Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 19:1-11

  • Yehu amkemea Yehoshafati (1-3)

  • Mabadiliko yaliyofanywa na Yehoshafati (4-11)

19  Kisha Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama salimini+ katika nyumba yake* huko Yerusalemu.  Yehu+ mwana wa mwonaji Hanani+ alienda kukutana na Mfalme Yehoshafati na kumuuliza: “Je, unapaswa kuwasaidia waovu,+ na je, unapaswa kuwapenda wale wanaomchukia Yehova?+ Kwa sababu hiyo ghadhabu ya Yehova iko dhidi yako.  Hata hivyo, kuna mambo mema ambayo yamepatikana ndani yako,+ kwa sababu uliiondoa kabisa miti mitakatifu* nchini, nawe umeutayarisha moyo wako* kumtafuta Mungu wa kweli.”+  Yehoshafati akaendelea kuishi Yerusalemu, naye akatoka tena na kwenda kukutana na watu kuanzia Beer-sheba mpaka kwenye eneo lenye milima la Efraimu,+ ili awarudishe kwa Yehova Mungu wa mababu zao.+  Pia, aliwaweka waamuzi katika nchi yote, katika majiji yote ya Yuda yenye ngome, jiji baada ya jiji.+  Akawaambia hivi waamuzi: “Iweni waangalifu kuhusu mambo mnayotenda, kwa maana hamhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Yehova, naye yupo pamoja nanyi mnapotoa hukumu.+  Basi hofu ya Yehova na iwe juu yenu.+ Iweni waangalifu kuhusu mambo mnayotenda, kwa maana Yehova Mungu wetu hana ukosefu wa haki,+ hana ubaguzi,+ wala hapokei rushwa.”+  Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati aliwaweka baadhi ya Walawi na makuhani na baadhi ya viongozi wa koo* za Waisraeli watumikie wakiwa waamuzi kwa ajili ya Yehova na kusuluhisha kesi za wakaaji wa Yerusalemu.+  Akawaamuru: “Hivi ndivyo mnavyopaswa kufanya huku mkimwogopa Yehova, kwa uaminifu na kwa moyo kamili:* 10  Kila mara ndugu zenu wanaoishi katika majiji yao wakiwaletea kesi inayohusu umwagaji wa damu+ au swali kuhusu sheria fulani, amri, masharti, au maamuzi, mnapaswa kuwaonya ili wasiwe na hatia mbele za Yehova; msipofanya hivyo ghadhabu yake itakuja dhidi yenu na dhidi ya ndugu zenu. Hivyo ndivyo mnavyopaswa kufanya ili msiwe na hatia. 11  Ndiye huyu Amaria mkuu wa makuhani anayewasimamia katika kila jambo linalomhusu Yehova.+ Zebadia mwana wa Ishmaeli ndiye kiongozi wa ukoo wa Yuda katika kila jambo linalomhusu mfalme. Na Walawi watatumikia wakiwa maofisa wenu. Iweni imara, na mtende, na Yehova awe pamoja na wale wanaotenda mema.”*+

Maelezo ya Chini

Au “jumba lake la kifalme.”
Angalia Kamusi.
Au “na moyo wako umeazimia.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “moyo wenye ujitoaji kamili.”
Au “awe na kilicho chema.”