Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 27:1-9

  • Yothamu, mfalme wa Yuda (1-9)

27  Yothamu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yerusha binti ya Sadoki.+  Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, kama alivyotenda Uzia baba yake,+ ila tu hakuingia kwa nguvu katika hekalu la Yehova.+ Lakini bado watu walikuwa wakitenda maovu.  Alijenga lango la juu la nyumba ya Yehova,+ naye alifanya kazi kubwa ya ujenzi kwenye ukuta wa Ofeli.+  Alijenga pia majiji+ katika eneo lenye milima la Yuda,+ akajenga ngome+ na minara+ misituni.  Alipigana vita na mfalme wa Waamoni+ na hatimaye akawashinda, hivi kwamba mwaka huo Waamoni wakampa talanta 100 za fedha,* kori 10,000 za ngano,* na 10,000 za shayiri. Waamoni walimlipa vitu hivyo katika mwaka wa pili na wa tatu pia.+  Basi Yothamu akaendelea kupata nguvu, kwa maana aliziimarisha* njia zake mbele za Yehova Mungu wake.  Na mambo mengine katika historia ya Yothamu, vita vyake vyote na njia zake, yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na wa Yuda.+  Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu.+  Kisha Yothamu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ Na Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.+

Maelezo ya Chini

Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Kori moja ilikuwa sawa na lita 220 (kilogramu 170 hivi). Angalia Nyongeza B14.
Au “alizitayarisha.”