Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 22:1-12

  • Ahazia, mfalme wa Yuda (1-9)

  • Athalia anyakua ufalme (10-12)

22  Kisha wakaaji wa Yerusalemu wakamweka Ahazia mwanawe wa mwisho kuwa mfalme baada yake, kwa maana kundi la wavamizi lililokuja kambini pamoja na Waarabu lilikuwa limewaua wana wote wakubwa wa Yehoramu.+ Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu akaanza kutawala akiwa mfalme wa Yuda.+  Ahazia alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa mwaka mmoja huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Athalia+ mjukuu wa* Omri.+  Yeye pia alitembea katika njia za nyumba ya Ahabu,+ kwa maana mama yake alikuwa mshauri wake katika kutenda maovu.  Naye aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, kama watu wa nyumba ya Ahabu, kwa maana walikuwa washauri wake baada ya kifo cha baba yake, jambo lililofanya aangamie.⁠  Alifuata ushauri wao, akaenda pamoja na Yehoramu mwana wa Mfalme Ahabu wa Israeli kupigana vita na Mfalme Hazaeli+ wa Siria kule Ramothi-gileadi,+ ambako wapiga-mishale walimjeruhi Yehoramu.  Akarudi Yezreeli+ ili apone majeraha aliyopata kule Rama alipopigana na Mfalme Hazaeli wa Siria.+ Ahazia* mwana wa Yehoramu+ mfalme wa Yuda alishuka kwenda Yezreeli kumwona Yehoramu+ mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.*+  Lakini Mungu alisababisha Ahazia aangamie alipokuja kwa Yehoramu; na alipokuja, alienda pamoja na Yehoramu kukutana na Yehu+ mjukuu* wa Nimshi, ambaye Yehova alikuwa amemtia mafuta ili awaangamize kabisa watu wa nyumba ya Ahabu.+  Yehu alipoanza kutekeleza hukumu dhidi ya watu wa nyumba ya Ahabu, aliwapata wakuu wa Yuda na pia wana wa ndugu za Ahazia, wahudumu wa Ahazia, akawaua.+  Kisha akamtafuta Ahazia; wakamkamata mahali alipokuwa akijificha kule Samaria na kumleta kwa Yehu. Halafu wakamuua na kumzika,+ kwa maana walisema: “Yeye ni mjukuu wa Yehoshafati, aliyemtafuta Yehova kwa moyo wake wote.”+ Hapakuwa na mtu yeyote wa nyumba ya Ahazia aliyekuwa na mamlaka ya kutawala ufalme huo. 10  Athalia,+ mama ya Ahazia, alipoona kwamba mwanawe amekufa, alitoka na kuangamiza uzao wote wa kifalme* wa nyumba ya Yuda.+ 11  Hata hivyo, Yehoshabeathi binti ya mfalme alimchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia, akamwiba kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliopaswa kuuawa na kumweka yeye pamoja na mlezi wake katika chumba cha ndani cha kulala. Yehoshabeathi binti ya Mfalme Yehoramu+ (alikuwa mke wa kuhani Yehoyada+ na dada ya Ahazia) alifanikiwa kumficha ili Athalia asimwone, kwa hiyo hakumuua.+ 12  Akakaa pamoja nao kwa miaka sita, akiwa amefichwa katika nyumba ya Mungu wa kweli Athalia alipokuwa akiitawala nchi.

Maelezo ya Chini

Tnn., “binti ya.”
Anaitwa “Azaria,” katika baadhi ya hati za Kiebrania.
Au “alikuwa mgonjwa.”
Tnn., “mwana.”
Tnn., “mbegu yote ya ufalme.”