Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 13:1-13

  • Upendo​—⁠njia bora zaidi (1-13)

13  Nikisema kwa lugha za wanadamu na za malaika lakini sina upendo, nimekuwa chuma kinachovuma au toazi linalolia.  Na ikiwa nina zawadi ya kutoa unabii nami ninazielewa siri zote takatifu na ujuzi wote,+ na ikiwa nina imani yenye nguvu hata niweze kuhamisha* milima, lakini sina upendo, mimi si kitu.*+  Nami nikitoa mali zangu zote ili kuwalisha wengine,+ na nikiutoa mwili wangu ili nijisifu, lakini sina upendo,+ sipati faida yoyote.  Upendo+ ni wenye subira*+ na fadhili.+ Upendo hauna wivu.+ Haujigambi, haujivuni,+  haujiendeshi bila adabu,+ hautafuti faida zake wenyewe,+ hauchokozeki.+ Hauweki hesabu ya ubaya.*+  Haushangilii ukosefu wa uadilifu,+ bali hushangilia pamoja na kweli.  Huhimili mambo yote,+ huamini mambo yote,+ hutumaini mambo yote,+ huvumilia mambo yote.+  Upendo haushindwi kamwe. Lakini kama kuna zawadi za unabii, zitaondolewa; kama kuna lugha,* zitakoma; kama kuna ujuzi, utaondolewa.  Kwa maana tuna ujuzi usio kamili+ nasi tunatoa unabii usio kamili; 10  lakini kile kilicho kamili kitakapokuja, kile kisicho kamili kitaondolewa. 11  Nilipokuwa mtoto, nilikuwa nikisema kama mtoto, nikifikiri kama mtoto, nikiwaza kama mtoto; lakini kwa kuwa sasa nimekuwa mtu mzima, nimeziacha tabia za mtoto. 12  Kwa maana sasa tunaona kwa njia isiyo ya waziwazi* kupitia kioo cha chuma, lakini wakati huo itakuwa uso kwa uso. Kwa sasa sijui kikamili, lakini wakati huo nitajua kwa usahihi,* kama vile ninavyojulikana kwa usahihi. 13  Hata hivyo, sasa yanabaki mambo haya matatu: imani, tumaini, upendo; lakini lililo kubwa zaidi kati ya hayo ni upendo.+

Maelezo ya Chini

Au “kusogeza.”
Au “sifai kitu.”
Au “ustahimilivu.”
Au “makosa.”
Yaani, kuzungumza lugha nyingine kimuujiza.
Au “iliyo hafifu.”
Au “kikamili.”