Barua ya Kwanza kwa Timotheo 4:1-16

  • Onyo dhidi ya mafundisho ya roho waovu (1-5)

  • Jinsi ya kuwa mhudumu mzuri wa Kristo (6-10)

    • Tofauti kati ya mazoezi ya kimwili na ujitoaji-kimungu (8)

  • Angalia kufundisha kwako (11-16)

4  Hata hivyo, neno lililoongozwa na roho linasema* wazi kwamba wakati ujao watu fulani wataiacha imani, wakisikiliza maneno ya uwongo yaliyoongozwa na roho waovu*+ na mafundisho ya roho waovu,  kupitia unafiki wa watu wanaosema uwongo,+ ambao dhamiri zao zimetiwa alama kama kwa chuma cha moto.  Wanakataza watu kufunga ndoa+ na kuwaamuru wasile vyakula+ ambavyo Mungu aliumba viliwe+ kwa shukrani na watu wenye imani+ na wanaoijua kweli kwa usahihi.  Kwa sababu kila kiumbe cha Mungu ni kizuri,+ na hakuna kitu kinachopaswa kukataliwa+ ikiwa kinapokewa kwa shukrani,  kwa maana kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kutolewa sala.  Ukiwapa akina ndugu mashauri haya utakuwa mhudumu mzuri wa Kristo Yesu, aliyelishwa maneno ya imani na fundisho bora ambalo umefuata kwa makini.+  Lakini kataa hadithi za uwongo zisizo na heshima,+ kama zile zinazosimuliwa na wanawake wazee. Badala yake, endelea kujizoeza ukiwa na lengo la ujitoaji-kimungu.*  Kwa maana mazoezi ya kimwili ni yenye faida kidogo, lakini ujitoaji-kimungu* una faida katika mambo yote, kwa kuwa una ahadi ya uhai wa sasa na ule utakaokuja.+  Maneno hayo ni yenye kutegemeka na yanastahili kukubaliwa kabisa. 10  Hiyo ndiyo sababu tunafanya kazi kwa bidii na kujitahidi,+ kwa sababu tumemtumaini Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi+ wa watu wa namna zote,+ hasa wa walio waaminifu. 11  Endelea kutoa amri hizi na kuzifundisha. 12  Usiruhusu kamwe mtu yeyote audharau ujana wako. Badala yake, uwe mfano mzuri kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, na katika usafi wa kiadili. 13  Mpaka nitakapokuja, endelea kujitahidi kusoma mbele ya watu,+ kuhimiza,* na kufundisha. 14  Usipuuze zawadi uliyo nayo uliyopokea kupitia unabii, baraza la wazee lilipoweka mikono juu yako.+ 15  Tafakari* mambo haya; zama katika hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote. 16  Jiangalie daima wewe mwenyewe na kufundisha kwako.+ Endelea kufanya mambo haya, kwa maana ukifanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaokusikiliza pia.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “roho inasema.”
Tnn., “roho wadanganyifu.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “kutia moyo.”
Au “Fikiria kwa makini.”