Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 4:1-22

  • Madhabahu, Bahari, na mabeseni (1-6)

  • Vinara vya taa, meza, na nyua (7-11a)

  • Vyombo vyote vya hekalu vyakamilishwa (11b-22)

4  Kisha akatengeneza madhabahu ya shaba+ yenye urefu wa mikono 20, upana wa mikono 20, na kimo cha mikono 10.  Alitengeneza Bahari*+ kwa madini yaliyoyeyushwa. Ilikuwa ya mviringo, yenye upana wa mikono 10 ukingo hadi ukingo na kimo cha mikono 5, na ingeweza kuzungukwa na kamba yenye urefu wa mikono 30.+  Na chini yake kulikuwa na mapambo ya vibuyu,+ ambayo yalizunguka ukingo wote, vibuyu kumi kwa kila mkono mmoja kuzunguka Bahari yote. Vibuyu hivyo vilikuwa katika safu mbili, navyo vilitengenezwa kwa kuyeyushwa vikiwa sehemu ya Bahari hiyo.  Ilikuwa juu ya ng’ombe dume 12,+ watatu walitazama kaskazini, watatu walitazama magharibi, watatu walitazama kusini, na watatu walitazama mashariki; na Bahari hiyo ilikuwa juu yao, na sehemu zao zote za nyuma zilielekea katikati.  Na unene wake ulikuwa upana wa kiganja kimoja;* na ukingo wake ulitengenezwa kama ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi. Ingeweza kujaa maji kiasi cha bathi 3,000.*  Pia, alitengeneza mabeseni kumi ya kuoshea, akaweka matano upande wa kulia na matano upande wa kushoto.+ Waliyatumia kuoshea vitu vilivyotumiwa kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.+ Lakini Bahari ilitumiwa na makuhani kuogea.+  Kisha alitengeneza vinara kumi vya taa vya dhahabu,+ kulingana na maagizo,+ akaviweka hekaluni, vitano upande wa kulia na vitano upande wa kushoto.+  Alitengeneza pia meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kulia na tano upande wa kushoto;+ naye alitengeneza mabakuli 100 ya dhahabu.  Kisha akatengeneza ua+ wa makuhani+ na ule ua mkuu+ na milango ya ua huo, akaifunika milango hiyo kwa shaba. 10  Akaiweka ile Bahari upande wa kulia, kuelekea kusini mashariki.+ 11  Hiramu alitengeneza pia ndoo za kuondolea majivu, pia sepetu, na mabakuli.+ Basi Hiramu akamaliza kazi yote aliyomfanyia Mfalme Sulemani kuhusiana na nyumba ya Mungu wa kweli:+ 12  zile nguzo mbili+ na vifuniko vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; na nyavu mbili+ za kufunika vifuniko hivyo viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; 13  yale makomamanga 400+ kwa ajili ya zile nyavu mbili, safu mbili za makomamanga kwa ajili ya kila wavu, ili kufunika vile vifuniko viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya zile nguzo;+ 14  yale magari* kumi na yale mabeseni kumi yaliyokuwa juu ya magari hayo;+ 15  ile Bahari na wale ng’ombe dume 12 waliokuwa chini yake;+ 16  na ndoo za kuondolea majivu, sepetu, nyuma,*+ na vyombo vingine vyote ambavyo Hiram-abivu+ alimtengenezea Mfalme Sulemani kwa shaba iliyong’arishwa kwa ajili ya nyumba ya Yehova. 17  Mfalme alivitengeneza katika kalibu za udongo wa mfinyanzi katika wilaya ya Yordani kwenye eneo lenye udongo mwingi wa mfinyanzi, kati ya Sukothi+ na Sarethani. 18  Sulemani alitengeneza vyombo hivyo vyote kwa wingi sana; uzito wa shaba haukujulikana.+ 19  Sulemani alivitengeneza vitu vyote+ vya nyumba ya Mungu wa kweli: madhabahu ya dhahabu;+ meza+ na mikate ya wonyesho iliyokuwa juu ya meza hizo;+ 20  vinara vya taa na taa zake za dhahabu safi,+ ili ziwake mbele ya chumba cha ndani zaidi kulingana na maagizo; 21  na maua, taa, na koleo, vyote vya dhahabu, dhahabu safi kabisa; 22  mikasi ya kukatia tambi za taa, mabakuli, vikombe, na vyetezo, vyote vya dhahabu safi; na lango la nyumba, na milango ya ndani ya Patakatifu Zaidi,+ na milango ya nyumba ya hekalu, ya dhahabu.+

Maelezo ya Chini

Au “tangi.”
Karibu sentimita 7.4 (inchi 2.9). Angalia Nyongeza B14.
Bathi ilikuwa sawa na lita 22. Angalia Nyongeza B14.
Au “mikokoteni kumi ya maji.”
Wingi wa kifaa kinachoitwa uma.