Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 35:1-27

  • Yosia apanga Pasaka kubwa (1-19)

  • Farao Neko amuua Yosia (20-27)

35  Yosia alifanya sherehe ya Pasaka+ ya Yehova huko Yerusalemu, nao wakamchinja mnyama wa Pasaka+ katika siku ya 14 ya mwezi wa kwanza.+  Aliwaweka makuhani katika zamu zao na kuwatia moyo watekeleze utumishi wao wa nyumba ya Yehova.+  Kisha akawaambia hivi Walawi, walimu wa Waisraeli wote,+ waliokuwa watakatifu kwa Yehova: “Liwekeni Sanduku takatifu ndani ya nyumba ambayo Sulemani mwana wa Daudi mfalme wa Israeli alijenga;+ hampaswi kulibeba tena mabegani mwenu.+ Sasa mtumikieni Yehova Mungu wenu na watu wake Waisraeli.  Na mjitayarishe kulingana na koo zenu,* kulingana na vikundi vyenu, mkifuata mambo yaliyoandikwa na Mfalme Daudi+ wa Israeli na Sulemani mwanawe.+  Simameni mahali patakatifu mkiwa katika vikundi kulingana na koo* za ndugu zenu, ambao si Walawi,* pamoja na kikundi kinacholingana cha ukoo* wa Walawi.  Mchinjeni mnyama wa Pasaka+ na mjitakase na kufanya matayarisho kwa ajili ya ndugu zenu ili kutekeleza neno la Yehova kupitia Musa.”  Yosia akawachangia watu wote waliokuwepo makundi ya kondoo na mbuzi, wanakondoo dume na wanambuzi dume, kwa ajili ya dhabihu za Pasaka, jumla ya wanakondoo na wanambuzi 30,000, na pia ng’ombe 3,000. Wanyama hao walitolewa katika mali za mfalme mwenyewe.+  Wakuu wake pia walitoa mchango uwe toleo la hiari kwa ajili ya watu, makuhani, na Walawi. Hilkia,+ Zekaria, na Yehieli, viongozi wa nyumba ya Mungu wa kweli, waliwapa makuhani wanyama 2,600 wa dhabihu za Pasaka na ng’ombe 300.  Konania na ndugu zake Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli, na Yozabadi, wakuu wa Walawi, waliwapa Walawi wanyama 5,000 wa dhabihu za Pasaka pamoja na ng’ombe 500 kuwa mchango. 10  Matayarisho ya utumishi huo yakafanywa, na makuhani wakasimama mahali pao na Walawi wakasimama kulingana na vikundi vyao,+ kama mfalme alivyokuwa ameamuru. 11  Wakawachinja wanyama wa Pasaka,+ na makuhani wakanyunyiza damu waliyopokea kutoka kwao,+ huku Walawi wakiwachuna ngozi wanyama hao.+ 12  Kisha wakatayarisha dhabihu za kuteketezwa ili kuwagawia watu wasio Walawi, ambao walikuwa wamepangwa kulingana na koo zao,* ili zitolewe kwa Yehova kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa; wakafanya vivyo hivyo kwa wale ng’ombe. 13  Waliipika* dhabihu ya Pasaka juu ya moto kulingana na desturi;+ nao wakapika matoleo matakatifu kwenye vyungu, sufuria kubwa, na vikaangio, kisha wakawaletea haraka watu wengine wote. 14  Kisha wakaitayarisha kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu makuhani, wazao wa Haruni, walikuwa wakitoa dhabihu za kuteketezwa na vipande vyenye mafuta mpaka giza lilipoingia, kwa hiyo Walawi wakaitayarisha kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, wazao wa Haruni. 15  Na waimbaji, wana wa Asafu,+ walisimama mahali pao kama alivyoamuru Daudi,+ Asafu,+ Hemani, na Yeduthuni,+ mwonaji wa mfalme; na walinzi wa malango walikuwa kwenye malango mbalimbali.+ Hawakuhitaji kuacha utumishi wao, kwa sababu ndugu zao Walawi walikuwa wamewatayarishia Pasaka. 16  Kwa hiyo utumishi wote wa Yehova ukatayarishwa siku hiyo ili kuadhimisha Pasaka+ na kutoa dhabihu za kuteketezwa kwenye madhabahu ya Yehova, kulingana na agizo la Mfalme Yosia.+ 17  Waisraeli waliokuwepo waliadhimisha Pasaka wakati huo na pia Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu kwa siku saba.+ 18  Pasaka kama hiyo haikuwa imewahi kuadhimishwa Israeli tangu siku za nabii Samweli; wala wafalme wengine wa Israeli hawakuwa wameadhimisha Pasaka kama hiyo iliyoadhimishwa na Yosia,+ makuhani, Walawi, watu wote wa Yuda na Israeli waliokuwepo, na wakaaji wa Yerusalemu. 19  Pasaka hii ilifanywa katika mwaka wa 18 wa utawala wa Yosia. 20  Baada ya hayo yote, Yosia alipokuwa ametayarisha hekalu,* Mfalme Neko+ wa Misri alipanda kuja kupigana Karkemishi karibu na Mto Efrati. Kisha Yosia akaenda kukabiliana naye.+ 21  Kwa hiyo akamtumia Yosia wajumbe, akisema: “Vita hivi vinakuhusuje, Ee mfalme wa Yuda? Sijaja kupigana nawe leo, nimekuja kupigana na nyumba nyingine, na Mungu anasema kwamba ninapaswa kufanya haraka. Kwa faida yako mwenyewe, acha kumpinga Mungu, aliye pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.” 22  Hata hivyo, Yosia hakugeuka na kumwacha, lakini alibadili sura yake+ ili apigane naye, akakataa kabisa kusikiliza maneno ya Neko, yaliyotoka kinywani mwa Mungu. Basi akaja kupigana naye katika Nchi Tambarare ya Megido.+ 23  Na wapiga mishale wakampiga Mfalme Yosia, akawaambia watumishi wake: “Niondoeni hapa, kwa maana nimejeruhiwa vibaya sana.” 24  Kwa hiyo watumishi wake wakamtoa garini, wakamweka kwenye gari lake la pili la vita na kumpeleka Yerusalemu. Kwa hiyo akafa na kuzikwa katika kaburi la mababu zake,+ na watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia. 25  Na Yeremia+ akamwimbia Yosia wimbo wa maombolezo, na tangu siku hiyo waimbaji wote wa kiume na wa kike+ wanaendelea kuimba kumhusu Yosia katika nyimbo zao za huzuni;* na uamuzi ukafanywa kwamba nyimbo hizo zinapaswa kuimbwa katika nchi ya Israeli, nazo zimeandikwa katika nyimbo za huzuni. 26  Na mambo mengine katika historia ya Yosia na matendo yake ya upendo mshikamanifu, kulingana na mambo yaliyoandikwa katika Sheria ya Yehova, 27  na mambo aliyofanya, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na wa Yuda.+

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “wana wa watu.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au labda, “Waliichoma.”
Tnn., “nyumba.”
Au “maombolezo.”