Kitabu cha Kwanza cha Samweli 27:1-12

  • Wafilisti wampa Daudi Siklagi (1-12)

27  Hata hivyo, Daudi akasema moyoni mwake: “Siku moja mkono wa Sauli utaniua. Jambo bora la kufanya ni kukimbilia+ nchi ya Wafilisti; halafu Sauli atakata tamaa ya kunitafuta katika eneo lote la Israeli,+ nami nitaponyoka kutoka mkononi mwake.”  Basi Daudi akaondoka pamoja na wanaume 600+ waliokuwa naye, akavuka kwenda kwa Akishi+ mwana wa Maoki, mfalme wa Gathi.  Daudi na wanaume wake wakakaa na Akishi huko Gathi, kila mwanamume na familia yake. Daudi alikuwa na wake zake wawili, Ahinoamu+ wa Yezreeli na Abigaili+ Mkarmeli, mjane wa Nabali.  Sauli alipoambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbia kwenda Gathi, aliacha kumtafuta.+  Ndipo Daudi akamwambia Akishi: “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, naomba unipe mahali katika mojawapo ya majiji ya mashambani, ili niishi huko. Kwa nini mimi mtumishi wako niishi pamoja nawe katika jiji hili la kifalme?”  Basi Akishi akampa Siklagi+ siku hiyo. Ndiyo sababu tangu siku hiyo Siklagi limekuwa jiji la wafalme wa Yuda.  Daudi aliishi katika eneo la mashambani la Wafilisti kwa muda wa mwaka mmoja na miezi minne.+  Daudi alikuwa akipanda pamoja na wanaume wake kuwavamia Wageshuri,+ Wagirzi, na Waamaleki,+ kwa maana walikuwa wakikaa katika nchi iliyoanzia Telamu mpaka Shuri+ na kushuka mpaka nchi ya Misri.  Daudi alipokuwa akiishambulia nchi, hakumwacha hai mwanamume wala mwanamke yeyote,+ bali alichukua kondoo, ng’ombe, punda, ngamia, na mavazi, kisha alirudi kwa Akishi. 10  Na Akishi alipokuwa akimuuliza: “Ulivamia wapi leo?” Daudi alimjibu: “Upande wa kusini wa* Yuda”+ au “Upande wa kusini wa Wayerahmeeli”+ au “Upande wa kusini wa Wakeni.”+ 11  Daudi hakumwacha hai mwanamume au mwanamke yeyote ili wasiletwe Gathi, kwa kuwa alisema: “Wasije wakawaambia habari zetu wakisema, ‘Hivi ndivyo Daudi alivyofanya.’” (Alizoea kufanya hivyo muda wote alioishi katika eneo la mashambani la Wafilisti.) 12  Kwa hiyo Akishi akamwamini Daudi akisema moyoni mwake: “Bila shaka ananuka miongoni mwa watu wake wa Israeli, kwa hiyo atakuwa mtumishi wangu sikuzote.”

Maelezo ya Chini

Au “Dhidi ya Negebu ya.”