Barua ya Kwanza ya Yohana 1:1-10

  • Neno la uzima (1-4)

  • Kutembea katika nuru (5-7)

  • Uhitaji wa kuungama dhambi (8-10)

1  Kile kilichokuwapo tangu mwanzo, tulichokisikia na kukiona kwa macho yetu, ambacho tumekitazama na mikono yetu ikakigusa, kuhusiana na neno la uzima,+  (ndiyo, uzima ulifunuliwa, nasi tumeona na tunatoa ushahidi+ na kuwajulisha kuhusu uzima wa milele+ ambao Baba alikuwa nao, na uliofunuliwa kwetu),  kile ambacho tumeona na kusikia tunawajulisha pia,+ ili ninyi vilevile muwe na ushirika pamoja nasi. Na huu ushirika wetu ni pamoja na Baba na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.+  Nasi tunaandika mambo haya ili shangwe yetu iwe kamili.  Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake nasi tunawatangazia ninyi: Mungu ni nuru,+ na hakuna giza kamwe ndani yake.*  Ikiwa tunasema, “Tuna ushirika pamoja naye,” na bado tunaendelea kutembea katika giza, tunasema uwongo nasi hatuishi kulingana na kweli.+  Hata hivyo, ikiwa tunatembea katika nuru kama yeye mwenyewe alivyo katika nuru, tuna ushirika sisi kwa sisi, na damu ya Yesu Mwana wake hutusafisha kutoka katika dhambi yote.+  Ikiwa tunasema, “Hatuna dhambi,” tunajipotosha wenyewe+ na kweli haimo ndani yetu.  Tukiungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na mwadilifu naye atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha ukosefu wote wa uadilifu.+ 10  Ikiwa tunasema, “Hatujatenda dhambi,” tunamfanya yeye kuwa mwongo, na neno lake halimo ndani yetu.

Maelezo ya Chini

Au “katika muungano naye.”