Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 1:1-31

  • Salamu (1-3)

  • Paulo amshukuru Mungu kwa sababu ya Wakorintho (4-9)

  • Wahimizwa kuwa na umoja (10-17)

  • Kristo, nguvu na hekima ya Mungu (18-25)

  • Kujisifu tu katika Yehova (26-31)

1  Paulo, aliyeitwa kuwa mtume+ wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,  kwa kutaniko la Mungu lililo huko Korintho,+ kwenu ninyi ambao mmetakaswa katika muungano na Kristo Yesu,+ mlioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo,+ Bwana wao na wetu:  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.  Sikuzote ninamshukuru Mungu wangu kwa ajili yenu kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu mlizopewa katika Kristo Yesu;  kwa kuwa katika yeye mmetajirishwa katika kila jambo, katika uwezo kamili wa kusema na katika ujuzi kamili,+  kama vile ushahidi kumhusu Kristo+ ulivyofanywa kuwa imara miongoni mwenu,  ili msipungukiwe hata kidogo katika zawadi yoyote, huku mkisubiri kwa hamu ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.+  Yeye pia atawafanya ninyi muwe imara mpaka mwisho, ili msiwe na shtaka lolote katika siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.+  Mungu ni mwaminifu,+ aliyewaita muwe na ushirika pamoja na Mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu. 10  Sasa ninawahimiza ninyi, akina ndugu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mseme kwa upatano, na kwamba kusiwe na migawanyiko kati yenu,+ bali kwamba muunganishwe kabisa katika akili ileile na njia ileile ya kufikiri.+ 11  Kwa maana baadhi ya watu wa nyumba ya Kloe wamenijulisha kuwahusu ninyi ndugu zangu, kwamba kuna ugomvi kati yenu. 12  Ninalomaanisha ni hili, kwamba kila mmoja wenu anasema: “Mimi ni wa Paulo,” “Lakini mimi ni wa Apolo,”+ “Lakini mimi ni wa Kefa,”* “Lakini mimi ni wa Kristo.” 13  Je, Kristo amegawanyika? Paulo hakuuawa kwenye mti kwa ajili yenu, sivyo? Au je, mlibatizwa katika jina la Paulo? 14  Ninamshukuru Mungu kwa kuwa sikumbatiza hata mmoja wenu isipokuwa Krispo+ na Gayo,+ 15  ili yeyote asiseme kwamba mlibatizwa katika jina langu. 16  Ndiyo, niliibatiza pia nyumba ya Stefana.+ Kuhusu wale wengine, sijui kama nilimbatiza mwingine yeyote. 17  Kwa maana Kristo alinituma, si kubatiza, bali kutangaza habari njema;+ na si kwa maneno ya hekima,* ili mti wa mateso* wa Kristo usifanywe kuwa kitu kisicho na maana. 18  Kwa maana maneno kuhusu mti wa mateso* ni upumbavu kwa wale wanaoangamia,+ lakini kwetu sisi tunaookolewa, ni nguvu za Mungu.+ 19  Kwa maana imeandikwa: “Nitaiangamiza hekima ya watu wenye hekima, nami nitaikataa* akili ya watu wenye akili.”+ 20  Yuko wapi mtu mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi?* Yuko wapi anayebishania maneno katika mfumo huu wa mambo?* Je, Mungu hakuifanya hekima ya ulimwengu iwe upumbavu? 21  Kwa kuwa, katika hekima ya Mungu, ulimwengu haukumjua Mungu+ kupitia hekima yake,+ Mungu alipenda kuwaokoa wale wanaoamini kupitia upumbavu+ wa ujumbe unaohubiriwa. 22  Kwa maana Wayahudi wanaomba ishara+ na Wagiriki wanatafuta hekima; 23  lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyeuawa kwenye mti, kwa Wayahudi ni sababu ya kujikwaa lakini kwa mataifa ni upumbavu.+ 24  Hata hivyo, kwa wale walioitwa, Wayahudi na Wagiriki, Kristo ni nguvu za Mungu na hekima ya Mungu.+ 25  Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu kuliko wanadamu.+ 26  Kwa maana akina ndugu, mnaona mwito wake kwenu, kwamba si wengi wenye hekima kwa njia ya kimwili,*+ si wengi wenye nguvu, si wengi wa kutoka familia mashuhuri,+ 27  bali Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe watu wenye hekima; na Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu, ili aviaibishe vitu vyenye nguvu;+ 28  na Mungu alivichagua vitu vinyonge vya ulimwengu na vitu vinavyodharauliwa, vitu ambavyo si kitu, ili kuvifanya vitu ambavyo ni kitu visiwe kitu,+ 29  ili mtu yeyote asijisifu* machoni pa Mungu. 30  Lakini ni kwa sababu yake kwamba ninyi mko katika muungano na Kristo Yesu, ambaye kwetu amekuwa hekima kutoka kwa Mungu, pia uadilifu+ na utakaso+ na kuachiliwa huru kupitia fidia,+ 31  ili iwe kama ilivyoandikwa: “Yule anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.”*+

Maelezo ya Chini

Pia anaitwa Petro.
Au “ujanja.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “nitaiweka kando.”
Yaani, mtaalamu wa Sheria.
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “kwa viwango vya wanadamu.”
Tnn., “mwili wowote usijisifu.”