Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 8:1-13

  • Kuhusu chakula kinachotolewa kwa sanamu (1-13)

    • Kwetu kuna Mungu mmoja tu (5, 6)

8  Basi kuhusu chakula kilichotolewa kwa sanamu:+ Tunajua sote tuna ujuzi.+ Ujuzi huleta majivuno, lakini upendo hujenga.+  Yeyote akifikiri anajua jambo fulani, bado hajalijua kama anavyopaswa kulijua.  Lakini ikiwa yeyote anampenda Mungu, huyo anajulikana naye.  Sasa kuhusu kula chakula kilichotolewa kwa sanamu, tunajua kwamba sanamu si kitu+ ulimwenguni na kwamba hakuna Mungu isipokuwa mmoja.+  Kwa maana hata ingawa kuna wale wanaoitwa miungu, iwe ni mbinguni au duniani,+ kama vile kulivyo na “miungu” mingi na “mabwana” wengi,  kwa kweli kwetu kuna Mungu mmoja+ aliye Baba,+ ambaye vitu vyote vimetoka kwake na sisi kwa ajili yake;+ na kuna Bwana mmoja, Yesu Kristo, ambaye vitu vyote vimepitia kwake+ na sisi kupitia kwake.  Hata hivyo, si watu wote walio na ujuzi huu.+ Lakini wengine, kwa sababu zamani waliabudu sanamu, wanakula chakula kama kitu kilichotolewa dhabihu kwa sanamu,+ na dhamiri yao, kwa kuwa ni dhaifu, inatiwa unajisi.+  Lakini chakula hakitafanya tumkaribie zaidi Mungu;+ hatupotezi chochote tusipokula, wala hatuongezi chochote tunapokula.+  Lakini endeleeni kujihadhari kwamba haki yenu ya kuchagua isije ikawa kwa njia fulani kikwazo kwa wale walio dhaifu.+ 10  Kwa maana yeyote akikuona wewe uliye na ujuzi ukila mlo katika hekalu la sanamu, je, dhamiri ya huyo aliye dhaifu haitapata ujasiri kufikia hatua ya kula chakula kilichotolewa kwa sanamu? 11  Basi, kwa ujuzi wako, mtu ambaye ni dhaifu anaharibiwa, ndugu yako ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.+ 12  Mnapowatendea dhambi ndugu zenu katika njia hii na kuiumiza dhamiri yao dhaifu,+ mnamtendea dhambi Kristo. 13  Kwa sababu hiyo, ikiwa chakula kinamkwaza ndugu yangu, mimi sitakula nyama tena kamwe, ili nisije nikamkwaza ndugu yangu.+

Maelezo ya Chini