Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 23:1-21

  • Yehoyada aingilia kati; Yehoashi awekwa kuwa mfalme (1-11)

  • Athalia auawa (12-15)

  • Mabadiliko yaliyofanywa na Yehoyada (16-21)

23  Katika mwaka wa saba, Yehoyada alitenda kwa ujasiri na kufanya mapatano* na wakuu wa mamia,+ yaani, Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri.  Kisha wakazunguka katika nchi yote ya Yuda na kuwakusanya pamoja Walawi+ kutoka katika majiji yote ya Yuda na viongozi wa koo* za Waisraeli. Walipofika Yerusalemu,  kutaniko lote lilifanya agano+ pamoja na mfalme katika nyumba ya Mungu wa kweli, kisha akawaambia: “Tazama! Mwana wa mfalme atatawala, kama Yehova alivyoahidi kuhusu wana wa Daudi.+  Hivi ndivyo mtakavyofanya: Theluthi moja ya makuhani na ya Walawi watakaoshika zamu+ siku ya Sabato watalinda malango;+  na theluthi nyingine watakuwa katika nyumba ya* mfalme,+ na theluthi nyingine watakuwa katika Lango la Msingi, na watu wote watakuwa katika nyua za nyumba ya Yehova.+  Msimruhusu mtu yeyote aingie katika nyumba ya Yehova isipokuwa makuhani na Walawi wanaohudumu.+ Hao wanaweza kuingia kwa sababu ni kikundi kitakatifu, na watu wote watatimiza wajibu kwa Yehova.  Walawi wanapaswa kumzunguka mfalme pande zote, kila mmoja akiwa na silaha zake mikononi mwake. Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo atauawa. Mfuateni mfalme popote aendapo.”*  Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya sawasawa na alivyoamuru kuhani Yehoyada. Basi kila mmoja wao akachukua wanaume wake waliokuwa na zamu siku ya Sabato, pamoja na wale ambao hawakuwa na zamu siku ya Sabato,+ kwa maana kuhani Yehoyada hakuwa ameviruhusu vikundi+ vilivyoshika zamu viondoke.  Kisha kuhani Yehoyada akawapa wakuu wa mamia+ mikuki na ngao ndogo* na ngao za mviringo zilizokuwa za Mfalme Daudi,+ ambazo zilikuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli.+ 10  Halafu akawaweka watu wote, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi, kuanzia upande wa kulia wa nyumba mpaka upande wa kushoto wa nyumba, kando ya madhabahu na kando ya nyumba hiyo, kumzunguka mfalme pande zote. 11  Kisha wakamtoa nje mwana wa mfalme+ na kumvika taji na Ushahidi,*+ wakamweka kuwa mfalme, ndipo Yehoyada na wanawe wakamtia mafuta. Halafu wakasema: “Mfalme na aishi muda mrefu!”+ 12  Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia na kumsifu mfalme, mara moja akaja na kujiunga na watu katika nyumba ya Yehova.+ 13  Kisha akamwona mfalme akiwa amesimama hapo karibu na nguzo ya mfalme karibu na lango. Wakuu+ na wapiga tarumbeta walikuwa na mfalme, na watu wote nchini walikuwa wakishangilia+ na kupiga tarumbeta, na waimbaji wakiwa na ala za muziki waliongoza katika kutoa sifa.* Ndipo Athalia akayararua mavazi yake na kupaza sauti: “Ni njama! Ni njama!” 14  Lakini kuhani Yehoyada akawatoa nje wakuu wa mamia, wale waliowekwa kulisimamia jeshi, akawaambia: “Mwondoeni miongoni mwa vikosi, na yeyote akimfuata, muueni kwa upanga!” Kwa maana kuhani alikuwa amesema: “Msimuue ndani ya nyumba ya Yehova.” 15  Basi wakamkamata, na alipofika njia ya kuingia katika Lango la Farasi la nyumba ya* mfalme, mara moja wakamuua hapo. 16  Kisha Yehoyada akafanya agano kati yake na watu wote na mfalme, kwamba wataendelea kuwa watu wa Yehova.+ 17  Baada ya hayo, watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Baali na kuibomoa,*+ wakavunja vipandevipande madhabahu zake na sanamu zake,+ nao wakamuua Matani kuhani wa Baali+ mbele ya madhabahu. 18  Kisha Yehoyada akaweka usimamizi wa nyumba ya Yehova mikononi mwa makuhani na Walawi, ambao Daudi alikuwa amewapanga katika vikundi wahudumu katika nyumba ya Yehova na kutoa dhabihu za kuteketezwa za Yehova+ kulingana na yale yaliyoandikwa katika Sheria ya Musa,+ wakishangilia na kuimba, kama alivyoagiza* Daudi. 19  Aliwaweka pia walinzi wa malango+ karibu na malango ya nyumba ya Yehova, ili mtu yeyote asiye safi kwa njia yoyote ile asiingie. 20  Kisha akawachukua wakuu wa mamia,+ watu mashuhuri, watawala wa watu, na watu wote nchini, wakamsindikiza mfalme kushuka kutoka katika nyumba ya Yehova. Halafu wakaja katika nyumba ya* mfalme kupitia lango la juu na kumweka mfalme kwenye kiti+ cha ufalme.+ 21  Basi watu wote nchini wakashangilia na jiji likatulia, kwa maana walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga.

Maelezo ya Chini

Au “agano.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “jumba la.”
Tnn., “anapotoka nje na anapoingia ndani.”
Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Labda ni kitabu cha kukunjwa kilichokuwa na Sheria ya Mungu.
Au “walitoa ishara ya kutoa sifa.”
Au “jumba la.”
Au “hekalu la Baali na kulibomoa.”
Tnn., “kwa mikono ya.”
Au “jumba la.”