Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 14:1-40

  • Zawadi za unabii na lugha (1-25)

  • Mikutano ya Kikristo yenye utaratibu (26-40)

    • Sehemu ya wanawake katika kutaniko (34, 35)

14  Fuatieni upendo, na bado endeleeni kutafuta kwa bidii* zawadi za kiroho, lakini ni afadhali zaidi kwamba mtoe unabii.+  Kwa maana yule anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu, bali na Mungu, kwa maana hakuna anayesikiliza,+ bali yeye husema kwa roho siri zilizo takatifu.+  Hata hivyo, yule anayetoa unabii huwajenga na kuwatia moyo na kuwafariji watu kwa maneno yake.  Yule anayesema kwa lugha hujijenga mwenyewe, lakini yule anayetoa unabii hulijenga kutaniko.  Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha,+ lakini ninapendelea zaidi mtoe unabii.+ Kwa kweli, yule anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yule anayezungumza kwa lugha, isipokuwa afasiri* kwa ajili ya kutaniko ili lijengwe.  Lakini wakati huu, akina ndugu, kama ningekuja kwenu nikisema kwa lugha, ningewapa faida gani kama singezungumza nanyi kwa ufunuo+ au kwa ujuzi+ au kwa unabii au kwa fundisho?  Ndivyo ilivyo pia kwa vitu visivyo na uhai ambavyo hutoa sauti, iwe ni filimbi au kinubi. Kusipokuwa na tofauti kati ya sauti, kinachopigwa kwenye filimbi au kwenye kinubi kitajulikanaje?  Kwa maana tarumbeta ikipiga mwito usiojulikana, ni nani atakayejitayarisha kwa ajili ya vita?  Vivyo hivyo, msiposema maneno yanayoeleweka kwa urahisi kupitia lugha hiyo, watu watajuaje kinachosemwa? Kwa kweli, mtakuwa mkizungumza hewani. 10  Huenda kuna aina nyingi za maneno ulimwenguni, hata hivyo hakuna aina isiyo na maana. 11  Ikiwa sielewi maana ya maneno, nitakuwa mgeni kwa yule anayezungumza, naye anayezungumza atakuwa mgeni kwangu. 12  Nanyi pia, kwa kuwa mnatamani sana zawadi za roho, jitahidini kujawa na zawadi ambazo zitalijenga kutaniko.+ 13  Kwa hiyo, yule anayezungumza kwa lugha na asali ili afasiri.*+ 14  Kwa maana ikiwa ninasali kwa lugha, ni zawadi yangu ya roho inayosali, lakini akili yangu haizai matunda. 15  Basi, nini kifanywe? Nitasali kwa zawadi ya roho, lakini nitasali pia kwa akili yangu. Nitaimba sifa kwa zawadi ya roho, lakini pia nitaimba sifa kwa akili yangu. 16  Kama sivyo, ukitoa sifa kwa zawadi ya roho, mtu wa kawaida miongoni mwenu atasemaje “Amina” unapotoa shukrani, kwa kuwa hajui unachosema? 17  Kweli, unatoa shukrani kwa njia nzuri, lakini yule mtu mwingine hajengwi. 18  Ninamshukuru Mungu kwamba ninasema kwa lugha nyingi kuliko ninyi nyote. 19  Hata hivyo, katika kutaniko afadhali niseme maneno matano kwa akili yangu,* ili pia niwafundishe* wengine, kuliko maneno elfu kumi kwa lugha.+ 20  Akina ndugu, msiwe watoto wadogo katika uelewaji wenu,+ lakini iweni watoto wadogo kuhusiana na ubaya;+ nanyi muwe watu wazima katika uelewaji wenu.+ 21  Katika Sheria imeandikwa: “‘Nitazungumza na watu hawa kwa lugha za watu wa kigeni na kwa midomo ya wageni, na hata wakati huo watakataa kunisikiliza,’ asema Yehova.”*+ 22  Kwa hiyo, lugha si ishara kwa ajili ya waamini bali kwa wasio waamini,+ lakini unabii si kwa ajili ya wasio waamini bali ni kwa ajili ya waamini. 23  Basi kutaniko lote likikusanyika mahali pamoja na wote waseme kwa lugha, nao watu wa kawaida au wasio waamini waingie, je, hawatasema kwamba ninyi mmerukwa na akili? 24  Lakini ikiwa nyote mnatoa unabii na mtu asiye mwamini au mtu wa kawaida aingie, atakaripiwa na kuchunguzwa na wote. 25  Siri za moyo wake zitakuwa wazi, hivi kwamba ataanguka kifudifudi na kumwabudu Mungu, akitangaza: “Kwa kweli Mungu yupo kati yenu.”+ 26  Basi, tuseme nini akina ndugu? Mnapokusanyika pamoja, mmoja ana zaburi, mwingine ana fundisho, mwingine ana ufunuo, mwingine ana lugha, na mwingine ana fasiri.+ Mambo yote na yatendeke kwa ajili ya kujenga. 27  Mtu akisema kwa lugha, na wawe wawili au wasizidi watatu, na wafanye hivyo kwa zamu, na lazima mtu fulani afasiri.*+ 28  Lakini ikiwa hakuna mkalimani,* anapaswa kukaa kimya kutanikoni na kuzungumza moyoni mwake na kwa Mungu. 29  Manabii+ wawili au watatu na wazungumze, na wale wengine watambue maana. 30  Lakini ikiwa mwingine anapokea ufunuo akiwa ameketi hapo, msemaji wa kwanza anapaswa kukaa kimya. 31  Kwa maana nyote mnaweza kutoa unabii kila mtu kwa wakati wake, ili wote wajifunze na wote watiwe moyo.+ 32  Na zawadi za roho ya manabii zinapaswa kuelekezwa na manabii. 33  Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni wa amani.+ Kama ilivyo katika makutaniko yote ya watakatifu, 34  wanawake na wakae kimya katika makutaniko, kwa maana hawaruhusiwi kuzungumza.+ Badala yake, na wajitiishe,+ kama vile Sheria inavyosema pia. 35  Ikiwa wanataka kujifunza jambo fulani, acheni wawaulize waume zao nyumbani, kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kutanikoni. 36  Je, neno la Mungu lilitoka kwenu, au liliwafikia ninyi peke yenu? 37  Ikiwa yeyote anafikiri yeye ni nabii au amepewa zawadi ya roho, anapaswa kutambua kwamba mambo ninayowaandikia ni amri ya Bwana. 38  Lakini yeyote akiyapuuza, yeye pia atapuuzwa.* 39  Basi ndugu zangu, endeleeni kujitahidi kutoa unabii,+ na bado msikataze kusema kwa lugha.+ 40  Lakini mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango.*+

Maelezo ya Chini

Au “kujitahidi kupata.”
Au “atafsiri.”
Au “atafsiri.”
Au “uelewaji.”
Au “niwafundishe kwa mdomo.”
Au “atafsiri.”
Au “mtafsiri.”
Au labda, “Ikiwa yeyote hajui, ataendelea kutojua.”
Au “kwa utaratibu.”