Kitabu cha Kwanza cha Samweli 31:1-13

  • Kifo cha Sauli na wanawe watatu (1-13)

31  Sasa Wafilisti walikuwa wakipigana na Waisraeli.+ Na wanaume wa Israeli wakawakimbia Wafilisti, na wengi wakauawa kwenye Mlima Gilboa.+  Wafilisti wakamkaribia sana Sauli na wanawe, nao wakamuua Yonathani,+ Abinadabu, na Malki-shua, wana wa Sauli.+  Vita vikawa vikali sana dhidi ya Sauli, na wapiga mishale wakampata na kumjeruhi vibaya.+  Ndipo Sauli akamwambia mtu aliyembebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije kunichoma kwa upanga na kunitendea kikatili.”* Lakini mtu huyo aliyembebea silaha hakutaka kufanya hivyo, kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga na kuuangukia.+  Mtu aliyembebea silaha alipoona kwamba Sauli amekufa,+ yeye pia akauangukia upanga wake mwenyewe, akafa pamoja naye.  Basi Sauli, wanawe watatu, mtu aliyembebea silaha, na wanaume wake wote wakafa pamoja siku hiyo.+  Watu wa Israeli waliokuwa katika eneo la bondeni na katika eneo la Yordani walipoona kwamba wanaume wa Israeli wamekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaanza kuyaacha majiji na kukimbia;+ kisha Wafilisti wakaja na kukaa humo.  Siku iliyofuata, Wafilisti walipokuja kuwavua waliouawa vitu walivyokuwa navyo, walimkuta Sauli na wanawe watatu wakiwa wameanguka kwenye Mlima Gilboa.+  Basi wakamkata kichwa na kumvua silaha zake na kutuma ujumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili habari+ zienezwe katika nyumba za* sanamu zao+ na miongoni mwa watu. 10  Kisha wakaweka silaha zake katika nyumba ya sanamu za Ashtorethi na kuitundika maiti yake kwenye ukuta wa Beth-shani.+ 11  Wakaaji wa Yabeshi-gileadi+ waliposikia mambo ambayo Wafilisti walikuwa wamemtendea Sauli, 12  mashujaa wote wakaondoka na kusafiri usiku kucha, wakaondoa maiti za Sauli na wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-shani. Wakarudi Yabeshi na kuzichoma moto huko. 13  Kisha wakachukua mifupa yao+ na kuizika chini ya mti wa mwesheli huko Yabeshi,+ nao wakafunga kwa siku saba.

Maelezo ya Chini

Au “na kunitesa.”
Au “mahekalu ya.”