Barua ya Kwanza ya Yohana 3:1-24

  • Sisi ni watoto wa Mungu (1-3)

  • Tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi (4-12)

    • Yesu atazivunja kazi za Ibilisi (8)

  • Mpendane (13-18)

  • Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu (19-24)

3  Oneni upendo ambao Baba ametuonyesha,+ kwamba tunapaswa kuitwa watoto wa Mungu!+ Na hivyo ndivyo tulivyo. Ndiyo sababu ulimwengu hautujui,+ kwa sababu haumjui yeye.+  Wapendwa, sasa sisi ni watoto wa Mungu,+ lakini bado haijafunuliwa jinsi tutakavyokuwa.+ Tunajua kwamba atakapofunuliwa tutakuwa kama yeye, kwa sababu tutamwona kama alivyo.  Na kila mtu aliye na tumaini hili ndani yake hujisafisha,+ kama huyo alivyo safi.  Kila mtu aliye na mazoea ya kufanya dhambi anaendelea pia kufanya uasi sheria, na dhambi ni uasi sheria.  Mnajua pia kwamba alifunuliwa ili kuondoa dhambi zetu,+ na hakuna dhambi ndani yake.  Kila mtu anayekaa katika muungano na yeye hana mazoea ya kufanya dhambi;+ mtu yeyote aliye na mazoea ya kufanya dhambi hajamwona wala kumjua.  Watoto wadogo, yeyote asiwapotoshe; mtu anayeendelea kufanya uadilifu ni mwadilifu, kama huyo alivyo mwadilifu.  Mtu aliye na mazoea ya kufanya dhambi hutokana na Ibilisi, kwa sababu Ibilisi amekuwa akifanya dhambi tangu mwanzo.*+ Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alifunuliwa, ili avunje* kazi za Ibilisi.+  Kila mtu ambaye amezaliwa kutokana na Mungu haendelei kufanya dhambi,+ kwa sababu mbegu* Yake hukaa ndani ya mtu huyo, naye hawezi kuendelea kufanya dhambi, kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.+ 10  Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni wazi kwa jambo hili: Yeyote ambaye haendelei kufanya uadilifu hatokani na Mungu, wala yule ambaye hampendi ndugu yake.+ 11  Kwa maana huu ndio ujumbe ambao mmesikia tangu mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana;+ 12  si kama Kaini, aliyetokana na yule mwovu akamuua ndugu yake. Na kwa nini alimuua?+ Kwa sababu matendo yake mwenyewe yalikuwa maovu,+ lakini matendo ya ndugu yake yalikuwa ya uadilifu.+ 13  Akina ndugu, msishangae kwamba ulimwengu unawachukia.+ 14  Tunajua kwamba tumevuka kutoka kifo mpaka uzima,+ kwa sababu tunawapenda akina ndugu.+ Mtu ambaye hapendi hukaa katika kifo.+ 15  Kila mtu anayemchukia ndugu yake ni muuaji,+ nanyi mnajua kwamba hakuna muuaji aliye na uzima wa milele ndani yake.+ 16  Sisi tumeujua upendo, kwa sababu huyo alitoa uhai wake* kwa ajili yetu,+ nasi tuna wajibu wa kutoa uhai wetu* kwa ajili ya ndugu zetu.+ 17  Lakini yeyote aliye na mali za ulimwengu huu akimwona ndugu yake akiwa na uhitaji naye akatae kumhurumia, anawezaje kuwa na upendo wa Mungu ndani yake?+ 18  Watoto wadogo, tunapaswa kupendana, si kwa neno au kwa ulimi,+ bali kwa tendo+ na kweli.+ 19  Kwa jambo hili tutajua kwamba tunatokana na kweli, nasi tutaihakikishia* mioyo yetu mbele zake 20  kuhusu jambo lolote ambalo huenda mioyo yetu ikatuhukumu, kwa sababu Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua mambo yote.+ 21  Wapendwa, ikiwa mioyo yetu haituhukumu, tuna uhuru wa kusema na Mungu;+ 22  na chochote tunachoomba tunapokea kutoka kwake,+ kwa sababu tunazishika amri zake na tunafanya mambo yanayopendeza machoni pake. 23  Kwa kweli, hii ndiyo amri yake: kwamba tuwe na imani katika jina la Mwana wake Yesu Kristo+ na tupendane,+ kama vile alivyotupatia amri. 24  Zaidi ya hayo, mtu anayeshika amri zake hukaa katika muungano na yeye, na yeye katika muungano na mtu huyo.+ Na kupitia roho aliyotupatia, tunajua kwamba anakaa katika muungano pamoja nasi.+

Maelezo ya Chini

Au “aangamize.”
Au “tangu alipoanza.”
Yaani, mbegu inayoweza kuzaa, au inayotokeza matunda.
Au “nafsi yake.”
Au “nafsi zetu.”
Au “tutaishawishi; tutaisadikisha.”