Kitabu cha Kwanza cha Wafalme 6:1-38

  • Sulemani ajenga hekalu (1-38)

    • Chumba cha ndani zaidi (19-22)

    • Makerubi (23-28)

    • Michongo, milango, ua wa ndani (29-36)

    • Hekalu lakamilishwa kwa muda wa miaka saba hivi (37, 38)

6  Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli* kutoka katika nchi ya Misri,+ mwaka wa nne baada ya Sulemani kuwekwa kuwa mfalme wa Israeli, mwezi wa Zivu*+ (yaani, mwezi wa pili), Sulemani alianza kujenga nyumba ya Yehova.*+  Nyumba ambayo Mfalme Sulemani alimjengea Yehova ilikuwa na urefu wa mikono 60,* upana wa mikono 20, na kimo cha mikono 30.+  Ukumbi+ wa mbele wa hekalu* ulikuwa na urefu* wa mikono 20, nao ulilingana na upana wa nyumba. Ulikuwa na kina cha mikono kumi kuanzia mbele ya nyumba.  Aliitengenezea nyumba hiyo madirisha yenye viunzi ambavyo ukubwa wake ulipungua kutoka nje kwenda ndani.+  Pia, alijenga jengo la kando lililokaribiana na ukuta wa nyumba hiyo; jengo hilo lilizunguka kuta za nyumba hiyo, kuta za hekalu* na za chumba cha ndani zaidi,+ naye akajenga vyumba vya pembeni kuzunguka pande zote.+  Ghorofa ya chini ya vyumba hivyo vya pembeni ilikuwa na upana wa mikono mitano, ghorofa ya katikati ilikuwa na upana wa mikono sita, na ghorofa ya tatu ilikuwa na upana wa mikono saba, kwa maana aliacha sehemu zilizoingia ndani ukutani kuzunguka nyumba yote, ili kitu chochote kisifungwe kwenye kuta za nyumba hiyo.+  Nyumba hiyo ilijengwa kwa mawe ya machimboni ambayo tayari yalikuwa yamechongwa,+ hivi kwamba hakuna nyundo wala mashoka wala kifaa chochote cha chuma kilichosikika katika nyumba hiyo ilipokuwa ikijengwa.  Mlango wa ghorofa ya chini ulikuwa upande wa kusini* wa nyumba hiyo,+ na ngazi iliyopindapinda ilielekea kwenye ghorofa ya katikati, na kutoka ghorofa ya katikati mpaka ghorofa ya tatu.  Aliendelea kujenga nyumba hiyo na kuikamilisha,+ akaifunika nyumba hiyo kwa maboriti ya mierezi na safu za mbao za mierezi.+ 10  Alijenga vyumba vya pembeni kuizunguka,+ kila chumba kilikuwa na kimo cha mikono mitano, navyo viliunganishwa kwenye nyumba hiyo kwa mbao za mierezi. 11  Wakati huo, neno hili la Yehova lilimjia Sulemani: 12  “Kuhusu nyumba hii unayojenga, ikiwa utatembea katika maagizo yangu na kutekeleza sheria zangu* na kushika amri zangu zote kwa kuzifuata,+ mimi pia nitakutimizia ahadi yangu niliyomwahidi baba yako Daudi,+ 13  nami nitakaa miongoni mwa Waisraeli,+ nami sitawaacha watu wangu Waisraeli.”+ 14  Sulemani akaendelea kujenga nyumba hiyo ili aikamilishe. 15  Alijenga kuta za ndani za nyumba hiyo kwa mbao za mierezi. Alifunika kuta za ndani kwa mbao, kuanzia sakafu ya nyumba mpaka kwenye maboriti ya dari, akaifunika sakafu yake kwa mbao za miberoshi.+ 16  Na upande wa nyuma wa nyumba hiyo alijenga sehemu fulani yenye ukubwa wa mikono 20 kwa mbao za mierezi, kuanzia sakafuni mpaka kwenye maboriti, na ndani yake* akajenga chumba cha ndani zaidi,+ yaani, Patakatifu Zaidi.+ 17  Na hekalu*+—sehemu ya nyumba iliyokuwa mbele ya Patakatifu Zaidi—lilikuwa mikono 40. 18  Mbao za mierezi zilizokuwa ndani ya nyumba hiyo zilikuwa na michongo ya vibuyu+ na maua yaliyochanua.+ Sehemu yote ilifunikwa kwa mbao za mierezi; hakuna jiwe ambalo lilionekana. 19  Naye akatayarisha chumba cha ndani zaidi+ katika nyumba hiyo ili kuweka humo sanduku la agano la Yehova.+ 20  Chumba hicho cha ndani zaidi kilikuwa na urefu wa mikono 20, upana wa mikono 20, na kimo cha mikono 20;+ naye akakifunika kwa dhahabu safi; akaifunika madhabahu+ kwa mbao za mierezi. 