Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 15:1-19

  • Mabadiliko yaliyofanywa na Asa (1-19)

15  Sasa roho ya Mungu ilimjia Azaria mwana wa Odedi.  Kwa hiyo akatoka kwenda kukutana na Asa, akamwambia: “Nisikilizeni, Asa na watu wote wa Yuda na Benjamini! Yehova yuko pamoja nanyi maadamu mnaendelea kuwa pamoja naye;+ nanyi mkimtafuta, atawaruhusu mumpate,+ lakini mkimwacha yeye atawaacha ninyi.+  Kwa muda mrefu* Waisraeli hawakuwa na Mungu wa kweli, hawakuwa na kuhani wa kuwafundisha, na hawakuwa na sheria.+  Lakini walipokuwa wakiteseka, walimrudia Yehova Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akawaruhusu wampate.+  Siku hizo hakuna yeyote aliyeweza kusafiri akiwa salama,* kwa sababu kulikuwa na misukosuko mingi miongoni mwa wakaaji wote wa nchi mbalimbali.  Taifa lilikuwa likipondwa na taifa lingine na jiji likipondwa na jiji lingine, kwa sababu Mungu aliwavuruga kwa kila aina ya mateso.+  Lakini ninyi, iweni imara na msivunjike moyo,*+ kwa maana mtapata thawabu kwa ajili ya kazi yenu.”  Mara tu Asa aliposikia maneno hayo na unabii wa nabii Odedi, akajipa ujasiri, akaondoa sanamu zenye kuchukiza katika nchi yote ya Yuda+ na Benjamini na katika majiji aliyokuwa ameteka katika eneo lenye milima la Efraimu, naye akajenga upya madhabahu ya Yehova iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Yehova.+  Akawakusanya pamoja watu wote wa Yuda na Benjamini na wakaaji wageni waliokuwa pamoja nao kutoka Efraimu na Manase na Simeoni,+ kwa maana walikuwa wamekimbia na kuja kwake kwa wingi kutoka Israeli walipoona kwamba Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye. 10  Basi wakakusanywa pamoja Yerusalemu katika mwezi wa tatu wa mwaka wa 15 wa utawala wa Asa. 11  Siku hiyo walimtolea Yehova dhabihu kutoka katika nyara walizoleta, ng’ombe 700 na kondoo 7,000. 12  Zaidi ya hayo, walifanya agano ili kumtafuta Yehova Mungu wa mababu zao kwa moyo wao wote na kwa nafsi* yao yote.+ 13  Mtu yeyote ambaye hangemtafuta Yehova Mungu wa Israeli angeuawa, awe mdogo au mkubwa, awe mwanamume au mwanamke.+ 14  Basi wakamwapia Yehova kwa sauti kubwa, kwa kelele za shangwe, na kwa tarumbeta na pembe. 15  Na watu wote wa Yuda wakashangilia kwa sababu ya kiapo hicho, kwa maana walikuwa wameapa kwa moyo wao wote, walimtafuta kwa bidii naye akawaruhusu wampate,+ na Yehova akaendelea kuwapumzisha pande zote.+ 16  Mfalme Asa alimwondoa hata Maaka+ nyanya yake kutoka katika cheo chake cha mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza sanamu chafu sana* kwa ajili ya ibada ya mti mtakatifu.*+ Asa akaikatakata sanamu hiyo chafu sana, akaipondaponda na kuiteketeza katika Bonde la Kidroni.+ 17  Lakini mahali pa juu hapakuondolewa+ Israeli.+ Hata hivyo, moyo wa Asa ulikuwa kamili* maisha yake yote.*+ 18  Naye alileta katika nyumba ya Mungu wa kweli vitu ambavyo yeye na baba yake walikuwa wamevifanya kuwa vitakatifu—fedha, dhahabu, na vyombo mbalimbali.+ 19  Hakukuwa na vita mpaka mwaka wa 35 wa utawala wa Asa.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “siku nyingi.”
Tnn., “hakukuwa na amani kwa yule aliyetoka nje au kuingia ndani.”
Tnn., “msilegeze mikono.”
Angalia Kamusi.
Yaani, kingono.
Angalia Kamusi.
Au “ulikuwa na ujitoaji kamili.”
Tnn., “siku zake zote.”