Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 5:1-13

  • Kisa cha uasherati (1-5)

  • Chachu kidogo huchachisha donge lote (6-8)

  • Mtu mwovu aondolewe (9-13)

5  Kwa kweli kuna habari kwamba kuna uasherati*+ miongoni mwenu, tena uasherati* ambao haujatokea hata miongoni mwa mataifa—mwanamume kuishi* na mke wa baba yake.+  Na je, ninyi mnajivunia jambo hilo? Je, hampaswi kuomboleza+ ili mtu aliyefanya kitendo hicho aondolewe miongoni mwenu?+  Ingawa sipo katika mwili, nipo katika roho, tayari nimemhukumu mtu huyo ambaye amefanya tendo hilo, kana kwamba nipo pamoja nanyi.  Mnapokusanyika pamoja katika jina la Bwana wetu Yesu, na kujua kwamba nipo nanyi katika roho pamoja na nguvu za Bwana wetu Yesu,  lazima mumkabidhi mtu wa namna hiyo kwa Shetani+ kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili, ili roho iokolewe katika siku ya Bwana.+  Kujisifu kwenu hakufai. Je, hamjui kwamba chachu* kidogo huchachisha donge lote?+  Ondoeni chachu ya zamani, ili muwe donge jipya, kwa kuwa ninyi hamna chachu. Kwa maana, kwa kweli, Kristo mwanakondoo wetu wa Pasaka+ ametolewa dhabihu.+  Basi na tufanye sherehe,+ si kwa chachu ya zamani, wala kwa chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mikate isiyo na chachu ya unyoofu na kweli.  Katika barua yangu niliwaandikia mwache kushirikiana* na waasherati,* 10  si kumaanisha waasherati* wa ulimwengu huu+ au watu wenye pupa na wanyang’anyi au waabudu-sanamu. Kama ingekuwa hivyo, kwa kweli ingewabidi mwondoke katika ulimwengu.+ 11  Lakini sasa ninawaandikia mwache kushirikiana*+ na mtu yeyote anayeitwa ndugu ambaye ni mwasherati* au mtu mwenye pupa+ au anayeabudu sanamu au mtukanaji* au mlevi+ au mnyang’anyi,+ hata msile chakula pamoja na mtu wa namna hiyo. 12  Kwa maana inanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Je, ninyi hamwahukumu wale walio ndani, 13  huku Mungu akiwahukumu wale walio nje?+ “Mwondoeni mtu mwovu miongoni mwenu.”+

Maelezo ya Chini

Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Tnn., “kuwa.”
Au “hamira.”
Au “kuchangamana.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “kuchangamana.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “mtu anayetumia maneno machafu.”