Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 4:1-21

  • Wasimamizi wanapaswa kuwa waaminifu (1-5)

  • Unyenyekevu wa wahudumu Wakristo (6-13)

    • “Msipite mambo yaliyoandikwa” (6)

    • Wakristo ni tamasha (9)

  • Paulo awajali watoto wake wa kiroho (14-21)

4  Mtu anapaswa kutuona kuwa wahudumu* wa Kristo na wasimamizi wa siri takatifu za Mungu.+  Katika hali hii, kinachotarajiwa katika wasimamizi ni kupatwa wakiwa waaminifu.  Basi kwangu si muhimu sana kuchunguzwa na ninyi au na mahakama.* Hata mimi sijichunguzi mwenyewe.  Kwa maana sioni kosa lolote dhidi yangu mwenyewe. Lakini hilo halithibitishi kuwa mimi ni mwadilifu; anayenichunguza ni Yehova.*+  Kwa hiyo, msihukumu+ chochote kabla ya wakati unaofaa, mpaka Bwana aje. Ataleta mambo ya siri yaliyo ya giza kwenye nuru na pia kujulisha nia za mioyo, na ndipo kila mtu atakapopokea sifa yake kutoka kwa Mungu.+  Basi, akina ndugu, mambo haya nimeyatumia* kujihusu mimi mwenyewe na Apolo+ kwa faida yenu, ili kupitia sisi mjifunze kanuni hii: “Msipite mambo yaliyoandikwa,” ili msiwe na kiburi,+ na kumpendelea mtu mmoja kuliko mwingine.  Kwa maana ni nani anayekufanya wewe kuwa tofauti na mwingine? Kwa kweli, una nini ambacho hukupokea?+ Basi, ikiwa kwa kweli ulikipokea, kwa nini unajisifu kana kwamba hukukipokea?  Je, tayari mmetosheka? Je, tayari ninyi ni matajiri? Je, mmeanza kutawala mkiwa wafalme+ bila sisi? Ninatamani sana kwamba muwe mmeanza kutawala mkiwa wafalme, ili sisi pia tutawale pamoja nanyi tukiwa wafalme.+  Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume mwisho katika wonyesho wa hadharani kama watu waliohukumiwa kifo,+ kwa sababu tumekuwa tamasha kwa ulimwengu,+ na kwa malaika, na kwa wanadamu. 10  Sisi ni wapumbavu+ kwa sababu ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara katika Kristo; sisi ni dhaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu; ninyi mnaheshimika, lakini sisi hatuheshimiki. 11  Mpaka saa hii tunaendelea kuwa na njaa+ na kiu+ na kukosa mavazi ya kutosha* na kupigwa*+ na kuwa bila makao 12  na kufanya kazi ya taabu, tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe.+ Tunapotukanwa, tunabariki;+ tunapoteswa, tunavumilia kwa subira;+ 13  tunapochongewa, tunajibu kwa upole;*+ tumekuwa kama takataka ya ulimwengu, uchafu wa vitu vyote, mpaka sasa. 14  Ninaandika mambo haya, si ili niwaaibishe, bali niwaonye kama watoto wangu wapendwa. 15  Kwa maana ingawa huenda mkawa na walezi* 10,000 katika Kristo, hakika hamna baba wengi; kwa maana katika Kristo Yesu mimi nimekuwa baba yenu kupitia habari njema.+ 16  Kwa hiyo, ninawasihi, iweni waigaji wangu.+ 17  Ndiyo sababu ninamtuma Timotheo kwenu, kwa kuwa yeye ni mtoto wangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusha njia* zangu kuhusiana na Kristo Yesu,+ kama vile ninavyofundisha kila mahali katika kila kutaniko. 18  Wengine wamekuwa na kiburi wakidhani kwamba siji kwenu. 19  Lakini nitakuja kwenu hivi karibuni, Yehova* akipenda, nami nitajua, si maneno ya wale walio na kiburi, bali nguvu zao. 20  Kwa maana Ufalme wa Mungu si maneno tu bali ni nguvu. 21  Mngependa nini? Je, nije kwenu nikiwa na fimbo+ au kwa upendo na upole wa roho?

Maelezo ya Chini

Au “wasaidizi.”
Au “baraza la wanadamu.”
Au “nimeyahamisha.”
Au “kupigwa huku na huku.”
Tnn., “kuwa uchi.”
Tnn., “tunasihi.”
Au “watunzaji.”
Au “mbinu.”