Kitabu cha Kwanza cha Wafalme 9:1-28

  • Yehova amtokea tena Sulemani (1-9)

  • Zawadi ya Sulemani kwa Mfalme Hiramu (10-14)

  • Miradi mbalimbali ya Sulemani (15-28)

9  Mara tu Sulemani alipomaliza kujenga nyumba ya Yehova, nyumba ya mfalme,*+ na kila kitu ambacho Sulemani alitamani kufanya,+  Yehova akamtokea Sulemani mara ya pili, kama alivyokuwa amemtokea kule Gibeoni.+  Yehova akamwambia: “Nimesikia sala yako na ombi lako la kutaka kibali ulilotoa mbele zangu. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umejenga kwa kuliweka jina langu humu milele,+ na macho yangu na moyo wangu utakuwa humu sikuzote.+  Nawe, ikiwa utatembea mbele zangu kama Daudi baba yako alivyotembea,+ kwa utimilifu wa moyo+ na kwa unyoofu,+ kwa kutenda mambo yote niliyokuamuru,+ nawe ukitii masharti yangu na sheria* zangu,+  ndipo nitakapoimarisha kiti chako cha ufalme juu ya Israeli milele, kama nilivyomwahidi Daudi baba yako, kwa kusema, ‘Hutakosa kamwe mwanamume wa uzao wako atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’+  Lakini ikiwa ninyi na wana wenu mtageuka na kuacha kunifuata na kuacha kushika amri zangu na maagizo yangu ambayo nimeweka mbele yenu, nanyi mwende na kuabudu miungu mingine na kuiinamia,+  nitawaondolea mbali Waisraeli kutoka katika nchi ambayo nimewapa,+ na nyumba ambayo nimeitakasa kwa ajili ya jina langu nitaitupilia mbali kutoka mbele za macho yangu,+ na Israeli itakuwa kitu cha kudharauliwa* na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa mataifa yote.+  Na nyumba hii itakuwa marundo ya magofu.+ Kila mtu atakayepita karibu nayo ataitazama kwa mshangao, atapiga mluzi na kuuliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+  Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova Mungu wao, aliyewatoa mababu zao kutoka nchini Misri, nao wakashikamana na miungu mingine, wakaiinamia na kuiabudu. Ndiyo sababu Yehova aliwaletea msiba huo wote.’”+ 10  Katika muda wa miaka 20 ambayo Sulemani alijenga nyumba hizo mbili, yaani, nyumba ya Yehova na nyumba ya* mfalme,+ 11  Hiramu+ mfalme wa Tiro alimpa Sulemani mbao za mierezi na mbao za miberoshi na dhahabu nyingi sana kadiri alivyohitaji,+ naye Mfalme Sulemani akampa Hiramu majiji 20 katika nchi ya Galilaya. 12  Basi Hiramu akatoka Tiro kwenda kuyaona majiji ambayo Sulemani alikuwa amempa, lakini hakuridhika nayo.* 13  Akamuuliza: “Ndugu yangu, ni majiji gani haya ambayo umenipa?” Basi tangu siku hiyo yakaitwa Nchi ya Kabuli.* 14  Wakati huo, Hiramu akamtumia mfalme talanta 120* za dhahabu.+ 15  Habari ifuatayo inawahusu watu ambao Mfalme Sulemani aliwaandikisha kufanya kazi ya kulazimishwa+ ili wajenge nyumba ya Yehova,+ nyumba yake mwenyewe,* Kilima,*+ ukuta wa Yerusalemu, Hasori,+ Megido,+ na Gezeri.+ 16  (Farao mfalme wa Misri alikuwa amekuja na kuliteka jiji la Gezeri na kuliteketeza kwa moto, na alikuwa pia amewaua Wakanaani+ walioishi katika jiji hilo. Basi akampa binti yake,+ mke wa Sulemani, jiji hilo kama zawadi ya kumuaga.*) 17  Sulemani akalijenga* jiji la Gezeri, Beth-horoni la Chini,+ 18  Baalathi,+ na Tamari lililo nyikani, yaliyokuwa nchini, 19  na pia majiji yote ya Sulemani yenye maghala, majiji ya magari ya vita,+ majiji ya wapanda farasi, na chochote ambacho Sulemani alitamani kujenga huko Yerusalemu, Lebanoni, na katika nchi yote iliyokuwa chini ya mamlaka yake. 20  Watu wengine wote waliobaki miongoni mwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ ambao hawakuwa sehemu ya taifa la Israeli,+ 21  wazao wao waliobaki nchini, ambao Waisraeli walishindwa kuwaangamiza, Sulemani aliwaandikisha ili wafanye kazi ya kulazimishwa kama watumwa mpaka leo hii.+ 22  Lakini Sulemani hakumfanya Mwisraeli yeyote kuwa mtumwa,+ kwa sababu walikuwa mashujaa wake, watumishi, wakuu, makamanda wasaidizi, wakuu wa wale walioendesha magari yake ya vita na wapanda farasi wake. 23  Kulikuwa na wakuu 550 wa wasaidizi waliosimamia kazi ya Sulemani, wasimamizi wa watu waliokuwa wakifanya kazi.+ 24  Lakini binti ya Farao+ akatoka katika Jiji la Daudi+ akaenda kuishi katika nyumba yake ambayo Sulemani alimjengea; kisha Sulemani akajenga Kilima.*+ 25  Mara tatu kwa mwaka+ Sulemani alitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika kwenye madhabahu aliyomjengea Yehova,+ pia alifukiza moshi wa dhabihu kwenye madhabahu iliyokuwa mbele za Yehova, basi akaikamilisha nyumba.+ 26  Mfalme Sulemani akatengeneza pia kundi la meli katika jiji la Esion-geberi,+ lililo kando ya Elothi, ufuoni mwa Bahari Nyekundu katika nchi ya Edomu.+ 27  Hiramu akawatuma watumishi wake mwenyewe, mabaharia wenye uzoefu, wakafanye kazi pamoja na watumishi wa Sulemani kwenye kundi hilo la meli.+ 28  Wakaenda Ofiri,+ wakachukua talanta 420 za dhahabu na kumletea Mfalme Sulemani.

Maelezo ya Chini

Au “jumba la mfalme.”
Tnn., “hukumu.”
Tnn., “methali.”
Au “jumba la.”
Tnn., “hayakuwa sawa machoni pake.”
Au labda, “Nchi Isiyofaa Kitu.”
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Au “Milo.” Neno la Kiebrania linalomaanisha “jaza.”
Au “jumba lake mwenyewe la mfalme.”
Au “zawadi ya harusi; mahari.”
Au “akaliimarisha.”
Au “Milo.” Neno la Kiebrania linalomaanisha “jaza.”