Kitabu cha Kwanza cha Samweli 28:1-25

  • Sauli amtembelea mtu anayewasiliana na roho waovu kule En-dori (1-25)

28  Siku hizo Wafilisti walikusanya majeshi yao kwenda kupigana vita na Waisraeli.+ Basi Akishi akamwambia Daudi: “Bila shaka unajua kwamba wewe na wanaume wako mtaenda pamoja nami vitani.”+  Kwa hiyo Daudi akamwambia Akishi: “Kwa hakika unajua jambo ambalo mimi mtumishi wako nitafanya.” Akishi akamwambia Daudi: “Ndiyo sababu nitakuweka kuwa mlinzi wangu wa kudumu.”*+  Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, na Waisraeli wote walikuwa wamemwombolezea na kumzika katika jiji lake mwenyewe la Rama.+ Naye Sauli alikuwa amewaondoa nchini watu wanaowasiliana na roho na pia wabashiri.+  Wafilisti wakakusanyika na kwenda kupiga kambi Shunemu.+ Basi Sauli akawakusanya Waisraeli wote, nao wakapiga kambi Gilboa.+  Sauli alipoona kambi ya Wafilisti, akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana.+  Ingawa Sauli alikuwa akimwomba Yehova ushauri,+ Yehova hakumjibu kamwe, iwe ni katika ndoto au kwa Urimu+ au kupitia manabii.  Hatimaye Sauli akawaambia watumishi wake: “Nitafutieni mwanamke anayewasiliana na roho,+ nitaenda kwake kumwomba ushauri.” Watumishi wake wakamwambia: “Tazama! Kuna mwanamke anayewasiliana na roho kule En-dori.”+  Kwa hiyo Sauli akaficha sura yake, akavaa mavazi mengine na kwenda kwa mwanamke huyo usiku akiwa na wanaume wake wawili. Akasema: “Tafadhali, nifanyie uaguzi* kwa kuwasiliana na roho,+ nipandishie yule nitakayekutajia.”  Hata hivyo, mwanamke huyo akamwambia: “Unajua vizuri mambo ambayo Sauli alifanya, jinsi alivyowaondoa nchini watu wanaowasiliana na roho na pia wabashiri.+ Kwa nini basi unajaribu kunitega ili niuawe?”+ 10  Ndipo Sauli akamwapia kwa jina la Yehova, akisema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, hutakuwa na hatia yoyote kuhusu jambo hili!” 11  Basi mwanamke huyo akamuuliza: “Nikupandishie nani?” Akajibu: “Nipandishie Samweli.” 12  Mwanamke huyo alipomwona “Samweli,”*+ akapiga kelele kwa sauti yake yote na kumwambia Sauli: “Kwa nini ulinidanganya? Wewe ni Sauli!” 13  Mfalme akamwambia: “Usiogope, lakini unaona nini?” Mwanamke huyo akamjibu Sauli: “Ninaona mtu fulani kama mungu akipanda kutoka duniani.” 14  Mara moja Sauli akamuuliza mwanamke huyo: “Yukoje?” akamwambia: “Ni mwanamume mzee anayepanda, amevaa joho lisilo na mikono.”+ Ndipo Sauli akatambua kwamba ni “Samweli,” naye akainama chini kifudifudi na kusujudu. 15  Kisha “Samweli” akamuuliza Sauli: “Kwa nini umenisumbua kwa kufanya nipandishwe?” Sauli akamjibu: “Niko katika taabu kubwa. Wafilisti wanapigana nami, na Mungu ameniacha, hanijibu tena, iwe ni kupitia manabii au katika ndoto;+ ndiyo sababu nimekuita uniambie ninalopaswa kufanya.”+ 16  “Samweli” akamuuliza: “Kwa nini unaniomba ushauri wakati ambapo Yehova amekuacha+ na kuwa adui yako? 17  Yehova atajifanyia mwenyewe yale aliyotabiri kupitia mimi: Yehova ataurarua ufalme kutoka mikononi mwako na kumpa mwenzako, Daudi.+ 18  Kwa sababu hukuitii sauti ya Yehova, nawe hukutekeleza hasira yake kali dhidi ya Waamaleki,+ ndiyo sababu Yehova anakutendea mambo haya leo. 19  Pia, Yehova atakutia wewe pamoja na Waisraeli mikononi mwa Wafilisti,+ na kesho wewe+ na wana wako+ mtakuwa pamoja nami. Yehova atalitia pia jeshi la Israeli mikononi mwa Wafilisti.”+ 20  Papo hapo Sauli akaanguka chini akiwa amenyooka mwili mzima naye akaogopa sana kwa sababu ya maneno ya “Samweli.” Nguvu zikamwishia, kwa sababu hakuwa amekula chakula mchana wote na usiku kucha. 21  Mwanamke huyo alipomkaribia Sauli na kuona kwamba ana wasiwasi mwingi, akamwambia: “Mimi kijakazi wako nimetii jambo ulilosema, na nimehatarisha uhai wangu*+ kwa kufanya uliloniambia nifanye. 22  Sasa, tafadhali, sikiliza maneno ninayotaka kukwambia mimi mtumishi wako. Acha nikuandalie kipande cha mkate, ule ili upate nguvu za kuendelea na safari.” 23  Lakini akakataa na kusema: “Sitakula.” Hata hivyo, watumishi wake na pia mwanamke huyo wakaendelea kumsihi ale. Mwishowe akawasikiliza, akainuka kutoka ardhini na kuketi kitandani. 24  Mwanamke huyo alikuwa na ndama aliyenona nyumbani mwake, basi akamchinja* haraka, akachukua unga, akaukanda na kuoka mikate isiyo na chachu. 25  Akamwandalia Sauli na watumishi wake, nao wakala. Kisha wakaondoka na kwenda zao usiku huo.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuwa mlinzi wa kichwa changu siku zote.”
Au “nibashirie.”
Au “mtu aliyeonekana kama Samweli.”
Au “nimetia nafsi yangu mikononi mwangu.”
Au “akamtoa dhabihu.”