Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 33:1-25

  • Manase, mfalme wa Yuda (1-9)

  • Manase atubu uovu wake (10-17)

  • Kifo cha Manase (18-20)

  • Amoni, mfalme wa Yuda (21-25)

33  Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 55 huko Yerusalemu.+  Alitenda maovu machoni pa Yehova, akafuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.+  Alijenga upya mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akajenga madhabahu kwa ajili ya Mabaali na kutengeneza miti mitakatifu,* naye akaliinamia jeshi lote la mbinguni na kuliabudu.+  Alijenga pia madhabahu katika nyumba ya Yehova,+ ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Nitaweka jina langu Yerusalemu milele.”+  Naye alijenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+  Na pia aliwateketeza* motoni wanawe mwenyewe+ katika Bonde la Mwana wa Hinomu;+ alifanya uchawi,+ alifanya uaguzi,* alifanya ulozi, na kuwaweka rasmi watu wanaowasiliana na roho na wabashiri.+ Alitenda kwa kiwango kikubwa sana mambo maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.  Sanamu aliyokuwa amechonga aliiweka katika nyumba ya Mungu wa kweli+ ambayo Mungu alikuwa amemwambia hivi Daudi na Sulemani mwanawe kuihusu: “Nitaweka jina langu milele katika nyumba hii na katika jiji la Yerusalemu, ambalo nimelichagua kati ya makabila yote ya Israeli.+  Ikiwa Waisraeli watashika kwa uangalifu mambo yote niliyowaamuru, Sheria yote, masharti na amri nilizowapa* kupitia Musa mtumishi wangu, sitaiondoa tena kamwe miguu yao katika nchi niliyowapa mababu zao.”  Manase aliendelea kuwapotosha watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, akasababisha watende mambo maovu zaidi kuliko mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya Waisraeli.+ 10  Yehova aliendelea kuzungumza na Manase na watu wake, lakini hawakumsikiliza.+ 11  Kwa hiyo Yehova akawaleta wakuu wa jeshi la mfalme wa Ashuru ili wawashambulie, nao wakamkamata Manase kwa kulabu* na kumfunga kwa pingu mbili za shaba na kumpeleka Babiloni. 12  Alipokuwa akiteseka, alimsihi* Yehova Mungu wake amwonyeshe kibali, naye akaendelea kujinyenyekeza sana mbele za Mungu wa mababu zake. 13  Aliendelea kusali kwa Mungu, naye akaguswa na sala yake ya kusihi, akasikia ombi lake la kutaka kibali, akamrudisha Yerusalemu kwenye ufalme wake.+ Ndipo Manase akajua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+ 14  Baada ya hayo alijenga ukuta wa nje wa Jiji la Daudi+ upande wa magharibi wa Gihoni,+ bondeni,* na mpaka kwenye Lango la Samaki,+ akauzungusha hadi Ofeli,+ na kuufanya uwe mrefu sana. Zaidi ya hayo, aliwaweka wakuu wa jeshi katika majiji yote yenye ngome nchini Yuda. 15  Kisha akaondoa katika nyumba ya Yehova+ miungu ya kigeni na ile sanamu iliyochongwa na pia madhabahu zote alizokuwa amejenga kwenye mlima wa nyumba ya Yehova+ na Yerusalemu, akaagiza vitu hivyo vitupwe nje ya jiji. 16  Aliitayarisha pia madhabahu ya Yehova,+ akaanza kutoa juu yake dhabihu za ushirika+ na dhabihu za shukrani,+ naye akawaambia watu wa Yuda wamtumikie Yehova Mungu wa Israeli. 17  Hata hivyo, bado watu walikuwa wakitoa dhabihu mahali pa juu, ila tu sasa walimtolea Yehova Mungu wao. 18  Na mambo mengine katika historia ya Manase, sala aliyotoa kwa Mungu wake, na maneno ya waonaji waliozungumza naye katika jina la Yehova Mungu wa Israeli, yameandikwa katika historia ya wafalme wa Israeli. 19  Pia sala yake+ na jinsi ombi lake lilivyojibiwa, dhambi zake zote na jinsi alivyokosa kuwa mwaminifu,+ sehemu alizojenga mahali pa juu na kusimamisha miti mitakatifu*+ na sanamu za kuchongwa kabla hajajinyenyekeza, mambo hayo yameandikwa katika maandishi ya waonaji wake. 20  Kisha Manase akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake nyumbani kwake; na Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.+ 21  Amoni+ alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka miwili huko Yerusalemu.+ 22  Naye aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, kama alivyofanya Manase baba yake;+ na Amoni akatoa dhabihu kwa sanamu zote za kuchongwa ambazo Manase baba yake alikuwa ametengeneza,+ naye akaendelea kuziabudu. 23  Lakini hakujinyenyekeza mbele za Yehova+ kama Manase baba yake alivyojinyenyekeza;+ badala yake, Amoni alizidisha sana hatia yake. 24  Hatimaye watumishi wake wakapanga njama dhidi yake+ na kumuua ndani ya nyumba yake mwenyewe. 25  Lakini watu wa nchi hiyo wakawaua wale wote waliopanga njama dhidi ya Mfalme Amoni,+ nao wakamweka Yosia mwanawe+ kuwa mfalme baada yake.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “alibashiri.”
Tnn., “aliwapitisha.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu niliyowapa.”
Au labda, “mashimoni.”
Au “aliutuliza uso wa Yehova Mungu wake.”
Au “kwenye korongo.”
Angalia Kamusi.