21  Sulemani aliifunika sehemu ya ndani ya nyumba hiyo kwa dhahabu safi,+ naye akaweka minyororo ya dhahabu kutoka upande mmoja hadi mwingine mbele ya chumba hicho cha ndani zaidi+ kilichokuwa kimefunikwa kwa dhahabu. 22  Aliifunika nyumba yote kwa dhahabu mpaka nyumba yote ilipokamilika; pia aliifunika kwa dhahabu madhabahu yote+ iliyokuwa karibu na chumba cha ndani zaidi. 23  Katika chumba cha ndani zaidi alitengeneza makerubi wawili+ kwa mbao za msonobari,* kila kerubi alikuwa na kimo cha mikono kumi.+ 24  Bawa moja la kerubi lilikuwa na urefu wa mikono mitano, na bawa lingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano. Urefu kutoka ncha ya bawa moja mpaka ncha ya bawa lingine ulikuwa mikono kumi. 25  Kerubi wa pili alikuwa pia na kimo cha mikono kumi. Makerubi wote wawili walikuwa na ukubwa uleule na umbo lilelile. 26  Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mikono kumi, sawa na kimo cha kerubi wa pili. 27  Kisha akawaweka makerubi+ hao ndani ya chumba cha ndani zaidi cha nyumba hiyo.* Mabawa ya makerubi hao yalikunjuliwa hivi kwamba bawa la kerubi moja lilifika kwenye ukuta mmoja na bawa la kerubi mwingine lilifika kwenye ukuta wa pili, na mabawa yao yalipanuka kuelekea katikati ya nyumba hiyo, hivi kwamba yaligusana. 28  Naye aliwafunika makerubi hao kwa dhahabu. 29  Na kwenye kuta zote kuzunguka nyumba hiyo katika vyumba vyote vya ndani na vya nje, alichonga makerubi,+ mitende,+ na maua yaliyochanua.+ 30  Aliifunika sakafu ya nyumba hiyo kwa dhahabu katika vyumba vya ndani na vya nje. 31  Na aliitengeneza milango ya chumba cha ndani zaidi kwa mbao za msonobari, na pia nguzo za pembeni, na miimo yake, ikiwa sehemu ya tano.* 32  Alitengeneza milango hiyo miwili kwa mbao za msonobari, na kwenye milango hiyo alichonga makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, kisha akaifunika kwa dhahabu; akawafunika makerubi hao na mitende hiyo kwa dhahabu akitumia nyundo. 33  Hivyo ndivyo alivyotengeneza miimo ya mlango wa hekalu* iliyokuwa ya mbao za msonobari, zilikuwa sehemu ya nne.* 34  Naye alitengeneza milango miwili kwa mbao za mberoshi. Mlango mmoja ulikuwa na bawaba mbili ambazo zilizunguka kwenye maegemeo, na mlango mwingine ulikuwa na bawaba mbili ambazo zilizunguka kwenye maegemeo.+ 35  Alichonga makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, na kufunika michongo hiyo kwa bamba jembamba la dhahabu. 36  Alijenga ua wa ndani+ kwa safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu ya maboriti ya mierezi.+ 37  Katika mwaka wa nne, mwezi wa Zivu,* msingi wa nyumba ya Yehova ulijengwa;+ 38  na katika mwaka wa 11, mwezi wa Buli,* (yaani, mwezi wa nane), kila kitu katika nyumba hiyo kilikamilishwa kulingana na ramani yake.+ Basi aliijenga kwa miaka saba.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wana wa Israeli.”
Mkono mmoja ulilingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “hekalu la nyumba.”
Au “upana.”
Yaani, Patakatifu.
Tnn., “kulia.”
Tnn., “maamuzi yangu.”
Yaani, ndani ya nyumba hiyo.
Yaani, Patakatifu, palipokuwa mbele ya Patakatifu Zaidi.
Tnn., “mti wa mafuta,” labda ni msonobari wa Aleppo.
Yaani, Patakatifu Zaidi.
Huenda inarejelea ujenzi wa kiunzi cha mlango au ukubwa wa milango.
Yaani, Patakatifu.
Huenda inarejelea ujenzi wa kiunzi cha mlango au ukubwa wa milango.