Kitabu cha Kwanza cha Wafalme 3:1-28

3  Sulemani alifanya mapatano ya ndoa na Farao mfalme wa Misri. Alimwoa* binti ya Farao+ na kumleta katika Jiji la Daudi+ mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe,+ na nyumba ya Yehova,+ na ukuta kuzunguka Yerusalemu.+  Lakini bado watu walikuwa wakitoa dhabihu mahali pa juu,+ kwa maana kufikia wakati huo nyumba haikuwa imejengwa kwa ajili ya jina la Yehova.+  Sulemani akaendelea kumpenda Yehova kwa kutembea katika sheria za Daudi baba yake, ila tu alikuwa akitoa dhabihu na kufanya matoleo yafuke moshi mahali pa juu.+  Mfalme alienda Gibeoni kutoa dhabihu huko, kwa maana ndipo palipokuwa mahali maarufu* zaidi pa juu.+ Sulemani alitoa dhabihu 1,000 za kuteketezwa juu ya madhabahu hiyo.+  Huko Gibeoni, Yehova alimtokea Sulemani katika ndoto usiku na kumwambia: “Niombe unachotaka nikupe.”+  Basi Sulemani akasema: “Umemtendea mtumishi wako Daudi baba yangu kwa upendo mwingi mshikamanifu alipokuwa akitembea mbele zako kwa uaminifu na kwa uadilifu na kwa unyoofu wa moyo. Umeendelea kumtendea kwa upendo huo mwingi mshikamanifu mpaka leo hii kwa kumpa mwana aketi kwenye kiti chake cha ufalme.+  Na sasa, Yehova Mungu wangu, umeniweka mimi mtumishi wako niwe mfalme baada ya Daudi baba yangu, ingawa mimi ni kijana* tu na sina uzoefu.*+  Mimi mtumishi wako ni miongoni mwa watu wako uliowachagua,+ watu wengi sana hivi kwamba hawawezi kuhesabiwa wala idadi yao kujulikana.  Basi nipe mimi mtumishi wako moyo mtiifu ili niwahukumu watu wako,+ nitofautishe mema na mabaya,+ kwa sababu ni nani anayeweza kuwahukumu watu hawa wako ambao ni wengi sana?”* 10  Ombi hilo la Sulemani lilimpendeza Yehova.+ 11  Basi Mungu akamwambia: “Kwa kuwa umeomba jambo hili, nawe hukujiombea maisha marefu* wala utajiri wala kuomba maadui wako wafe, lakini uliomba uelewaji wa kusikiliza kesi,+ 12  nitafanya uliloomba.+ Nitakupa moyo wenye hekima na uelewaji,+ hivi kwamba kama vile ambavyo hajawahi kamwe kuwapo mtu mwingine kama wewe kabla yako, hatawahi kamwe kuwapo mtu mwingine kama wewe baada yako.+ 13  Isitoshe, nitakupa vitu ambavyo hukuomba,+ utajiri na utukufu,+ hivi kwamba hatakuwapo mfalme mwingine kama wewe katika maisha yako yote.*+ 14  Nawe ukitembea katika njia zangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama Daudi baba yako alivyotembea,+ nitakupa pia maisha marefu.”*+ 15  Sulemani alipoamka, aligundua kwamba ilikuwa ndoto. Kisha akaenda Yerusalemu, akasimama mbele ya sanduku la agano la Yehova, akatoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika+ na kuwaandalia karamu watumishi wake wote. 16  Wakati huo makahaba wawili wakaja kwa mfalme na kusimama mbele yake. 17  Mwanamke wa kwanza akasema: “Tafadhali, bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi katika nyumba moja, nami nilizaa mtoto alipokuwa nyumbani. 18  Siku ya tatu baada ya mimi kuzaa mtoto, mwanamke huyu pia alizaa mtoto. Tulikuwa pamoja, sisi wawili tu; hapakuwa na mtu mwingine yeyote nyumbani. 19  Usiku, mwana wa mwanamke huyu akafa, kwa sababu alimlalia. 20  Basi akaamka katikati ya usiku, akamchukua mwanangu kutoka kando yangu mimi kijakazi wako nilipokuwa nimelala usingizi, akamlaza mikononi mwake,* kisha akamlaza mwana wake mfu mikononi mwangu. 21  Nilipoamka asubuhi ili kumnyonyesha mwanangu, nikaona amekufa. Kwa hiyo nikamchunguza kwa makini, nikagundua kwamba hakuwa mwanangu niliyemzaa.” 22  Lakini mwanamke huyo mwingine akasema: “Hapana, aliye hai ni mwanangu na aliyekufa ndiye mwanao!” Lakini mwanamke wa kwanza aliendelea kusema: “Hapana, aliyekufa ndiye mwanao, na mwanangu ndiye aliye hai.” Hivyo ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme. 23  Mwishowe mfalme akasema: “Huyu anasema, ‘Huyu aliye hai ni mwanangu, aliyekufa ni mwanao!’ na huyu anasema, ‘Hapana, aliyekufa ni mwanao, aliye hai ni mwanangu!’” 24  Mfalme akasema: “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga. 25  Kisha mfalme akasema: “Mkateni vipande viwili mtoto aliye hai, mpeni mwanamke mmoja nusu moja na nusu nyingine mpeni mwingine.” 26  Mara moja mwanamke ambaye ni mama ya mtoto aliye hai akamsihi mfalme, kwa maana alishikwa na huruma kwa ajili ya mwanawe. Akasema: “Tafadhali, bwana wangu! Mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue kamwe.” Lakini yule mwanamke mwingine alikuwa akisema: “Hatakuwa wako wala hatakuwa wangu. Acha wamkate vipande viwili!” 27  Ndipo mfalme akasema: “Mpeni mwanamke wa kwanza mtoto aliye hai! Msimuue kamwe, kwa maana yeye ndiye mama yake.” 28  Kwa hiyo Waisraeli wote wakasikia kuhusu uamuzi uliofanywa na mfalme, nao wakamwogopa mfalme,+ kwa maana waliona kwamba alikuwa na hekima ya Mungu katika kutekeleza haki.+

Maelezo ya Chini

Au “Alimchukua.”
Tnn., “pakuu.”
Au “mvulana mdogo.”
Tnn., “na sijui kutoka nje na kuingia ndani.”
Au labda, “wagumu.” Tnn., “wazito.”
Tnn., “siku nyingi.”
Tnn., “siku zako zote.”
Tnn., “nitarefusha siku zako.”
Tnn., “kifuani pake.”