehema yake kubwa alituzaa sisi upya+ kwenye tumaini lililo hai+ kupitia ufufuo wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu,+  kwenye urithi usioharibika na usio na unajisi na usiofifia.+ Urithi huo umewekwa akiba mbinguni kwa ajili yenu,+  ninyi mnaolindwa kwa nguvu za Mungu kupitia imani kwa ajili ya wokovu ulio tayari kufunuliwa katika kipindi cha mwisho cha wakati.  Kwa sababu ya jambo hilo mnashangilia sana, ingawa kwa muda mfupi, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu mbalimbali,+  ili sifa iliyojaribiwa ya imani yenu,+ iliyo na thamani kubwa zaidi kuliko dhahabu ambayo huharibika ijapokuwa inajaribiwa* kwa moto, ipatikane kuwa sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo wa Yesu Kristo.+  Mnampenda ingawa hamkumwona kamwe. Ijapokuwa hammwoni sasa, bado mnaonyesha imani katika yeye na mnashangilia sana kwa shangwe isiyoelezeka na iliyotukuka,  huku mkifikia lengo la* imani yenu, wokovu wenu.*+ 10  Kuhusu wokovu huu, manabii waliotoa unabii kuhusu fadhili zisizostahiliwa zilizokusudiwa kwa ajili yenu, walifanya uchunguzi kwa bidii na kutafuta kwa uangalifu.+ 11  Waliendelea kuchunguza wakati hususa au majira ambayo roho iliyokuwa ndani yao ilikuwa ikionyesha kumhusu Kristo+ ilipokuwa ikitoa ushahidi mapema kuhusu mateso ya Kristo+ na kuhusu utukufu ambao ungefuata. 12  Walifunuliwa kwamba hawakuwa wakijihudumia wenyewe, bali walikuwa wakiwahudumia ninyi, kwa mambo ambayo sasa mmetangaziwa na wale ambao waliwatangazia habari njema kwa roho takatifu iliyotumwa kutoka mbinguni.+ Malaika wanatamani kuchungulia ndani ya mambo hayo. 13  Kwa hiyo kazeni akili zenu kwa ajili ya utendaji;+ tunzeni akili zenu kwa ukamili;+ kazeni tumaini lenu juu ya fadhili zisizostahiliwa zitakazoletwa kwenu wakati wa ufunuo wa Yesu Kristo. 14  Kama watoto watiifu, acheni kufinyangwa* na tamaa mlizokuwa nazo zamani katika hali yenu ya kutojua, 15  lakini iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote kama Yule Mtakatifu aliyewaita ninyi,+ 16  kwa maana imeandikwa: “Lazima muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.”+ 17  Na ikiwa mnamwitia Baba ambaye huhukumu bila ubaguzi+ kulingana na matendo ya kila mmoja, jiendesheni kwa kuogopa+ wakati ambao ninyi ni wakaaji wa muda. 18  Kwa maana mnajua kwamba mliwekwa huru*+ kutoka kwenye mwenendo wenu usio na faida ambao mlipokea kutoka kwa mababu zenu,* si kwa vitu vyenye kuharibika, kwa fedha au dhahabu, 19  bali ilikuwa kwa damu yenye thamani,+ kama ile ya mwanakondoo asiye na dosari+ na asiye na doa, ile ya Kristo.+ 20  Ni kweli, yeye alijulikana mapema kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu,+ lakini alifunuliwa mwishoni mwa nyakati kwa ajili yenu.+ 21  Kupitia yeye mnamwamini Mungu,+ yule aliyemfufua kutoka kwa wafu+ na kumpa utukufu,+ ili imani na tumaini lenu liwe katika Mungu. 22  Sasa kwa sababu mmejitakasa wenyewe* kwa kuwa watiifu kwa ile kweli na hivyo kuwa na upendo wa kindugu+ bila unafiki, pendaneni sana kutoka moyoni.+ 23  Kwa maana mmezaliwa upya,+ si kupitia mbegu* yenye kuharibika, bali kupitia ile isiyoharibika,+ kupitia neno la Mungu aliye hai na anayedumu.+ 24  Kwa maana “wote wenye mwili ni kama nyasi, na utukufu wao wote ni kama ua la shambani; nyasi hukauka, na ua huanguka, 25  bali neno la Yehova* linadumu milele.”+ Na “neno” hilo ni habari njema mliyotangaziwa.+

Maelezo ya Chini

Au “inasafishwa.”
Au “mradi wa.”
Au “wokovu wa nafsi zenu.”
Au “kufanyizwa kulingana.”
Tnn., “mlilipiwa fidia; mlikombolewa.”
Au “kutokana na desturi.”
Au “mmezitakasa nafsi zenu.”
Yaani, mbegu inayoweza kuzaa, au inayotokeza matunda.