Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 6:1-20

  • Kesi miongoni mwa akina ndugu Wakristo (1-8)

  • Wale ambao hawataurithi Ufalme (9-11)

  • Mtukuzeni Mungu katika miili yenu (12-20)

    • “Ukimbieni uasherati!” (18)

6  Je, kuna yeyote kati yenu aliye na ugomvi na mwenzake+ atakayethubutu kwenda mahakamani mbele ya watu wasio waadilifu, na si mbele ya watakatifu?  Au je, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu?+ Na ikiwa ninyi mtauhukumu ulimwengu, je, hamna uwezo wa kuamua mambo madogo sana?  Je, hamjui kwamba tutawahukumu malaika?+ Basi, kwa nini isiwe mambo ya maisha haya?  Basi, ikiwa mna mambo ya maisha haya yanayohitaji kuamuliwa,+ je, mnawaweka watu wanaodharauliwa na kutaniko kuwa waamuzi?  Ninasema ili kuwatia ninyi aibu. Je, hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima miongoni mwenu anayeweza kuhukumu kati ya ndugu zake?  Badala yake ndugu anaenda mahakamani kumshtaki ndugu, na tena mbele ya wasio waamini!  Kwa kweli, tayari mmeshindwa mnapokuwa na mashtaka ya kisheria wenyewe kwa wenyewe. Je, si afadhali mkubali kukosewa?+ Je, si afadhali mkubali kupunjwa?  Badala yake, mnawakosea na kuwapunja, tena ndugu zenu!  Au je, hamjui kwamba watu wasio waadilifu hawataurithi Ufalme wa Mungu?+ Msipotoshwe.* Waasherati,*+ waabudu-sanamu,+ wazinzi,+ wanaume wanaofanya ngono na wanaume,*+ 10  wezi, watu wenye pupa,+ walevi,+ watukanaji,* na wanyang’anyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.+ 11  Na bado baadhi yenu mlikuwa hivyo. Lakini mmeoshwa mkawa safi;+ mmetakaswa;+ mmetangazwa kuwa waadilifu+ katika jina la Bwana Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu. 12  Mambo yote ni halali* kwangu, lakini si mambo yote yenye faida.+ Mambo yote ni halali kwangu, lakini sitaruhusu kitu chochote kinitawale.* 13  Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa ajili ya chakula, lakini Mungu atavifanya vyote viwe si kitu.+ Mwili si kwa ajili ya uasherati,* bali ni kwa ajili ya Bwana,+ na Bwana ni kwa ajili ya mwili. 14  Lakini Mungu alimfufua Bwana+ na pia atatufufua sisi kutoka kwenye kifo+ kupitia nguvu zake.+ 15  Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Kristo?+ Basi, je, nivichukue viungo vya Kristo na kuviunganisha na kahaba? La hasha! 16  Je, hamjui kwamba yeyote ambaye ameungana na kahaba ni mwili mmoja naye? Kwa maana yeye anasema, “hao wawili watakuwa mwili mmoja.”+ 17  Lakini yeyote anayeungana na Bwana ana umoja naye katika roho.+ 18  Ukimbieni uasherati!*+ Dhambi nyingine yoyote ambayo huenda mtu akafanya iko nje ya mwili wake, lakini yeyote aliye na mazoea ya kufanya uasherati anautendea dhambi mwili wake mwenyewe.+ 19  Je, hamjui kwamba mwili wenu ni hekalu+ la roho takatifu ndani yenu, mliyopokea kutoka kwa Mungu?+ Pia, ninyi si mali yenu wenyewe,+ 20  kwa maana mlinunuliwa kwa bei.+ Kwa vyovyote, mtukuzeni Mungu+ katika mwili wenu.+

Maelezo ya Chini

Au “Msidanganywe.”
Au “wanaume wanaotenda au kukubali kutendewa mambo hayo.” Tnn., “wanaume wanaolala na wanaume.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “watu wanaotumia maneno machafu.”
Au “sitakubali kuwa chini ya mamlaka ya kitu chochote.”
Au “yanakubalika.’
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.