Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 13:1-22

  • Abiya, mfalme wa Yuda (1-22)

    • Abiya amshinda Yeroboamu (3-20)

13  Katika mwaka wa 18 wa utawala wa Mfalme Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda.+  Alitawala kwa miaka mitatu huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Mikaya+ binti ya Urieli wa Gibea.+ Na kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.+  Basi Abiya akaenda vitani akiwa na jeshi lenye mashujaa hodari 400,000 waliozoezwa.*+ Na Yeroboamu akajipanga kivita ili kupigana naye akiwa na wanaume 800,000, mashujaa hodari waliozoezwa.*  Sasa Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika eneo lenye milima la Efraimu, akasema: “Nisikilizeni, Ee Yeroboamu na Waisraeli wote.  Je, hamjui kwamba Yehova Mungu wa Israeli alimpa Daudi ufalme juu ya Israeli milele,+ yeye na wanawe,+ kupitia agano la chumvi?*+  Lakini Yeroboamu+ mwana wa Nebati, mtumishi wa Sulemani mwana wa Daudi, akainuka na kumwasi bwana wake.+  Na wanaume wazembe, wasiofaa kitu wakaendelea kujiunga naye. Nao walimzidi maarifa Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana mchanga asiye na ujasiri, naye hangeweza kushindana nao.  “Na sasa mnafikiri kwamba mnaweza kushindana na ufalme wa Yehova ulio mikononi mwa wana wa Daudi kwa sababu ninyi ni umati mkubwa nanyi mna ndama wa dhahabu ambao Yeroboamu aliwatengenezea wawe miungu yenu.+  Je, hamjawafukuza makuhani wa Yehova,+ wazao wa Haruni, na Walawi, na je, hamjawaweka makuhani wenu wenyewe kama yalivyofanya mataifa ya nchi nyingine?+ Yeyote aliyeleta* ng’ombe dume mchanga na kondoo dume saba, angeweza kuwa kuhani wa vitu ambavyo si miungu. 10  Lakini sisi, Yehova ndiye Mungu wetu,+ nasi hatujamwacha; makuhani wetu, wazao wa Haruni, wanamhudumia Yehova, na Walawi wanawasaidia kazi. 11  Wanamfukizia Yehova moshi wa dhabihu za kuteketezwa kila asubuhi na kila jioni+ pamoja na uvumba uliotiwa manukato,+ na mikate ya tabaka*+ iko kwenye meza iliyotengenezwa kwa dhahabu safi, nao wanawasha kinara cha taa cha dhahabu+ na taa zake kila jioni,+ kwa sababu tunatekeleza jukumu letu kwa Yehova Mungu wetu; lakini ninyi mmemwacha. 12  Sasa tazama! Mungu wa kweli yuko pamoja nasi, akituongoza, na makuhani wake wakiwa na tarumbeta za kutoa ishara ya vita dhidi yenu. Enyi wanaume wa Israeli, msipigane na Yehova Mungu wa mababu zenu, kwa maana hamtafanikiwa.”+ 13  Lakini Yeroboamu alituma wanajeshi wawavizie kutoka nyuma, hivi kwamba jeshi lake lilikabili Yuda upande wa mbele na wanajeshi waliovizia walikuwa nyuma yao. 14  Wanaume wa Yuda walipogeuka, waligundua kwamba wanashambuliwa kutoka mbele na nyuma. Kwa hiyo wakaanza kumlilia Yehova,+ huku makuhani wakipiga tarumbeta kwa sauti kubwa. 15  Wanaume wa Yuda wakaanza kupiga kelele za vita, na wanaume hao wa Yuda walipopiga kelele za vita, Mungu wa kweli akamshinda Yeroboamu na Waisraeli wote mbele ya Abiya na Yuda. 16  Waisraeli wakawakimbia wanaume wa Yuda, na Mungu akawatia mikononi mwao. 17  Abiya na watu wake wakawachinja wanajeshi wengi, wakaendelea kuwaua wanajeshi wa Israeli, waliwaua wanaume 500,000 waliozoezwa.* 18  Basi wanaume wa Israeli wakanyenyekezwa wakati huo, lakini wanaume wa Yuda waliwashinda kwa sababu walimtegemea* Yehova Mungu wa mababu zao.+ 19  Abiya akaendelea kumfuatia Yeroboamu, akateka majiji yake, Betheli+ na miji yake, Yeshana na miji yake, na Efraini+ na miji yake. 20  Na Yeroboamu hakupata tena mamlaka* katika siku za Abiya; kisha Yehova akampiga, naye akafa.+ 21  Lakini Abiya akaendelea kupata nguvu. Baada ya muda akaoa wake 14,+ akazaa wana 22 na mabinti 16.⁠ 22  Na mambo mengine katika historia ya Abiya, mambo aliyotenda na kusema, yameandikwa katika maandishi ya* nabii Ido.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “waliochaguliwa.”
Tnn., “waliochaguliwa.”
Yaani, agano linalodumu na lisilobadilika.
Tnn., “aliyeujaza mkono wake na.”
Yaani, mikate ya wonyesho.
Tnn., “waliochaguliwa.”
Tnn., “walimwegemea.”
Tnn., “nguvu.”
Au “ufafanuzi wa; maelezo ya.”