Barua ya Kwanza kwa Timotheo 5:1-25

  • Jinsi ya kuwatendea vijana na wazee (1, 2)

  • Kuwasaidia wajane (3-16)

    • Kuandaa mahitaji ya watu wa nyumba yako (8)

  • Kuheshimu wazee wenye bidii (17-25)

    • “Divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako” (23)

5  Usimkosoe kwa ukali mwanamume mzee.+ Badala yake, msihi kama baba, wanaume vijana kama ndugu,  wanawake wazee kama mama, na wanawake vijana kama dada, kwa usafi wote wa kiadili.  Wajali* wajane ambao ni wajane kwelikweli.*+  Lakini ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, wanapaswa kwanza kujifunza ujitoaji-kimungu* katika nyumba zao wenyewe+ na kuwalipa wazazi wao na wazazi wa wazazi wao kinachowastahili,+ kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.+  Basi mwanamke ambaye ni mjane kwelikweli na aliye maskini anamtumaini Mungu+ naye huendelea kusali na kutoa dua usiku na mchana.+  Lakini mwanamke anayefuatilia tamaa za mwili amekufa ingawa yuko hai.  Basi endelea kuwapa maagizo haya,* ili wasiwe na lawama.  Hakika ikiwa yeyote hawaandalii mahitaji watu wake mwenyewe, hasa watu wa nyumba yake, ameikana imani naye ni mbaya kuliko mtu asiye na imani.+  Mweke kwenye orodha mjane mwenye umri usiopungua miaka 60, ikiwa alikuwa mke wa mume mmoja, 10  alijulikana kwa kutenda mema,+ alilea watoto,+ alikuwa akiwakaribisha wageni,*+ aliiosha miguu ya watakatifu,+ aliwasaidia watu wenye taabu,+ na akajitolea kufanya kila kazi njema. 11  Kwa upande mwingine, usiwaweke kwenye orodha wajane wenye umri mdogo, kwa maana tamaa zao za ngono zinapokuja kati yao na Kristo, wao hutamani kuolewa. 12  Nao watahukumiwa kwa sababu wameacha imani waliyoonyesha mwanzoni.* 13  Vilevile wanakuwa na tabia ya kupoteza muda, wakizunguka kutoka nyumba moja hadi nyingine; ndiyo, hawapotezi muda tu, bali pia wanapiga porojo na kujiingiza katika mambo ya watu wengine,+ wakiongea kuhusu mambo ambayo hawapaswi. 14  Kwa hiyo, ninatamani wanawake wajane walio na umri mdogo waolewe,+ wazae watoto,+ wasimamie nyumba, ili wasimpe mpinzani sababu ya kukosoa. 15  Kwa kweli, tayari baadhi yao wamepotoshwa na kumfuata Shetani. 16  Ikiwa mwanamke yeyote mwamini ana watu wa ukoo ambao ni wajane, inafaa awasaidie ili kutaniko lisibebe mzigo huo, na hivyo liwasaidie wale walio wajane kwelikweli.*+ 17  Wazee wanaosimamia kwa njia nzuri+ wanastahili heshima mara mbili,+ hasa wale wanaofanya kazi kwa bidii katika kusema na kufundisha.+ 18  Kwa maana andiko linasema, “Hupaswi kumfunga kinywa ng’ombe dume anapopura nafaka,”+ pia, “Mfanyakazi anastahili mshahara wake.”+ 19  Usikubali mashtaka dhidi ya mwanamume mzee,* isipokuwa kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.+ 20  Wakaripie+ hadharani watu wanaozoea kutenda dhambi,+ ili liwe onyo kwa wengine.* 21  Ninakuagiza kwa uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu na malaika waliochaguliwa, ufuate maagizo haya bila kubagua wala kupendelea.+ 22  Usiharakishe kamwe kuweka mikono yako juu ya* mwanamume yeyote;+ wala usishiriki dhambi za wengine; endelea kuwa safi. 23  Usiendelee kunywa maji,* bali unywe divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako na ugonjwa wako wa mara kwa mara. 24  Dhambi za watu fulani hujulikana hadharani, na hivyo wanahukumiwa moja kwa moja, lakini dhambi za watu wengine hujulikana baadaye.+ 25  Vivyo hivyo, matendo mema hujulikana hadharani+ na hata yale yasiyojulikana hayawezi kuendelea kufichwa.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Waheshimu.”
Au “wajane maskini”; yaani, wasio na mtu wa kuwasaidia.
Angalia Kamusi.
Au “amri hizi.”
Au “alikuwa mkarimu.”
Au “ahadi waliyotoa mwanzoni.”
Au “wajane maskini”; yaani, wasio na mtu wa kuwasaidia.
Au “mzee.”
Tnn., “ili wengine waogope.”
Yaani, usimweke rasmi mtu yeyote haraka haraka.
Au “Usinywe maji tu.”