Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 12:1-31

  • Zawadi za roho (1-11)

  • Mwili mmoja, viungo vingi (12-31)

12  Basi kuhusu zawadi za kiroho,+ akina ndugu, sitaki mkose kujua.  Mnajua kwamba mlipokuwa watu wa mataifa,* mlikuwa mkishawishiwa na kuziabudu sanamu zisizo na sauti,+ mkizifuata popote zilipowaongoza.  Sasa ningetaka mjue kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anaposema kwa roho ya Mungu, husema: “Yesu amelaaniwa!” na hakuna mtu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana!” isipokuwa kwa roho takatifu.+  Basi kuna zawadi mbalimbali, lakini kuna roho ileile;+  na kuna huduma mbalimbali,+ na bado kuna Bwana yuleyule;  na kuna utendaji* mbalimbali, na bado ni Mungu yuleyule anayefanya utendaji huo wote katika kila mtu.+  Lakini roho hufunuliwa katika kila mmoja kwa kusudi lenye faida.+  Kwa maana mtu mmoja hupewa maneno ya* hekima kupitia roho, mwingine maneno ya ujuzi kulingana na roho ileile,  mwingine imani+ kwa roho ileile, mwingine zawadi za uponyaji+ kwa roho hiyo moja, 10  naye mwingine hupewa utendaji wa matendo yenye nguvu,+ mwingine kutoa unabii, mwingine utambuzi wa maneno yaliyoongozwa na roho,+ mwingine lugha* mbalimbali,+ na mwingine fasiri ya lugha.+ 11  Lakini ni roho ileile inayofanya utendaji huu wote, ikimgawia kila mmoja kama vile inavyopenda. 12  Kwa maana kama vile mwili ni mmoja lakini una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili huo, ingawa ni vingi, ni mwili mmoja,+ ndivyo pia alivyo Kristo. 13  Kwa maana kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja, iwe ni Wayahudi au ni Wagiriki, iwe ni watumwa au ni walio huru, nasi sote tulinyweshwa roho moja. 14  Kwa maana kwa kweli, mwili una viungo vingi, si kiungo kimoja.+ 15  Ikiwa mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hilo halifanyi usiwe sehemu ya mwili. 16  Na ikiwa sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hilo halilifanyi lisiwe sehemu ya mwili. 17  Ikiwa mwili wote ungekuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Ikiwa wote ungekuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi? 18  Lakini sasa Mungu amepanga kila kiungo cha mwili kama alivyopenda. 19  Ikiwa vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? 20  Lakini sasa viungo ni vingi, lakini mwili mmoja. 21  Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sikuhitaji wewe,” au tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Siwahitaji ninyi.” 22  Badala yake viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu zaidi ni muhimu sana, 23  na sehemu za mwili ambazo tunafikiri hazistahili kuheshimiwa sana, tunazipa heshima zaidi,+ basi sehemu zetu ambazo hazivutii tunazitendea kwa heshima* zaidi, 24  bali sehemu zetu zinazopendeza hazihitaji kitu chochote. Lakini hivyo ndivyo Mungu alivyouunganisha mwili, akiipa heshima zaidi sehemu iliyokuwa na upungufu, 25  ili kusiwe na mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyake vitunzane.+ 26  Kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote huumia pamoja nacho;+ au kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vingine vyote hushangilia pamoja nacho.+ 27  Basi ninyi ni mwili wa Kristo,+ na kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.+ 28  Naye Mungu amewaweka watu mbalimbali katika kutaniko: kwanza, mitume;+ pili, manabii;+ tatu, walimu;+ kisha matendo yenye nguvu;+ kisha zawadi za uponyaji;+ huduma za kusaidia; uwezo wa kuelekeza;+ na lugha mbalimbali.+ 29  Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote hufanya matendo yenye nguvu? 30  Je, wote wana zawadi za uponyaji? Je, wote husema kwa lugha?+ Je, wote ni wakalimani?*+ 31  Lakini endeleeni kutafuta kwa bidii* zawadi zilizo kubwa zaidi.+ Na bado nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.+

Maelezo ya Chini

Yaani, watu wasio waamini.
Au “kazi.”
Au “ujumbe wa.”
Au “ndimi.”
Au “kiasi.”
Au “watafsiri.”
Au “kujitahidi kupata.”